Makutano Show: Exclusive Interview na Mhe. John Mnyika - Oct 06, 2012

Makutano Show: Exclusive Interview na Mhe. John Mnyika - Oct 06, 2012

Anaulizwa kuna mazuri gani anayoyaona kwenye CCM??

Kwanza anaanza kwa kusema nchi hii kila jambo linalorudisha nyuma chanzo ni ufisadi.

Anasema CCM ya Nyerere ndio ilikuwa na mambo mazuri angalau.
 
Swali kwa Mnyika:

Mkuu, wewe ni msemaji wa kambi ya upinzani Bungeni katika kamati ya Nishati na Madini; hebu FUNGUKA; Tanzania haina tishio la mgao wa umeme?

Nikiisoma hotuba yako bungeni (ref. https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...nzani-wizara-ya-nishati-na-madini-2012-a.html ) napata shaka kuwa tunakoelelea si kuzuri. Labda tutarajie Bil 357 zilizotolewa na Ujerumani kwa Tz ndizo zitatuokoa? Ref. https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...mani-yaisaidia-tanzania-sh-bilioni-357-a.html

anajibu swali lako japo alijaulizwa kama lilivyo.

Anasema anazo nyaraka zinazoonesha kuwa maji kwenye mabwawa yamepungua sana,na ili tusirudi kwenye mgao tunaitaji kumuomba Mungu alete mvua.
 
He is bombing, TANESCO na wizara mama wanasali ili mvua zinyeshe, vinginevyo kutokana na nyaraka zinazotokana na analysis za kitaalam kutoka ndani ya shirika na wizara, zinaonesha nchi inaweza kuingia gizani, kutokana na tatizo la umeme. Ametoa wito kwa wahusika wawaambie Watanzania ukweli wa mambo kuliko kuficha ficha as if kila kitu kiko ok, wakati sivyo.
 
Mnyika jamani ni Jembe.Huyu ni kijana shujaa ndani ya Chama.Huyu ni Role model wa vijana kote nchini.Hili ni Jembe likilopikwa kweli kweli na Dr Slaa na Kamanda Mbowe.Anatiririka sasa kuhusu CDM inavyopambana na ufisadi nchini.Anashangaa jinsi CCM inavyokumbatia ufisadi.Anaelezea jinsi CDM ilivyoweka ilani yake ya uchaguzi uliopita.Anamsifu Mwl Nyerere alivyopambaba na maovu.
 
Fina kamchomekea swali la kama anampango au maono ya kuutaka urais iwapo katiba itabadilishwa na umri kumruhusu.

Amelijibu kikomavu sana..anasema kwa sasa kipaumbele chake ni wana Ubungo na kuhakikisha Chadema inashika dola 2015.
 
Kuhusu kugombea urais siku zijazo Mnyika amesema KAMWE HANA NDOTO HIZO NA SI KIPAUMBELE CHAKE KWA SASA.Amesema Kipaumbele chake kwa sasa ni kuwatumikia wananchi wa Ubungo na kukitumikia chama chake kwa moyo wake wote.
Kipindi kimeisha.Hongera sana CDM kwa kuwa na kijana asiye na mfano wake na Role model wetu John John Mnyika.
 
Show nimeipenda sana ya Leo....Nilitamani Kamanda mnyika aendelee mpaka kesho kuongea....

Hongera dada Fina Mango...
 
Jembe Mnyika anatisha..ni kijana asiyekurupuka,asiyeropoka,asiye na tamaa wala majivuno,amejaa maono na kabeba matumaini ya vijana wa TZ,anajua taifa linataka nini...kwa kweli ukikaa chini kumsikiliza unapata picha ya kiongozi shupavu na mstaharabu..ni full package ya kiongozi tunaemtaka sisi kama vijana wa kitanzania..

Kamaliza interview,na ameifanya siku yangu kuwa supa,

ngojea nijipange nikale bata sasa...wazee wa bata leo nitakuwa Seanage Lounge Oyerstabay kwenye the Legend iz Back na Dj John Dilinga..ukiwa pale si vibaya ukani PM tufahamiane.
 
Fina kamchomekea swali la kama anampango au maono ya kuutaka urais iwapo katiba itabadilishwa na umri kumruhusu.

Amelijibu kikomavu sana..anasema kwa sasa kipaumbele chake ni wana Ubungo na kuhakikisha Chadema inashika dola 2015.
Mnyika ni Jembe linalolima mpaka lami..
 
Jembe Mnyika anatisha..ni kijana asiyekurupuka,asiyeropoka,asiye na tamaa wala majivuno,amejaa maono na kabeba matumaini ya vijana wa TZ,anajua taifa linataka nini...kwa kweli ukikaa chini kumsikiliza unapata picha ya kiongozi shupavu na mstaharabu..ni full package ya kiongozi tunaemtaka sisi kama vijana wa kitanzania..

Kamaliza interview,na ameifanya siku yangu kuwa supa,

ngojea nijipange nikale bata sasa...wazee wa bata leo nitakuwa Seanage Lounge Oyerstabay kwenye the Legend iz Back na Dj John Dilinga..ukiwa pale si vibaya ukani PM tufahamiane.

Mkuu wangu Mnyika ni Noumaaaaaaaaaa....
 
Nilichompenda Fina Mango amembana vilivyo Mnyika na amemuuliza maswali makali ile mbaya Lakini Mnyika ameyajibu kwa ustadi na weledi mkubwa.

Kitu kingine Mnyika amezitumia dakika chache alizopata vilivyo kukijenga chama chake cha CDM.Naweza kusema amekipaisha kwani amezungumzia propaganda zote zinazopigwa na maadui wa CDM na amezichana mbaya.Abarikiwe aliyemteua Mnyika kuwa mkuu wa habari na uenezi.
 
Dah huyu Mh Mnyika leo ameifanya siku yangu iwe njema na mpaka nimesahau habari za kwenda fiesta. Ngoja nijidunge jack daniels huku namsikiliza tena kwa utulivu zaidi.

Amesema Prof Muhongo amefanya uamuzi mgumu wa kupunguza ratio ya gas kwa makampuni binafsi ili mzigo mkubwa wa gesi uende Tanesco.
My take Tujiandae bei ya bia kupanda maana TBL wanatumia Songosongo kwa kiasi kikubwa.

Ila hii ya CUF kupokea misaada kwa chama kinachounga mkono ushoga imeniacha hoi

Siasa ni mchezo mchafu na kama huujui basi twende kwenye Leka Dutigite
 
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi-CDM John Mnyika amesema hana mpango wa kugombea urais hivi karibuni wala katika kipindi cha miaka kumi ijayo na zaidi.Amesema Urais kamwe si kipaumbele chake.
Akihojiwa wiki iliyopita Mnyika ambaye pia ni Mbunge wa Ubungo alisema kwa sasa anayo majukumu makubwa mawili ambayo ameyaweka kama kipaumbele chake.
Mnyika amesema kipaumbele cha kwanza ni kukitumikia chama chake cha CDM kwa moyo mmoja na kuwaunganisha wanachama wote ili kujiandaa kuchukua dola 2015.
Mnyika amesema kipaumbele cha pili ni kuwatumikia wananchi wa ubungo kwa uwezo wake wote.Alisema wananchi wa Ubungo walimuamini yeye na chama chake na kamwe hatawaangusha.
 
Go Go Mnyika!!! Yaani kijana ana busara huyu sijapata kuona. Heri tumbo lililokuzaa na ziwa ulilonyonya!!! Keep it up, parents who raised him to this level!!! Respectable one!!!! Always culm!! Hana papara!!! Zitto upo?
 
Jembeeeeeeee...Hilo ndilo Jembe la CDM bwana.Nakumbuka CCM walikuwa wanasema Malecela ni tingatinga la CCM lakini mimi nasema Mnyika ni Kifaru cha CDM
 
Thank you Mnyika & God bless you. trully!
 
Urais ni issue kubwa siku hizi aisee.Anaetamka kugombea ni adui, anaetamka kutogombea ni hero.
Kaazi kweli kweli
 
Back
Top Bottom