Wamezoea, Mzee Malecela anajiamini sana, tena siku hizi ni nadra sana akasikika anajenga hoja, anajisemea tu maana anaamini neno lake litapokelewa bila kuguswa. Tumsamehe tu!!!
Ila kuna kitu ambacho sijakielewa bado; hawa wananchi ndugu zetu huko vijijini, ni nini kinawatuma kwenda kuwasikiliza hawa watu miaka nenda rudi, hadithi ni zile zile, maisha ni yale yale, watu ni wale wale, lakini bado tu wanajitokeza kuwasikiliza. Ni mahali gani tunakosea! Kwa nini wakiambiwa mapya wanasita!
Tunahitaji programu za radio zaidi, magazeti hayawezi kwani ni lazima wayanunue na hawana hela, ni lazima wayasome na wengi wao hawajui tena kusoma (elimu ya ngumbaru ilikufa na Nyerere), wengine wanajua kusoma lakini wana shida ya macho na huko vijijini hakuna kliniki za macho, na Aga Khani hawajaweza kutembelea kote.
Mungu wabariki wanakijiji wetu wote!