Katibu Mkuu anayekifaa CCM ni aliyekitumikia TANU kwa wadhifa andamizi

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Sep 20, 2021
3,214
3,587
CCM kujivua gamba ni ngumu sana.

Binafsi nadhani CCM kinahitaji Katibu Mkuu aliyekuwepo kwenye ama TANU au ASP pia ili kukidhi mahitaji ya sifa ya uzalendo na uadilifu.

Umma umeishaaminishwa kuwa ufisadi ni zao la CCM na siyo zao la TANU na ASP. Kama wapo mafisadi wa CCM ambao walikuwa wafuasi wa TANU na ASP basi hao wameambukizwa ufisadi na CCM.

TANU na ASP havikuwa na rekodi ya ufisadi bali uadilifu na uzalendo vilivyojulikana duniani.

Hakuna wafuasi, Makada na Makamisaa waliopata ukwasi ndani ya TANU na ASP bali wamepata ndani ya CCM ambacho falsafa yake ni kujitegemea na kwamba ni chama cha wakulima na wafanyakazi kada ambazo haziwezi kutengeneza matajiri wa haki kutokana na kuwa hazina mazingira ya kutajirika hapa Tanzania.

TANU na ASP iliamini hao ni wanyonyaji na makupe kutokana na kuwa kazi ndani ya vyama hivi na taasisi zao zilikuwa ni za kujitolea 100%.

TANU na ASP vilitegemea rasilimali za wafuasi kujiendesha SIYO wafusi walitegemea rasilimali za vyama hivi kutajirika. Mfumo huu ulikuwa mzuri sana kwa sababu ulikuwa unachuja mchele na chuya.

CCM kimekuja kurithi tunu hiyo tangu 1977 lakini kimeelemewa na uchu mkali, tamaa kali, kiburi kikali, udikteta mkali na kujikuta kikipoteza tunu hiyo.

CCM madaraka yanagombaniwa kwa utakatifu na ulozi pia wakati dhamana za madaraka ndani ya TANU na ASP ziliogopwa kama ukoma.

Katibu Mkuu anayekifaa CCM ni aliyekitumikia TANU pia kwa wadhifa andamizi.

Naomba kutoa hoja.
 
CCM kujivua gamba ni ngumu sana.

Binafsi nadhani CCM kinahitaji Katibu Mkuu aliyekuwepo kwenye ama TANU au ASP pia ili kukidhi mahitaji ya sifa ya uzalendo na uadilifu.

Umma umeishaaminishwa kuwa ufisadi ni zao la CCM na siyo zao la TANU na ASP. Kama wapo mafisadi wa CCM ambao walikuwa wafuasi wa TANU na ASP basi hao wameambukizwa ufisadi na CCM.

TANU na ASP havikuwa na rekodi ya ufisadi bali uadilifu na uzalendo vilivyojulikana duniani.

Hakuna wafuasi, Makada na Makamisaa waliopata ukwasi ndani ya TANU na ASP bali wamepata ndani ya CCM ambacho falsafa yake ni kujitegemea na kwamba ni chama cha wakulima na wafanyakazi kada ambazo haziwezi kutengeneza matajiri wa haki kutokana na kuwa hazina mazingira ya kutajirika hapa Tanzania.

TANU na ASP iliamini hao ni wanyonyaji na makupe kutokana na kuwa kazi ndani ya vyama hivi na taasisi zao zilikuwa ni za kujitolea 100%.

TANU na ASP vilitegemea rasilimali za wafuasi kujiendesha SIYO wafusi walitegemea rasilimali za vyama hivi kutajirika. Mfumo huu ulikuwa mzuri sana kwa sababu ulikuwa unachuja mchele na chuya.

CCM kimekuja kurithi tunu hiyo tangu 1977 lakini kimeelemewa na uchu mkali, tamaa kali, kiburi kikali, udikteta mkali na kujikuta kikipoteza tunu hiyo.

CCM madaraka yanagombaniwa kwa utakatifu na ulozi pia wakati dhamana za madaraka ndani ya TANU na ASP ziliogopwa kama ukoma.

Katibu Mkuu anayekifaa CCM ni aliyekitumikia TANU pia kwa wadhifa andamizi.

Naomba kutoa hoja.
KAMA NI TANU badi ni MZEE WASIRA NA MKUCHIKA

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
 
Wenye sifa hiyo wanaanzia minimum age ya 70+
Sahihi

Walee wajukuu na vitukuu

Succession plan muhimu chama hakiwezi kuwa tu na vikongwe

Wakati wakiwa ofisini wawafunze vijana vizuri washike nafasi kubwa mapema wakiwa na nguvu

Sasa kibabu Kiko miaka 70 plus kipo tu Ina maana kimeshindwa wajibu wa kutengeneza vijana walio vizuri wapokee uongozi na hiyo ni failure kubwa ya hicho kikongwe hata Mtu uwe na biashara binafsi lazima kuiga watu kama Azim Dewji kakabidhi biashara zake zote aendeshe Mwanawe Mo Dewji mapema akiwa Kijana au Mzee Bakhresa mapema kakabidhi Watoto yeye muda mwingi swala Tano

CCM Kuna vikongwe havi groom vijana wenye uwezo vibaki kuonekana vyenyewe star utafikiri vitaishi milele

Vikongwe ondokeni kabidhini chama vijana kwenye succession plan hamtaishi milele kitendeeni Haki chama Kwa kuwapa knowledge vijana washike hatamu za chama na Serikali mbaki washauri

Watoto mkubali wanakua na wamekua kabidhini mbaki washauri kuliko kukomaa tu ndani ya chama ugombea nk

Kuto groom vijana wa ku take over ni udhaifu mkubwa mno Kwa kiongozi yeyote kikongwe awe Serikalini kwenye chama Cha siasa chochote iwe CCM au upinzani au taasisu au family business Vikongwe hata kwenye private business kabidhini Watoto waendeshe

Fanyeni handover kama hamkuwaandaa akili nyie hamna vichwani mtajijua
 
Wenye sifa hiyo wanaanzia minimum age ya 70+
Kwenye siasa hakuna statutory age. Sasa hivi Amerika inagombaniwa na wazee Trump na Biden. Wazee hawana matumizi ya anasa kama vijana, wanaangalia kuacha positive legacy. More so, kwenye CCM elimu siyo sifa ya msingi.
 
KAMA NI TANU badi ni MZEE WASIRA NA MKUCHIKA

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
Safi sana mkuu, hao ni institutional memory ya nchi.

Mkuchika ana uzoefu wa kiserikali, kichama na kidola (jeshi).

Wassira ana audacity ambayo hakuna aliye nayo (labda Jaji Warioba).

Wassira aliweza kumweleza Mwl mapungufu yake bila kupapasa macho. Ndiyo maana Mwl alimuweka kando hadi 1992 akaamua kwenda upinzani ambako nako ujasiri wake wa kuwapa makavu viongozi ulimgharimu pia.

Wassira ni msomi, anakubalika kimataifa (ni mwanadiplomasia pia tena kwenye taifa kubwa la US).

Ana uzoefu wa chama tawala na upinzani na serikali pia (JK alimtumia kwa miaka 10 mfululizo akichota madini kwake).

Wassira amesoma digrii yake ya 3 ya uchumi akiwa na umri mkubwa zaidi ya umri wa kustaafu na kuibuka na matokeo bora zaidi.

Anaijuwa vzr taasisi ya Ikulu kama Mkuchika pia. NO ya Wassira ni NO tu hata kama unamtumbua. YES yake haibadiliki.

Ila orodha ni kubwa tu ya watu hawa akiwemo Lukuvi, Mwandosya et al, Nyerere aliwaandaa kila mkoa.
 
Back
Top Bottom