Mr George Francis
Senior Member
- Jun 27, 2022
- 186
- 212
FAHAMU KUHUSU MAKOSA YA RUSHWA NA ADHABU ZAKE KWA MUJIBU WA SHERIA.
SEHEMU YA KWANZA (01)
Mr. George Francis
Mwalimu Nyerere katika hotuba aliyoitoa kwa waandishi wa habari mwaka 1995 alisema,
“Kwa hivyo, tukatengeneza sheria ili tuwafundishe watu hawa kwamba jambo hili hatulipendi. Ikisha kuthibitika mahakamani kwamba kala rushwa hatukumwachia hakimu uamuzi wa adhabu. Tukasema atakwenda ndani muda usiopungua miaka miwili, atapata viboko ishirini na vinne, kumi na mbili siku anayoingia, kumi na mbili siku anayotoka”
Hii inaonesha ni kwa jinsi gani Mwalimu alikuwa mzalendo katika kupambana na rushwa. Taifa letu likewahi kupata viongozi wengi walio na nia ya dhati ya kupambana na rushwa lakini bado hata sasa rushwa imezidi kushamiri katika nchi yetu.
Jamii yetu kwa kiasi kikubwa bado haina elimu juu ya makosa ya rushwa na namna ya kupambana na rushwa. Jukumu hili kwa kiasi kikubwa limeachwa kwa viongozi na maafisa wa mamlaka husika ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa yaani TAKUKURU ambao nao miongoni mwao wapo ambao hawana uadilifu na wamekosa uaminifu.
Vita dhidi ya adui huyu ni kubwa na inapaswa kuwa vita ya jamii yote na sio kuwaachia viongozi au Mamlaka pekeeyake kushughulika na vita hivi.
Hawali ya yote jamii inapaswa kufahamu kuhusu makosa ya rushwa. Yaani lipi ni kosa la rushwa na kipi kifanyike kusudi kuzuia na kutokomeza kabisa vitendo vya rushwa nchini.
Katika makala hii, nakwenda kukuonesha makosa mbalimbali ya rushwa kama yalivyobainishwa katika Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, The Prevention and Combating of Corruption Act
[CAP. 329 R.E. 2022].
Makosa hayo ni haya yafuatayo;
1. Kupokea rushwa, kushawishi au kulazimisha kupewa rushwa, kutoa rushwa au kuahidi kutoa rushwa. Hili ni kosa kwa mujibu wa kifungu cha 15 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
✓ ADHABU:
Ukikutwa na hatia ya kutenda kosa hili adhabu yake ni faini isiyopungua shilingi laki tano (500,000/=) na isiyozidi shilingi milioni moja (1,000,000/=) au kifungo kisichopungua miaka mitatu (3) na kisichozidi miaka mitano (5) au faini na kifungo vyote kwa pamoja.
• Pia Mahakama inaweza kufanya yafuatayo.
(a). Kumwamuru mtuhumiwa kulipa kiasi chote au nusu ya pesa au mali alizopewa rushwa.
(b). Kuamuru kutaifisha pesa au mali iliyopokelewa kama rushwa na kuwa mali ya serikali.
Kuongeza maarifa zaidi kuhusu kosa hili na adhabu yake, hunabudi kusoma kifungu cha 15(1),(2)&(3) kwa umakini.
2. Kutoa au kupokea rushwa kwa ajili ya kupata mkataba
wa kutoa huduma kwa idara ya umma au shirika la umma. Hivyo, kutumia ushawishi usio halali kwa afisa wa idara au shirika la umma ili akusaidie kupata mkataba wa kufanya kazi fulani au kutoa huduma fulani katika idara au shirika la umma kwa makubaliano kuwa kuna faida fulani ataipata ni kosa.
Yeyote atakayethibitika kuhusika na vitendo hivi atahesabika kuwa ametenda kosa la rushwa kwa mujibu wa kifungu cha 16 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
✓ADHABU:
Adhabu yake ni faini isiyopungua milioni moja (1,000,000/=) na isiyozidi Shilingi milioni tatu (3,000,000/=) au Kifungo kisichopungua miaka mitatu (3) na kisichozidi miaka mitano (5) au faini na kifungo vyote kwa pamoja.
•Mbali na adhabu hii, pia mahakama inaweza kuamua yafuatayo.
(i) Kumwamuru mtuhumiwa kumlipa mtu au mwajiri wake kiasi
chote au nusu ya pesa au mali aliyopewa rushwa
au
(ii) Kutaifisha pesa au mali iliyopokelewa kama rushwa na kuwa mali ya serikali.
Kufahamu zaidi juu ya kosa hili hunabudi kusoma kifungu cha 16(1),(2),(3)&(4) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
Rushwa ni adui wa haki. Jukumu la Kuzuia na Kupambana na rushwa ni letu sote mimi, wewe na yule.
Ahsante kwa kusoma makala hii, niombe tuwe pamoja katika sehemu inayofuata ili kufahamu zaidi makosa ya rushwa na adhabu zake.
It's me
Mr George Francis
Email: mr.georgefrancis21@gmail.com
SEHEMU YA KWANZA (01)
Mr. George Francis
Mwalimu Nyerere katika hotuba aliyoitoa kwa waandishi wa habari mwaka 1995 alisema,
“Kwa hivyo, tukatengeneza sheria ili tuwafundishe watu hawa kwamba jambo hili hatulipendi. Ikisha kuthibitika mahakamani kwamba kala rushwa hatukumwachia hakimu uamuzi wa adhabu. Tukasema atakwenda ndani muda usiopungua miaka miwili, atapata viboko ishirini na vinne, kumi na mbili siku anayoingia, kumi na mbili siku anayotoka”
Hii inaonesha ni kwa jinsi gani Mwalimu alikuwa mzalendo katika kupambana na rushwa. Taifa letu likewahi kupata viongozi wengi walio na nia ya dhati ya kupambana na rushwa lakini bado hata sasa rushwa imezidi kushamiri katika nchi yetu.
Jamii yetu kwa kiasi kikubwa bado haina elimu juu ya makosa ya rushwa na namna ya kupambana na rushwa. Jukumu hili kwa kiasi kikubwa limeachwa kwa viongozi na maafisa wa mamlaka husika ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa yaani TAKUKURU ambao nao miongoni mwao wapo ambao hawana uadilifu na wamekosa uaminifu.
Vita dhidi ya adui huyu ni kubwa na inapaswa kuwa vita ya jamii yote na sio kuwaachia viongozi au Mamlaka pekeeyake kushughulika na vita hivi.
Hawali ya yote jamii inapaswa kufahamu kuhusu makosa ya rushwa. Yaani lipi ni kosa la rushwa na kipi kifanyike kusudi kuzuia na kutokomeza kabisa vitendo vya rushwa nchini.
Katika makala hii, nakwenda kukuonesha makosa mbalimbali ya rushwa kama yalivyobainishwa katika Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, The Prevention and Combating of Corruption Act
[CAP. 329 R.E. 2022].
Makosa hayo ni haya yafuatayo;
1. Kupokea rushwa, kushawishi au kulazimisha kupewa rushwa, kutoa rushwa au kuahidi kutoa rushwa. Hili ni kosa kwa mujibu wa kifungu cha 15 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
✓ ADHABU:
Ukikutwa na hatia ya kutenda kosa hili adhabu yake ni faini isiyopungua shilingi laki tano (500,000/=) na isiyozidi shilingi milioni moja (1,000,000/=) au kifungo kisichopungua miaka mitatu (3) na kisichozidi miaka mitano (5) au faini na kifungo vyote kwa pamoja.
• Pia Mahakama inaweza kufanya yafuatayo.
(a). Kumwamuru mtuhumiwa kulipa kiasi chote au nusu ya pesa au mali alizopewa rushwa.
(b). Kuamuru kutaifisha pesa au mali iliyopokelewa kama rushwa na kuwa mali ya serikali.
Kuongeza maarifa zaidi kuhusu kosa hili na adhabu yake, hunabudi kusoma kifungu cha 15(1),(2)&(3) kwa umakini.
2. Kutoa au kupokea rushwa kwa ajili ya kupata mkataba
wa kutoa huduma kwa idara ya umma au shirika la umma. Hivyo, kutumia ushawishi usio halali kwa afisa wa idara au shirika la umma ili akusaidie kupata mkataba wa kufanya kazi fulani au kutoa huduma fulani katika idara au shirika la umma kwa makubaliano kuwa kuna faida fulani ataipata ni kosa.
Yeyote atakayethibitika kuhusika na vitendo hivi atahesabika kuwa ametenda kosa la rushwa kwa mujibu wa kifungu cha 16 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
✓ADHABU:
Adhabu yake ni faini isiyopungua milioni moja (1,000,000/=) na isiyozidi Shilingi milioni tatu (3,000,000/=) au Kifungo kisichopungua miaka mitatu (3) na kisichozidi miaka mitano (5) au faini na kifungo vyote kwa pamoja.
•Mbali na adhabu hii, pia mahakama inaweza kuamua yafuatayo.
(i) Kumwamuru mtuhumiwa kumlipa mtu au mwajiri wake kiasi
chote au nusu ya pesa au mali aliyopewa rushwa
au
(ii) Kutaifisha pesa au mali iliyopokelewa kama rushwa na kuwa mali ya serikali.
Kufahamu zaidi juu ya kosa hili hunabudi kusoma kifungu cha 16(1),(2),(3)&(4) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
Rushwa ni adui wa haki. Jukumu la Kuzuia na Kupambana na rushwa ni letu sote mimi, wewe na yule.
Ahsante kwa kusoma makala hii, niombe tuwe pamoja katika sehemu inayofuata ili kufahamu zaidi makosa ya rushwa na adhabu zake.
It's me
Mr George Francis
Email: mr.georgefrancis21@gmail.com