Makosa 10 aliyotenda Mungu

Makosa 10 aliyotenda Mungu

Kwa nini tuanzishe mjadala wakati mjadala huu wa mungu kakosea hiki na kike utakuwa hauwezekaniki kuwapo kama tunaweza kuonesha mungu huyu hayupo kabisa?
Huoni kwamba swali la uwepo au kutokuwepo kwa mungu ni msingi wa swali la thread hii na kinaweza kuonesha kwa kina kwamba, kwa mfano, tukiweza kuonesha mungu hayupo, suala zima la mungu kakosea hili na like linakuwa halipo kwa sababu mungu mwenyewe hayupo kabisa?
Kiranga mimi kama free thinker haya maswali naweza kuyajibu yote bila kutumia kitabu cha dini wala kutoa sababu mf. matakwa ya Mungu au hila za shetani.Hii tread imefika pg ya 34 ila sijaona jibu la maana humu zaidi ya vitisho na lawama....kama watu wanamjua Mungu na mapenzi yake basi wangeweza kujibu....ila kujuwa kitu lazima kiexist kwanza.
 
Kiranga mimi kama free thinker haya maswali naweza kuyajibu yote bila kutumia kitabu cha dini wala kutoa sababu mf. matakwa ya Mungu au hila za shetani.Hii tread imefika pg ya 34 ila sijaona jibu la maana humu zaidi ya vitisho na lawama....kama watu wanamjua Mungu na mapenzi yake basi wangeweza kujibu....ila kujuwa kitu lazima kiexist kwanza.
Mungu huyu yupo au hayupo kwa mujibu wako?
 
Unaweza kuthibitisha chochote ambacho hakipo kwamba hakipo?

Unafahamu mantiki ya uthibitisho?

Utathibitishaje kwamba kisichopo hakipo?

Nadhani utakuwa na maana yako ya kipekee ya neno "uthibitisho" ambayo kimsingi sio maana sahihi kama ilivyo katika kamusi ya kiswahili.

Nimekwambia uthibitishe ulichokisema badala yake umekuja na counter-arguments nyepesi.

Kwanini usiwe na sababu/uthibitisho wa kitu ambacho hakipo kama kweli una huakika hicho kitu hakipo!!?

Kwani hata wewe ukijihisi unaumwa maralia hili kuthibitisha si lazima utapimwa na vipimo husika na kama kweli hauna maralia, vipimo vitaonyesha hauna... kwa hiyo hapo tayari unakuwa na sababu ya kwanini hauna malaria kwa maana hiyo unakuwa umethibitisha kutokuwepo kwa kitu ambacho hakipo.

Kwa mfano huu rahisi inashindikana nini kwako kuthibitisha kutokuwepo kwa hicho kitu ambacho unadai hakipo?
 
Mkuu mimi ni free thinker....nina ruhusu majadiliano huru ila ya kweli....kuhusu kuwepo au kutokuwepo kwake inabidi tuanzishe mjadala au kama upo tuwendeleze.
Sawa mr.free thinker wakati unaandika hayo uliyoandika, umejiridhisha vipi na kuona kwamba hayo ni makosa ya Mungu? Je kuna kitabu chochote cha maandiko unachotumia kama reference na kuona wakielezea hayo ni makosa ya Mungu!!?
 
Sawa mr.free thinker wakati unaandika hayo uliyoandika, umejiridhisha vipi na kuona kwamba hayo ni makosa ya Mungu? Je kuna kitabu chochote cha maandiko unachotumia kama reference na kuona wakielezea hayo ni makosa ya Mungu!!?
Hivi mtu akinya barabarani unahitaji reference kujua kama lile ni kosa???
 
Nadhani utakuwa na maana yako ya kipekee ya neno "uthibitisho" ambayo kimsingi sio maana sahihi kama ilivyo katika kamusi ya kiswahili.

Nimekwambia uthibitishe ulichokisema badala yake umekuja na counter-arguments nyepesi.

Kwanini usiwe na sababu/uthibitisho wa kitu ambacho hakipo kama kweli una huakika hicho kitu hakipo!!?

Kwani hata wewe ukijihisi unaumwa maralia hili kuthibitisha si lazima utapimwa na vipimo husika na kama kweli hauna maralia, vipimo vitaonyesha hauna... kwa hiyo hapo tayari unakuwa na sababu ya kwanini hauna malaria kwa maana hiyo unakuwa umethibitisha kutokuwepo kwa kitu ambacho hakipo.

Kwa mfano huu rahisi inashindikana nini kwako kuthibitisha kutokuwepo kwa hicho kitu ambacho unadai hakipo?
Ni hivi.

Uthibitisho nje ya nadharia ni kwa ajili ya vitu vilivyopo.

Si kwa ajili ya visivyopo.

Unathibitisha kitu kipo kwa sababu kipo, utakiona, utakipima uzito, utakinusa, utakipigia hesabu na kukuta kipo, utakiandikia truth table ya logic na kukiona kipo. Utafanya experimental observation kuondoa shaka.

Sasa kitu kama hakipo maana yake hakipo kuthibitishwa kwamba hakipo. Utathibitisha nini?

Mtu akikwambia katikati ya chumba chako kuna chemli ya dhahabu inayoelea hewani. Chemli hii haionekani kwa macho wala kuweza kupimika kwa kitu chochote. Tunajua kwamba hii chemli haipo. Lakini utathibitishaje kwamba haipo?

Unaweza kuthibitisha kwamba chemli hii ambayo haipo kwamba haipo?

Wakati ushaambiwa haionekani wala kupimika?

Uthibitisho wa kinadharia kwamba mungu hayupo ni ukweli kwamba wazo la kuwapo huyu mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na uoendo wote ambaye kaumba dunia yenye maovu yote haya linajipinga lenyewe.

Ni kama mtu aseme kuna pembetatu duara katika Euclidean geometry.

That is a contradiction.

Pembetatu si duara na duara si pembetatu hivyo oembetatu ambayo pia ni duara haiwezekaniki kuwapo katika Euclidean geometry. Ni contradiction.

Mungu wenu naye hawezi kuwapo.


Kwa sababu idea ya kuwapo kwake ni contradiction kama pembetatu duara.
 
I always prove things with practicality...anything less than that to me it is nonsense
Hujajibu swali.

Katika hiyo practicality yako. Mungu huyo yupo au hayupo?

Practicality may mean one thing to you and the complete different thing to another person.
 
Hijajibu swali.

Katika hiyo practicality yako. Mungu huyo yupo au hayupo?

Practicality may mean one thing to you and the complete different thing to another person.
''Mwanzoni Mungu alimuumba mwanadamu'' traditionally hiyo sentesi inasomwa kutokea kushoto kwenda kulia, ila mimi huwa naisoma kutokea kulia kwenda kushoto.Baada ya watu wa kale kukutana na mambo yasiyoelezeka kwenye jamii zao, waliamini kuwa kuna dude linalosababisha hayo mambo.Hivyo Mungu ni product ya human mind, chukulia mf. wa filamu ya bushman...aliokota chupa ya cocacola na kusema kuwa ni Mungu amemletea, lakini ile chupa ilitoka wapi??? Kwahiyo hamna kitu kiitwacho Mungu, bali ni mawzo ya watu tu.
 
''Mwanzoni Mungu alimuumba mwanadamu'' traditionally hiyo sentesi inasomwa kutokea kushoto kwenda kulia, ila mimi huwa naisoma kutokea kulia kwenda kushoto.Baada ya watu wa kale kukutana na mambo yasiyoelezeka kwenye jamii zao, waliamini kuwa kuna dude linalosababisha hayo mambo.Hivyo Mungu ni product ya human mind, chukulia mf. wa filamu ya bushman...aliokota chupa ya cocacola na kusema kuwa ni Mungu amemletea, lakini ile chupa ilitoka wapi??? Kwahiyo hamna kitu kiitwacho Mungu, bali ni mawzo ya watu tu.
Nimekuwa nikiandika hili hapa kitambo sasa.
 
Hivi mtu akinya barabarani unahitaji reference kujua kama lile ni kosa???
Na mimi nilitaka kujua tu kama kuna sehemu yoyote ya uhakika uliyopata maarifa na hatimae kuja kuandika haya.. ingenisaidia kutambua kama mimi ndio kuna vitu nnavi-miss na nnahitaji spiritual enlightenment au nikafanye rivisit ya kila nilichowahi kujifunza kinachohusiana na mambo ya kiroho.

Mathalani umeshaonyesha kwamba haya ni mawazo yako mwenyewe basi haina sababu ya kukutilia mashaka tena kwa sababu mawazo yako kwanza yamekaa kidunia zaidi, yaani kama vile unajaribu kutengeneza theories zako kwa mambo ya kiroho.

Nasema unatengeneza theories zako na hii ni dhiaka inayoenda kukuvunia dhambi ya mauti kwa sababu hata ulivyo ulivyoelezea humo ni meaningless.

Mfani unasema viungo vya binadamu kama matiti kwa mwanaume hayo ni makosa kisa sababu kazi yake hauioni!!? kama ni hivyo basi hata alivyotuumba na macho mawili napenyewe alifanya kosa kwa sababu kuna watu wanazaliwa na jicho moja na wanaona vizuri tu kama wewe mwenye macho mawili...
 
Ni hivi.

Uthibitisho nje ya nadharia ni kwa ajili ya vitu vilivyopo.

Si kwa ajili ya visivyopo.

Unathibitisha kitu kipo kwa sababu kipo, utakiona, utakipima uzito, utakinusa, utakipigia hesabu na kukuta kipo, utakiandikia truth table ya logic na kukiona kipo. Utafanya experimental observation kuondoa shaka.

Sasa kitu kama hakipo maana yake hakipo kuthibitishwa kwamba hakipo. Utathibitisha nini?

Mtu akikwambia katikatibya chumba chako kuna chemli ya dhahabu unayoelea hewani. Chemli hii haionekani kwa macho wala kuweza kupimika kwa kitu chochote. Tunajua kwamba hii chemli haipo. Lakini utathibitishaje kwamba haipo?

Unaweza kuthibitisha kwamba chemli hii ambayo haipo kwamba haipo?

Wakati ushaambiwa haionekani wala kupimika?

Uthibitisho wa kinadharia kwamba mungu hayupo ni ukweli kwamba wazo la kuwapo huyu mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na uoendo wote ambaye kaumba dunia yenye maovu yote haya linajipinga lenyewe.

Ni kama mtu aseme kuna pembetatu duara katika Euclidean geometry.

That is a contradiction.

Pembetatu si duara na duara si pembetatu hivyo oembetatu ambayo pia ni duara haiwezekaniki kuwapo katika Euclidean geometry. Ni contradiction.

Mungu wenu naye hawezi kuwapo.


Kwa sababu idea ya kuwapo kwake ni contradiction kama pembetatu duara.
Sawa...naomba utizame hapa

Swali kwako, je unaamini uwepo wa illuminant/freemasonry?

Na unaelewa nini ukiskia "roho"?
 
Sawa...naomba utizame hapa

Swali kwako, je unaamini uwepo wa illuminant/freemasonry?

Na unaelewa nini ukiskia "roho"?
Sitaki habari za kuamini, nataka kujua.

Roho ni nini?

Freemasonry ni jamii ya watu. Kama Ukristo au Uislamu. Wapo na wana Masonic Lodges zao. Wengine tunafanya nao kazi.

Ex-girlfriend wangu babu yake alikuwa Freemason mkubwa sana. Wengi wanakuwa katika siasa na Upolisi nchibkama Marekani. Marais wengi wa Marekani ni Freemasons.

Kwa nini unaona ni kitu cha ajabu sana mpaka kuulizia?
 
Sitaki habari za kuamini, nataka kujua.

Roho ni nini?

Freemasonry ni jamii ya watu. Kama Ukristo au Uislamu. Wapo na wana Masonic Lodges zao. Wengine tunafanya nao kazi.

Ex-girlfriend wangu babu yake alikuwa Freemason mkubwa sana. Wengi wanakuwa katika siasa na Upolisi nchibkama Marekani. Marais wengi wa Marekani ni Freemasons.

Kwa nini unaona ni kitu cha ajabu sana mpaka kuulizia?

Sawa sawa na hayo ndio yalikuwa madhumuni yangu mimi kuuliza hayo maswali na endapo kama ungesema haumani uwepo wa hivyo vyote viwili basi ningeaachana na wewe na kuamini kweli wewe ni pure atheist.

Lakini badala yake wewe umeonesha undumilakuwil na kunipa mashaka na huo msimamo wako, yaani unapinga uwepo wa Mungu wakati huo huo kuna vitu ambavyo chimbuko lake ni Mungu unakubaliana navyo.

Kama unakubali uwepo wa Freemasonry ambayo kihalisia ni dini/jamii ya kishetani, hauoni kwamba hapo tayari umeshakubaliana na uwepo wa Mungu?

Kwa sababu huyo shetani/ibilisi ambaye ndio mwenye hiyo dini ya Freemasonry chimbuko lake ni Mungu.
 
Sawa sawa na hayo ndio yalikuwa madhumuni yangu mimi kuuliza hayo maswali na endapo kama ungesema haumani uwepo wa hivyo vyote viwili basi ningeaachana na wewe na kuamini kweli wewe ni pure atheist.

Lakini badala yake wewe umeonesha undumilakuwil na kunipa mashaka na huo msimamo wako, yaani unapinga uwepo wa Mungu wakati huo huo kuna vitu ambavyo chimbuko lake ni Mungu unakubaliana navyo.

Kama unakubali uwepo wa Freemasonry ambayo kihalisia ni dini/jamii ya kishetani, hauoni kwamba hapo tayari umeshakubaliana na uwepo wa Mungu?

Kwa sababu huyo shetani/ibilisi ambaye ndio mwenye hiyo dini ya Freemasonry chimbuko lake ni Mungu.
Kuamini kwamba kuna mtu anaamini kwamba kuna pembetatu duara ni kuamini kwamba kuna pembetatu duara?

Unafahamu kwamba kuna watu mpaka leo wanaamini kwamba dunia ni bapa na si tufe?

Ukikubali kwamba watu hawa wapo maana yake na wewe umeamini dunia si tufe ni bapa?

Unafahamu kwamba kuna watu hawaamini kwamba kuna HIV na UKIMWI?

Ukikubali kwamba hawa watu wapo maana yake unaamini hakuna HIV na UKIMWI?

Unafahamu kwamba kuna vibabu huko vijijini bado vinaamini Julius Kambarage Nyerere ni rais wa Tanzania?

Ukikubali kwamba watu hao wapo maana yake umekubali kwamba Julius Kambarage Nyerere ni rais wa Tanzania?

Unafahamu kwamba kuna Wamarekani wanaamini kwamba Tanzania ni kisiwa kilichopo pwani ya Australia?

Ukikubali kuwapo kwa watu hao hilo lina maana umekubali kwamba Tanzania ni kisiwa kilichopo pwani ya Australia?

Unafahamu kwamba kuna watu wanaamini mlima Kilimanjaro uko Kenya?

Ukikubali kwamba kuna watu wanaamini mlima Kilimanjaro upo Kenya hilo lina maana unaamini mlima Kilimanjaro upo Kenya?

Ukiwa unaamini mungu yupo na unaamini kwamba kuna watu wanaamini mungu hayupo, kuamini kwamba kuna watu hawaamini mungu yupo kunaondoa imani yakobya kuamini mungu yupo?

Kukubali kwamba watu wana imani fulani hakumaanishi kwamba umekubali kwamba imani hiyo ni sahihi.

Unaweza kukubali kwamba kuna watu wanaamini kula nyama ya mtu kunawaongezea nguvu za uchawi wakati wewe mwenyewe hukubalibkwamba imani hiyo ina msingi sahihi.

Hujaweza kuthibitisha kwamba mungu yupo.

Kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote aumbe ulimwengu ambao ubaya unawezekanika? Hususan kwa sababu aliweza kuumba ulimwengu ambao ubaya hauwezekaniki na asipungukiwe chochote?
 
Kuamini kwamba kuna mtu anaamini kwamba kuna pembetatu duara ni kuamini kwamba kuna pembetatu duara?

Unafahamu kwamba kuna watu mpaka leo wanaamini kwamba dunia ni bapa na si tufe?

Ukikubali kwamba watu hawa wapo maana yake na wewe umeamini dunia si tufe ni bapa?

Unafahamu kwamba kuna watu hawaamini kwamba kuna HIV na UKIMWI?

Ukikubali kwamba hawa watu wapo maana yake unaamini hakuna HIV na UKIMWI?

Unafahamu kwamba kuna vibabu huko vijijini bado vinaamini Julius Kambarage Nyerere ni rais wa Tanzania?

Ukikubali kwamba watu hao wapo maana yake umekubali kwamba Julius Kambarage Nyerere ni rais wa Tanzania?

Unafahamu kwamba kuna Wamarekani wanaamini kwamba Tanzania ni kisiwa kilichopo pwani ya Australia?

Ukikubali kuwapo kwa watu hao hilo lina maana umekubali kwamba Tanzania ni kisiwa kilichopo pwani ya Australia?

Unafahamu kwamba kuna watu wanaamini mlima Kilimanjaro uko Kenya?

Ukikubali kwamba kuna watu wanaamini mlima Kilimanjaro upo Kenya hilo lina maana unaamini mlima Kilimanjaro upo Kenya?

Ukiwa unaamini mungu yupo na unaamini kwamba kuna watu wanaamini mungu hayupo, kuamini kwamba kuna watu hawaamini mungu yupo kunaondoa imani yakobya kuamini mungu yupo?

Kukubali kwamba watu wana imani fulani hakumaanishi kwamba umekubali kwamba imani hiyo ni sahihi.

Unaweza kukubali kwamba kuna watu wanaamini kula nyama ya mtu kunawaongezea nguvu za uchawi wakati wewe mwenyewe hukubalibkwamba imani hiyo ina msingi sahihi.

Hujaweza kuthibitisha kwamba mungu yupo.

Kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote aumbe ulimwengu ambao ubaya unawezekanika? Hususan kwa sababu aliweza kuumba ulimwengu ambao ubaya hauwezekaniki na asipungukiwe chochote?
Yaani swali linajibiwa na swali linafuatiwa na swali alafu tena swalii...... yaani mpaka nimechokaa.

Mkuu nimeuliza swali jepesi tu lakini jibu ulilotoa ni irrelevant na nilichokuuliza na ukarukia fasta kwenye conclusion wakati hata wewe mwenyewe bado hujathibitisha unachosimamia.

It is like you've miscontrued what exactly i have asked, i find hard to extend this argumentation with you anymore.. you derail my questions to your own way you want it to be and you ain't reaady to answer as it originally is.

Mimi hata sijauliza kama unaamini uwepo wa wanachama wa freemasonry kama ulekeo wa majibu yako unavyoonyesha, mimi nimeuliza je unaamini hiyo dini ya freemasonry ipo!!?

Kama ipo niambie who are those religion worshippers worshipping for if not the devil..!!?
 
Back
Top Bottom