Kila tarehe 22 ya Mwezi Septemba, nchi ya Mali inaadhimisha siku ya uhuru, ambapo kwa mwaka huu 2023, Kikosi tawala cha Mali, kimefutilia mbali sherehe zilizopangwa kuadhimisha kumbukumbu ya uhuru huo, kufuatia kuongezeka kwa wasiwasi wa mashambulizi yaliyotokea Kaskazini mwa nchi hiyo.
Nchi ya Mali ilipata uhuru wake kutoka kwa Mfaransa mwaka 1960 tarehe na mwezi kama huu.
Tangazo hilo lilitolewa kwenye baraza la mawaziri wa nchi hiyo.
Mwaka jana, kiongozi wa kijeshi wa Guinea alihudhuria gwaride la kijeshi lililoandaliwa kwa ajili ya sherehe za maadhimisho ya miaka 62 ya uhuru wa Mali.
Wakati wa baraza la mawaziri, kiongozi wa kijeshi wa Mali aliamuru serikali kutenga fedha zilizopangwa kwa sherehe za mwaka huu kusaidia wahasiriwa wa safu ya mashambulio ya hivi majuzi na familia zao.
Baraza pia lilijadili uwezekano wa uhamasishaji wa askari wa akiba.
Mali ilitumbukia katika machafuko mwaka 2012 baada ya watu wanaotaka kujitenga na maasi ya Kiislamu kuzuka kaskazini. Na mpaka sasa kumekuwa na vikundi jihad ambavyo vinahusishwa kuwa na uhusiano wa moja kwa moja na Al-Qaida kama Jihadist Alliance Support Group for Islam and Muslim ambacho kwa kifupi uitwa GSIM (Group to Support Islam and Muslims)
Ndio itasaidia Nchi ya Mali kupiga hatua kimaendeleo?Mimi binafsi naonaga sherehe za uhuru zimebaki Afrika tu. Nchi nyingi kubwa haziazimishi sherehe za uhuru, zinatakiwa kufutwa, au kubadilishwa kuwa sherehe za maonesho ya kivita. Hata mwenge wa uhuru ufutwe.
Mwendazake hakufuta sherehe, yeye alikuwa anasema pesa zipelekwe kwingineko kwa ajili ya maendeleo kwa maana siku hiyo utumia pesa nyingi ambapo sherehe yenyewe haina faida kwa jamii. Huyu wa Mali kafuta kabisa.Ndio itasaidia Nchi ya Mali kupiga hatua kimaendeleo?
Hizo ni mentality za ma failures kujaribu kujitafutia umaarufu baada ya kuharibu.
Mwendazake alifuta sana Je iliondoa matatizo Kwa watu? Ujinga.
Pesa nyingi zipi hata mil.500 haifikiMwendazake hakufuta sherehe, yeye alikuwa anasema pesa zipelekwe kwingineko kwa ajili ya maendeleo kwa maana siku hiyo utumia pesa nyingi ambapo sherehe yenyewe haina faida kwa jamii. Huyu wa Mali kafuta kabisa.
Nikuulize wewe, sherehe za uhuru zimekusaidia nini au zimesaidia je Tanzania?
Ina uwingi gani Sasa hiyo? Hizo pesa si Vijana wadogo wamekaa mtaani wanazo?Acha kauli za kifisadi, Kwa hiyo we unaona Mil 500 sio pesa nyingi au sio....
Hiyo pesa inajenga madarasa mangapi hapa bongo?
Mimi binafsi naonaga sherehe za uhuru zimebaki Afrika tu. Nchi nyingi kubwa haziazimishi sherehe za uhuru, zinatakiwa kufutwa, au kubadilishwa kuwa sherehe za maonesho ya kivita. Hata sherehe za mwenge wa uhuru zifutwe, mwenge ukakae makumbusho.
Uongo, USA, taifa kubwa kabisa linasherehekeaMimi binafsi naonaga sherehe za uhuru zimebaki Afrika tu. Nchi nyingi kubwa haziazimishi sherehe za uhuru, zinatakiwa kufutwa, au kubadilishwa kuwa sherehe za maonesho ya kivita. Hata sherehe za mwenge wa uhuru zifutwe, mwenge ukakae makumbusho.