Dingswayo
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 4,019
- 2,923
Malecela-CCM isihusishwe na ufisadi
Na Waandishi wetu
30th August 2010
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM), John Samwel Malecela
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM), John Samwel Malecela, amesema kamwe CCM kisihusishwe na ufisadi kwa kuwa kimeonyesha jitihada kubwa za kulishughulikia tatizo hilo.
Malecela alitoa kauli hiyo juzi katika viwanja vya Mwembetogwa mjini Iringa, wakati wa uzinduzi wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu Mkoa wa Iringa. Malecela alilazimika kuyasema hayo katika uwanja huo wakati akijibu hoja za wapinzani ambao alidai kuwa ajenda yao kubwa katika kampeni ni madai ya kuwepo kwa ufisadi ndani ya CCM.
Wapinzani wetu watakuja hapa na nataka niwaambie wananchi wa Iringa kwamba, hoja yao kubwa watakayokuja nayo ni kwamba CCM ni mafisadi, lakini watambue kuwa ufisadi upo duniani kote na si Tanzania tu, alisema.
Malecela alisema ufisadi ni jambo ambalo linaitesa kila nchi duniani ikiwemo Tanzania, lakini jambo la muhimu ni jinsi ambavyo serikali inayoongozwa na CCM.
Mafisadi ni sawa na majambazi hivyo wasihusishwe na CCM. Serikali yake na hata shughuli zingine zozote zinazofanywa kwa niaba ya CCM, jamani si sahihi kusema kwamba CCM ni mafisadi, alionya.
Alisema kwa kutambua hilo, Serikali ya CCM imeimarisha mahakama na kwamba watuhumiwa wa ufisadi wamepelekwa huko ili kujibu mashitaka yanayowakabili.
Serikali ya CCM ni ya utawala bora na wa haki inayofuata utawala wa sheria, sasa wanaotaka kila anayetajwa kuwa ni fisadi tumshughukie kama wanavyotaka wao, itakuwa siyo kutenda haki, tumewaachia mahakama, alisema.
Hata hivyo, alikiri kwamba CCM haijamaliza matatizo yote ya wananchi, lakini akadai kwamba ndicho chama ambacho kina mwelekeo mzuri na mikakati inayotekelezeka kuendelea kushughulikia kero za wananchi.
Pia, alikiri kwamba rasilimali za nchi hususani madini kutomnufaisha mwananchi wa kawaida awali, lakini Serikali iligundua na kuunda kamati ambayo ilitoa mapendekezo mazuri yaliyopelekea kutungwa kwa sheria nzuri ya usimamizi wa madini ambayo itawafanya wananchi wanufaike nayo.
Malecela pia alitumia muda huo kuzungumzia mgogoro ndani ya CCM Wilaya ya Iringa mjini ulioibuka baada ya Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) kuondoa jina la Mgombea aliyeongoza kwenye kura za maoni, Frederick Mwakalebela.
Imeandikwa na Mawazo Malembeka na Godfrey Mushi, Iringa.
CHANZO: NIPASHE
Serikali ya Tanzania ni ya chama kimoja, na watendaji wake ni wanachama wakuu. Ni vipi unaweza lutenganisha hivi viwili? Hata ushahidi unaonekana kuwa wahusika wakubwa katika ufisadi ni hao hao viongozi waliopo ccm. Haihitaji akili nyingi kujua kuwa uongozi wa ccm ni chanzo cha ufisadi na kinaendeleza na kukumbatia ufisadi. ccm=UFISADI.
Na Waandishi wetu
30th August 2010
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM), John Samwel Malecela
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM), John Samwel Malecela, amesema kamwe CCM kisihusishwe na ufisadi kwa kuwa kimeonyesha jitihada kubwa za kulishughulikia tatizo hilo.
Malecela alitoa kauli hiyo juzi katika viwanja vya Mwembetogwa mjini Iringa, wakati wa uzinduzi wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu Mkoa wa Iringa. Malecela alilazimika kuyasema hayo katika uwanja huo wakati akijibu hoja za wapinzani ambao alidai kuwa ajenda yao kubwa katika kampeni ni madai ya kuwepo kwa ufisadi ndani ya CCM.
Wapinzani wetu watakuja hapa na nataka niwaambie wananchi wa Iringa kwamba, hoja yao kubwa watakayokuja nayo ni kwamba CCM ni mafisadi, lakini watambue kuwa ufisadi upo duniani kote na si Tanzania tu, alisema.
Malecela alisema ufisadi ni jambo ambalo linaitesa kila nchi duniani ikiwemo Tanzania, lakini jambo la muhimu ni jinsi ambavyo serikali inayoongozwa na CCM.
Mafisadi ni sawa na majambazi hivyo wasihusishwe na CCM. Serikali yake na hata shughuli zingine zozote zinazofanywa kwa niaba ya CCM, jamani si sahihi kusema kwamba CCM ni mafisadi, alionya.
Alisema kwa kutambua hilo, Serikali ya CCM imeimarisha mahakama na kwamba watuhumiwa wa ufisadi wamepelekwa huko ili kujibu mashitaka yanayowakabili.
Serikali ya CCM ni ya utawala bora na wa haki inayofuata utawala wa sheria, sasa wanaotaka kila anayetajwa kuwa ni fisadi tumshughukie kama wanavyotaka wao, itakuwa siyo kutenda haki, tumewaachia mahakama, alisema.
Hata hivyo, alikiri kwamba CCM haijamaliza matatizo yote ya wananchi, lakini akadai kwamba ndicho chama ambacho kina mwelekeo mzuri na mikakati inayotekelezeka kuendelea kushughulikia kero za wananchi.
Pia, alikiri kwamba rasilimali za nchi hususani madini kutomnufaisha mwananchi wa kawaida awali, lakini Serikali iligundua na kuunda kamati ambayo ilitoa mapendekezo mazuri yaliyopelekea kutungwa kwa sheria nzuri ya usimamizi wa madini ambayo itawafanya wananchi wanufaike nayo.
Malecela pia alitumia muda huo kuzungumzia mgogoro ndani ya CCM Wilaya ya Iringa mjini ulioibuka baada ya Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) kuondoa jina la Mgombea aliyeongoza kwenye kura za maoni, Frederick Mwakalebela.
Imeandikwa na Mawazo Malembeka na Godfrey Mushi, Iringa.
CHANZO: NIPASHE
Serikali ya Tanzania ni ya chama kimoja, na watendaji wake ni wanachama wakuu. Ni vipi unaweza lutenganisha hivi viwili? Hata ushahidi unaonekana kuwa wahusika wakubwa katika ufisadi ni hao hao viongozi waliopo ccm. Haihitaji akili nyingi kujua kuwa uongozi wa ccm ni chanzo cha ufisadi na kinaendeleza na kukumbatia ufisadi. ccm=UFISADI.