Makonda: Hii dunia sio mali ya Mungu

Makonda: Hii dunia sio mali ya Mungu

Kwann kubishana na mpumbavu?huyo ni wa shetani ni kawaida kwa binadam anapokuwa ktk madaraka
 
Bado miaka nane tu....JPM ataondoka....mkuu wa mkoa nae ajiandae kuondoka nae...JPM mwenzake atakua anastaafu..sijui yeye atakua anaenda kufanya nn?
Nani kakwambia bado miaka nane, nani kakwambia ataondoka
 
Huyu bwana mdogo ameenda mbali kwa kusema hii dunia sio ya mwenyezi Mungu. Je nani muumba wa dunia hii na viumbe vilivyomo. Ni kosa kutafuta kiki za kisiasa kwa kumhusisha Mwenyezi Mungu.

Yaani kwakuwa kaongea mtu unayemchukia unatoka povu, Tena yeye anaamini Mungu yupo..mbona wanasayansi wengi tu wanaamini hakuna Mungu na hamshtuki? Wameewaandikia mpaka kwenye mavitabu ya Geography na biology na mnavisoma vizuri tuu.
 



Mpelekeeni taatifa Mkuu wa mkoa wa dar es salaam mwambieni kwa niaba ya watumishi wote duniani nampinga kwa maandiko zaidi ya saba yanayokanusha uongo aliouongea hadharani:-

1.kwanza hapo mwanzo MUNGU aliziumba mbingu na dunia.

2.Baba anaitwa Muumba wa mbingu na nchi (dunia)

3.Isaya 45:18
Maana BWANA, aliyeziumba mbingu, asema hivi; Yeye ni Mungu; ndiye aliyeiumba dunia na kuifanya; ndiye aliyeifanya imara; hakuiumba ukiwa, aliiumba ili ikaliwe na watu; Mimi ni BWANA, wala hapana mwingine.

4.Isaya 66:1
BWANA asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu......

5.Mathayo 28:18
Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.

6.Paulo anasema katika Waefeso 3:14-15
Kwa hiyo nampigia Baba magoti,ambaye kwa jina lake ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa,

7.makonda asichanganye maandiko ,MUNGU anasema anatawala mbinguni na duniani ,maana yake utawala wake upo hapa tayari,dola ipo hapa,usalama wa taifa la duniani tuko hapa tukishirikiana na usalama wa mbinguni......mwambieni aendelee
tu na siasa ,mambo ya MUNGU atuachie tunaotetea maslahi ya MUNGU wa mbingu na dunia!

Nukuu toka kwa Kuhani Philemon Mwansepe

(Zab 24:1)Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana, Dunia na wote wakaao ndani yake.

The earth is the LORD' s, and the fulness thereof; the world, and they that dwell therein.

MITHALI 16:18 Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.

Ni wenye Akili tu na Wanaosoma Neno na kuongozwa na Roho Mtakatifu wataelewa Makonda alimaanisha nini.
 
Nilichogundua ni kuwa kuna watu wanamchukia sana Makonda, hata angefanya jema lipi hakuna anaeona, ktk hiyo clip kwa upeo wangu sidhani kama kuna ubaya ameuongea kinachofanya jambo hili kuonekana kubwa ni chuki za kisiasa jambo hili hili lingefanywa na mtu mwingine lingepuuzwa na wala kusingekuwa na mjadala humu JF. Tujaribu kuwatia moyo viongozi wetu wanapofanya vizuri tuwapongeze pia wafanyapo vibaya tuwakosoe nao ni binadamu kama sisi hakuna mkamilifu chini ya jua.
 
Kwa mujibu wa biblia Makonda yuko sahihi maana ni biblia hiyohiyo imemtaja Shetani kuwa baba wa ulimwengu huu. Maana ya baba wa ulimwengu ni mwenye mamlaka ya juu hapa Duniani. Tusome biblia zetu vizuri jamani. Ni kweli kuwa Mungu aliumba mbingu na nchi/Dunia lkn baada ya uasi shetani alijitwalia sehemu kubwa ya uongozi wa Dunia hii na ndomana hata katika biblia hiyohiyo baada ya Yesu kutoka mlimani kwenye mfungo wa siku 40 alijaribiwa na shetanji kwa namna tofautitofauti ikiwa ni pamoja na kuahidiwa Mali zote za Dunia hii endapo angekubali kumuabudu shetani! Ni nani aweza kuahidi kutoa mali asiyokuwa na mamlaka nayo!!? Mpaka hapo tunagundua kuwa shetani alikuwa na ana mamlaka ya juu hapa Duniani, maana kama ameweza kumjaribu na kumshawishi Yesu kristo ambaye kwetu Wakristo ni Mwana wa Mungu, Bwana na mwokozi wa maisha yetu basi shetani yu'na mamlaka ya juu sana hapa Duniani. <br />Tusome biblia zetu jamani.

Ni sawa na sisi kuwa Watanzania.....tumkane Mungu kwa kuwa ardhi hiyo inatawaliwa na wenye mamlaka ni Watanzania. Ni kwa muda tu....ni sawa na mpangaji.......haitofautiani na kutembea na mke wa mwenye nyumba uliko panga....maana unaweza hata ukaoa lakini siku mwenye nyumba akikoroma huna chako.
 
Pale Bashite anapojifanya anajua maandiko ya Bibilia msishowe anakufuru tu.
Dah wale waliosoma Albadir mwoneeni huruma huyu chalii [emoji23]
 
Kimaandiko yupo sawa kabisa. Ni chuki zenu mnatokwa povu bila ya kuuliza.
 
MTU aliyefeli mtihani wa kidato cha NNE atapata wapi akili ya kuchambua biblia kwa usahihi??? Ushindwe kujua dhana rahisi ya evolution, kisha uje ujue kuchambua Biblia?
 
Back
Top Bottom