Makosa 10 aliyotenda Mungu

Makosa 10 aliyotenda Mungu

Unadhani maafa mbalimbali mfano tetemeko la ardhi husababishwa na nini?
Hapo sasa umeuliza swali linalofaa zaidi.

Maafa yanasababishwa na ukweli kwamba ulimwengu haujaumbwa na Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote.

Ungeumbwa na Mungu huyo, angezuia maafa yasitokee.

Lakini maafa haya yanayokana na mifumo kumomonyoka (kwa sababu haijaumbwa na Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ambaye angeweza kuzuia mifumo isimomonyoke).

Ni second law of thermodynamics at work.

Given enough time, without sustaining work, all closed systems break down. Entropy increase. Disorder increase. Disasters strike.
 
Ahsante kwa kujiona wewe upo katika wenye kujua hapo inaonyesha mungu hayupo, mungu mwenye busara na hekima kwanini anaumba wapumbavu na werevu ? Mbona hana fair

Maneno yako yamejaa shari ila kwasisi waungwana hatuwezi kukudharau wala kukutoa kasoro hata ukosee vipi ila sisi huwa tunasema

"Faidhaa khatwaba humul jahiiluuna qaluu salama"


Kaka hapo sijakudharau bali nimekupa haki yako.

Kaka hakuna binadamu aliyeumbwa anajua,wala binadamu aliyeumbwa mpumbavu,wala mjinga,haya ni matokeo,ingekuwa binadamu anaumbwa anajua basi wa mwanzo wao wamgeumbwa mitume wanajua,lakini mitume walifunzwa. Sasa usijilize na kutafuta kichaka.

Kaka unaonekana hauko makini na mipaka ya kielimu,laiti ungejua uzito wa elimu usingeeendelea kupuuza nasaha nilizokupa.

Kaka,naona unaikosea Qur'an na watu hicho ni kitabu ninacho kiamini na hakina shaka ndani yake.

Umemalizia aya kwa kurudia makosa vile vile,kaka kiheshimu kitabu haki.
 
Dini= Religion =دين

Hapo umetafsiri sijakuambia unipe tafsiri

Naomba maelzo ya dini sitaki tafsiri[/QUOTE]
Una sasa unavyopuyanga sasa tafsiri na kutaka maelezo kuna tofauti gani ?

Mkiambiwa muwe mnajifunza maana za istilahi za kielimu lengo muepukane na makosa madogo madogo kama haya.

Huyo hajatafsiri maana ya dini kwa ile maana hasa ya tafsiri.

Nakuja...........!
 
Hapo sasa umeuliza swali linalofaa zaidi.

Maafa yanasababishwa na ukweli kwamba ulimwengu haujaumbwa na Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote.

Ungeumbwa na Mungu huyo, angezuia maafa yasitokee.

Lakini maafa haya yanayokana na mifumo kumomonyoka (kwa sababu haijaumbwa na Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ambaye angeweza kuzuia mifumo isimomonyoke).

Ni second law of thermodynamics at work.

Given enough time, without sustaining work, all closed systems break down. Entropy increase. Disorder increase. Disasters strike.
Umekuja kwenye pointi yangu ya msingi niliyokuwa ninaitaka.

Kwa hiyo umekubali kwamba maafa hayatokani na Mungu bali ni hizi shughuli zetu za kila siku tunazozifanya, na hata ile ajali ya Mv Nyerere haiuhusiani kabisa na Mungu bali ni uzembe wetu sisi wenyewe, hivyo basi hata hoja yako ya kusema habari za Mungu zinajikanganya zenyewe kwa kuonesha upande mmoja ana huruma sana na upande mwengine ni mkatili kwa sababu ameumba kifo ambacho kimsingi kinatenganisha watu wanaopendana ni batili.


Na mpaka hapa tumeivunja hoja yako .
 
Ustadhi Zurri unanikimbia katka hoja ya muda me nimekuambia hakuna anayejua maana ya muda katka dunia ya leo

Nasikitika wewe unapotaka kujua muda nini?
Suala la muda nilishalimaliza kitambo,kwa nyie kushindwa swali langu nililo wauliza kuhusu muda ulianza lini.

Ushahidi wa muda upo katika Qur'an na nilishatoa ishara juu ya muda na kazi zake.

Sasa labda kama uwe hujaelewa au una jipya.

Kinda Kiranga katika mawanda ya kielimu alichemka swali hili,a sikumbuki kama nilishawahi kumuuliza swali akajibu swali langu hata moja.

Narudi............!
 
Hapo sasa umeuliza swali linalofaa zaidi.

Maafa yanasababishwa na ukweli kwamba ulimwengu haujaumbwa na Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote.

Ungeumbwa na Mungu huyo, angezuia maafa yasitokee.

Lakini maafa haya yanayokana na mifumo kumomonyoka (kwa sababu haijaumbwa na Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ambaye angeweza kuzuia mifumo isimomonyoke).

Ni second law of thermodynamics at work.

Given enough time, without sustaining work, all closed systems break down. Entropy increase. Disorder increase. Disasters strike.
Baada ya kukubali maafa hayatokani na Mungu bali shughuli zetu na uzembe wetu wa kila siku ndio unapelekea maafa,mpaka sasa hoja iliyobaki kwamba Mungu ana upendo sana kwa sababu hoja ya upande wa pili kuhusu maafa umekubali mwenyewe kwamba hayaletwi na Mungu.


Umekubali mpaka hapa kwamba habari za Mungu hazijikanganyi?
 
Umekuja kwenye pointi yangu ya msingi niliyokuwa ninaitaka.

Kwa hiyo umekubali kwamba maafa hayatokani na Mungu bali ni hizi shughuli zetu za kila siku tunazozifanya, na hata ile ajali ya Mv Nyerere haiuhusiani kabisa na Mungu bali ni uzembe wetu sisi wenyewe, hivyo basi hata hoja yako ya kusema habari za Mungu zinajikanganya zenyewe kwa kuonesha upande mmoja ana huruma sana na upande mwengine ni mkatili kwa sababu ameumba kifo ambacho kimsingi kinatenganisha watu wanaopendana ni batili.


Na mpaka hapa tumeivunja hoja yako .
Maafa hayawezi kutokana na Mungu katika ulimwengu ambao Mungu hayupo.

Na katika ulimwengu ambao Mungu yupo, maafa hayawezekani kuwepo.

Kwa hiyo, tunapoona ulimwengu huu una maafa, huo ni ushahidi kwamba Mungu hayupo.

Angekuwepo, angezuia maafa yasiwezekane tangu mwanzo kabisa anauumba ulimwengu.
 
Mtu asiyeamini ana haki ya kupewa vithibitisho ili aweze kuamini kuwa jambo fulani lipo.

Sasa inakuwaje mnaotetea mnaongea tu maneno mengi ambayo hayana facts ndani yake?

Hamuoni kama mnapoteza muda kutetea jambo ambalo hamuwezi kulithibitisha?

Hamuoni kuwa mmedandia tu gari mkaambiwa kuwa hili linaelekea mbinguni kwa Mungu mkapewa sifa kedekede za kupendeza na kupewa vitisho vingi pia vilivyo obscure your capacity to think out of the box kwa kuwa induced na fear kuwa utakufuru?

Nani aliewahi kumwona Mungu au kufika mbinguni/motoni/peponi/ahera n.k akaleta mrejesho wa hayo yote?

Jibu ni kuwa hakuna. Na kama upo ushahidi tunaomba hapa ili nasisi tuamini.
Kaka nakuuliza ili nikisaidie,nilitaka nikupuuze tangu ulipovamia hii mada kwa pupa. Sasa nataka twende kwa mtindo hui.

Kwako wewe ili jambo uliamini unataka liwe na sifa gani ?

Je kama Mola haonekani je hiki ni kigezo cha wewe kuto muamini ?

Vipi kuhusu njaa,upepo umewahi kuviona viwili hivi,je vipi kuhusu kesho je umewahi kuiona kesho au huamini kama kuna kesho ?

Narudi........!
 
Baada ya kukubali maafa hayatokani na Mungu bali shughuli zetu na uzembe wetu wa kila siku ndio unapelekea maafa,mpaka sasa hoja iliyobaki kwamba Mungu ana upendo sana kwa sababu hoja ya upande wa pili kuhusu maafa umekubali mwenyewe kwamba hayaletwi na Mungu.


Umekubali mpaka hapa kwamba habari za Mungu hazijikanganyi?

Hujaelewa nilichoandika.

Maafa hayawezi kutokana na Mungu katika ulimwengu ambao Mungu hayupo.

Na katika ulimwengu ambao Mungu yupo, maafa hayawezekani kuwepo.

Kwa hiyo, tunapoona ulimwengu huu una maafa, huo ni ushahidi kwamba Mungu hayupo.

Angekuwepo, angezuia maafa yasiwezekane tangu mwanzo kabisa anauumba ulimwengu.
 
Kama ana matatizo, hajui, ni mpumbavu kweli.

Hilo nalo ni ushahidi kwamba Mungu mwenye ujuzi wote, uwezo wote na upendo wote hayupo.

Angekuwepo, asingeumba ulimwengu ambao unaweza kuwa na viumbe wake wenye upumbavu.
Hili nilishakujibu kitambo.
 
Maafa hayawezi kutokana na Mungu katika ulimwengu ambao Mungu hayupo.

Na katika ulimwengu ambao Mungu yupo, maafa hayawezekani kuwepo.

Kwa hiyo, tunapoona ulimwengu huu una maafa, huo ni ushahidi kwamba Mungu hayupo.

Angekuwepo, angezuia maafa yasiwezekane tangu mwanzo kabisa anauumba ulimwengu.
Ili Mungu awepo lazima kuwe na sifa kuu zipi?

Embu ziorodheshe hapa, angalau tano.
 
Hujaelewa nilichoandika.

Maafa hayawezi kutokana na Mungu katika ulimwengu ambao Mungu hayupo.

Na katika ulimwengu ambao Mungu yupo, maafa hayawezekani kuwepo.

Kwa hiyo, tunapoona ulimwengu huu una maafa, huo ni ushahidi kwamba Mungu hayupo.

Angekuwepo, angezuia maafa yasiwezekane tangu mwanzo kabisa anauumba ulimwengu.
Kwa hiyo umekubali kwamba ulimwengu umeumbwa na Mungu?
 
Unajua kwamba ukishaanza kuchambua habari za madhaifu ya logic, ushatumia logic hapo hapo?

Unaweza kuthibitisha Mungu yupo?
Sijatumia logic sababu elimu ya mantiki imekuja baada ya watu kumakinika katika mambo mengi sana,kumakinika katika kuujia uweli,kumakinika katika kujua kujenga hoja.

Kama una amini wakina Thales,Homeri,Aristosto,Socrates na wengine walikuja baada ya mitume kadhaa kupita ujue elimu ya mantiki ni ujinga wa kupuuzwa sababu watu walikuwa wameshaelimika kitambo sana.


Ila hawa waitwao wanafalsafa waliamua kiacha dini kwa hiyari zao wenyewe ndio maana wakapotea wao na wakawapoteza wenzi wao.

Nakuja..........!
 
Ili Mungu awepo lazima kuwe na sifa kuu zipi?

Embu ziorodheshe hapa, angalau tano.
Awe na logical consiatency isiyo na contradiction.

Mungu anatakiwa asiwe na contradiction. Huyu Mungu wa Biblia, Quran Mungu omnipotent, omniscient, omni benevolent kwa mfano, mtu akiweza kuniondolea contradictions zote zilizopo katika habari zake, sio tu nitakubali, bali pia nitafurahi sana. Contradictions hizo ni hizi.
Kwa uchache.

1. Kwa nini Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote, upendo wote na utakatifu wote, kaumba ulimwengu ambao maovu yanaweza kutokea, wakati alikuwa ana uwezo wa kuumba ulimwengu ambao maovu hayawezi kutokea? Naomba jibu lisiwe kusema maovu yapo kwa sababu ya shetani. Swali linauliza kabla shetani hajaumbwa Mungu alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao shetani hawezi kuwepo. Jibu la swali lisiseme maovu ni matokeo ya dhambi za watu. Mungu angeweza kuumba ulimwengu ambao dhambi haiwezekani. Jibu lisiseme free will, hatuna hiyo inayoitwa free will katika mengi sana na hata kui define tu watu hawawezi.

2. Inakuwaje Mungu awe ndiyo mtoa rehema ya kumjua, anachagua mwenyewe nani amjue na nani asimjue, halafu mtu akishindwa kumjua Mungu, kwa sababu Mungu hajamchagua huyo mtu kumpa neema yake Mungu ya kumjua, huyo mtu aonekane ana makosa, ahukumiwe kuchomwa moto? Baba anawezaje kumhukumu mtoto ambaye hajui kusoma, kama mtoto hajui kusoma kwa sababu baba ndiye aliyemnyima nafasi ya kwenda shule?

3. Inakuwaje mahakama za watu tu zinakataza mtoto kuhukumiwa kwa makosa ya mzazi, lakini vitabu vya Mungu vinasema Mungu anahukumu watoto na wajukuu vizazi hata vizazi? Kwa kosa la mzazi wa zamani sana? Huyu Mungu mbona haki yake haijafikia hata haki yetu watu tu?

4. Mnasema Mungu anajua yote. Anayajua maisha ya mtu yote mwanzo mpaka mwisho kabla hata mtu hajaishi. Na anachojua huyo Mungu kitatokea, ni lazima kitokee. Anavyojua si kama utabiri wa hali ya hewa kwamba kuna 80% ya mvua. Yeye anajua kitu kamili hakina utata. Sasa kama anajua hivyo, ina maana mtu muuaji, alimjua huyu atakuwa muuaji kabla hata hajazaliwa. Na muuaji huyo hawezi kuepuka kuua hata afanye nini. Kwa sababu kuepuka kuua wakati Mungu kashajua huyu ataua ni kum prove Mungu wrong. Sasa kama huyu mtu anaenda kuwa muuaji, na hana jinsi ya kuepuka hilo, tutasemaje ana uhuru wa kuamua na anaua kwa uamuzu wake na atahukumiwa motoni kwa uuaji?

5. Mbona hivyo vitabu vinavyosemwa ni vya Mungu vina contradictions lukuki?

6. Mbona huyo Mungu mnayemsema yupo hathibitishiki? Anajificha asijulikanw vizuri kwa nini? Kwa nini hakufanya ulimwengu uweze kumjua vizuri bila uwezo wowote wa kuwepo ubishi juu ya uwepo wake?

7. Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote anaweza kuumba jiwe zito sana kiasi yeye mwenyewe ashindwe kulibeba? Akiweza kuumba jiwe hilo, atakuwa hawezi yote, maana kuna jiwe atakuwa kashindwa kulibeba. Akishindwa kuumba jiwe hilo, atakuwa hawezi yote maana kuna jiwe atakuwa kashindwa kuliumba.

8. Kwa nini Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, ameruhusu kifo kitenganishe wapendanao, baba na mama, wazazi na mtoto, marafiki etc, wakati alikuwa na uwezo, ujuzi na upendo wote wa kuumba ulimwengu ambao kifo hakiwezekani kuwepo?

Kwa nini watetezi wa Quran waajitapa sana kusema vitu fulani vichache vimethibitishwa kisayansi, kuinadi Quran kama kitabu cha ukweli, wakati vingi sana vina contradictions ama vinapingana na sayansi ama havijathibitishwa kisayansi, hawasemi vinapingana nansayansi au havijathibitishwa kisayansi?

10.Kama kuna Mungu kweli, kwa nini karuhusu confusion ya dini nyingi tofauti kuwa na vitabu vingi tofauti vyote vinasema vya Mungu wa kweli?
Kwa leo tuishie na maswali haya 10.

Unaweza kujibu?
 
Sijatumia logic sababu elimu ya mantiki imekuja baada ya watu kumakinika katika mambo mengi sana,kumakinika katika kuujia uweli,kumakinika katika kujua kujenga hoja.

Kama una amini wakina Thales,Homeri,Aristosto,Socrates na wengine walikuja baada ya mitume kadhaa kupita ujue elimu ya mantiki ni ujinga wa kupuuzwa sababu watu walikuwa wameshaelimika kitambo sana.


Ila hawa waitwao wanafalsafa waliamua kiacha dini kwa hiyari zao wenyewe ndio maana wakapotea wao na wakawapoteza wenzi wao.

Nakuja..........!
Logic ni nini?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom