Makonda nashauri utumie usafiri wa fisi Kanda ya Ziwa, utakuwa mwamba usiotikisika milele!

Kambi ya Fisi

JF-Expert Member
Feb 3, 2018
13,513
21,992
Ushatumia aina nyingi za usafiri kama vile bodaboda, bajaji, ndege, kimbinyiko, farasi n.k.

Upo kanda ya ziwa sasa kwa nini upande fuso? Huo sio usafiri wa wajanja huko kanda ya ziwa, wajanja wa huko hawatumii fuso wala gari la aina yoyote ile bali hutumia fisi.

Jaribu kutumia Fisi kama usafiri huko utakuwa mwamba usiotikisika milele, ataua kabisa upinzani ndani na nje ya chama maana hautakuwa mjanja tu bali mbabe kitaifa.

Usipuuze ushauri wa kambi ya fisi.
 
Nimefatilia kwa karibu tangu ndugu Makonda aliporudishwa chamani kama Katibu Mwenezi nimegundua kwamba Watanzania walimmiss sana katika utendaji wake.

Ujio wa Mwenezi huyu umedhihirisha wazi Watanzania wengi wameupokea kwa moyo mkunjufu wameufurahia.

Katika ziara zake zote inaonyesha ni namna gani Watanzania wanampenda tofauti na habari za watu wachache mtandaoni wanaomchafua.

Nimejaribu kuangalia mahaba ya watanzania Makonda anapendwa sana na Watanzania kuliko Nape na Januari.
 
1699853204423.jpg
 
Screenshot 2023-11-13 104209.png

Wote tumeshuhudia kazi kubwa na njema inayofanywa na mwenezi wa CCM komredi Makonda tangu ateuliwe kushika nafasi hiyo.

Napenda kuwaalika wote wenye Mapenzi Mema na Taifa letu karibuni katika uzi huu wa Ushauri kwa kiongozi wetu huyu.

Ushauri wenu utafanyiwa kazi kwani ukimshauri komredi Makonda ndio umekishauri Chama.

Mungu wa Mbinguni awabariki.😀

Karibuni!
 
Back
Top Bottom