Makonda asipokonda basi ataishia Makondeko

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,634
697,869
Tutofautishe nyakati
Tutofautishe nguvu
Tutofautishe ubabe
Tutofautishe uthubutu
Tutofautishe nafasi za kimamlaka serikalini na kwenye chama cha siasa

Ukatibu mwenezi wa chama ni tofauti kabisa na u DC ama u RC.. Ukiwa DC wewe ndio rais wa wilaya.. Yaani kiwilaya hakuna mamlaka mengine ya juu zaidi
Ukiwa RC wewe ndio rais wa mkoa hakuna nafasi ya juu zaidi kimkoa kuzidi hiyo.. Vyombo vyote vya ulinzi na usalama viko chini yako na una amri ya kimamlaka juu yao
Ukiwa katibu mwenezi wa chama huna madaraka ya kimamlaka na cycle ya watu inayowajibika kwako ni ndogo sana.. Na huna say ya mwisho kwenye lolote.. Ni lazima upokee maagizo kutoka juu
Kwenye hiyo nafasi ya kichama hakuna kamati ya usalama yenye kukusikiliza wewe ..na huna uwezo wa kusweka watu ndani utakavyo!

Makonda alipaishwa kipindi cha mkono wa chuma usioogopa kitu naye akapaa na kuenea vema.. Maguvu na ubabe bila staha kwa mkubwa wala mdogo ndio vilikuwa hobby yake! Alijisikia furaha sana,kudhalilisha yeyote kutokana na madaraka ya kimamlaka aliyokuwa nayo

Sasa hizi ni nyakati tofauti sana na zile.. Na nafasi aliyonayo haina nguvu ya kuamrisha kama zile nyingine... Na kibaya zaidi ndani ya chama kuna mipasuko kama ardhi ya kiangazi.. Huko hakuna ubabe na kuamrisha.. Na kuteuliwa kwake kumezidisha mipasuko.. Kwahiyo ni mwendo wa mitifuano nyuma ya zulia na mitafutano...

Mpaka hapo keshapwaya pakubwa.. Badala ya kung'ara na kuwika anaweza kufunikwa na wanazi wa chama asisikike wala asifurukute kabisa.. Kwakuwa hata ndani ya chama ana maadui wa kutosha sana!

Kitakachomuokoa labda awe kawekwa hapo kwa muda ili kusoma upepo kabla hajapewa nafasi inayoendana na kaliba yake ya kupayuka, kudhalilisha na kutumia maguvu hata panapohitaji diplomasia

Akiachwa hapo atakonda mpaka atapepesuka mwisho tukamuokote Makondeko
IMG-20231023-WA0044.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tutofautishe nyakati
Tutofautishe nguvu
Tutofautishe ubabe
Tutofautishe uthubutu
Tutofautishe nafasi za kimamlaka serikalini na kwenye chama cha siasa

Ukatibu mwenezi wa chama ni tofauti kabisa na u DC ama u RC.. Ukiwa DC wewe ndio rais wa wilaya.. Yaani kiwilaya hakuna mamlaka mengine ya juu zaidi
Ukiwa RC wewe ndio rais wa mkoa hakuna nafasi ya juu zaidi kimkoa kuzidi hiyo.. Vyombo vyote vya ulinzi na usalama viko chini yako na una amri ya kimamlaka juu yao
Ukiwa katibu mwenezi wa chama huna madaraka ya kimamlaka na cycle ya watu inayowajibika kwako ni ndogo sana.. Na huna say ya mwisho kwenye lolote.. Ni lazima upokee maagizo kutoka juu
Kwenye hiyo nafasi ya kichama hakuna kamati ya usalama yenye kukusikiliza wewe ..na huna uwezo wa kusweka watu ndani utakavyo!

Anaconda alipaishwa kipindi cha mkono wa chuma usioogopa kitu naye akapaa na kuenea vema.. Maguvu na ubabe bila staha kwa mkubwa wala mdogo ndio vilikuwa hobby yake! Alijisikia furaha sana,kudhalilisha yeyote kutokana na madaraka ya kimamlaka aliyokuwa nayo

Sasa hizi ni nyakati tofauti sana na zile.. Na nafasi aliyonayo haina nguvu ya kuamrisha kama zile nyingine... Na kibaya zaidi ndani ya chama kuna mipasuko kama ardhi ya kiangazi.. Huko hakuna ubabe na kuamrisha.. Na kuteuliwa kwake kumezidisha mipasuko.. Kwahiyo ni mwendo wa mitifuano nyuma ya zulia na mitafutano...

Mpaka hapo keshapwaya pakubwa.. Badala ya kung'ara na kuwika anaweza kufunikwa na wanazi wa chama asisikike wala asifurukute kabisa.. Kwakuwa hata ndani ya chama ana maadui wa kutosha sana!

Kitakachomuokoa labda awe kawekwa hapo kwa muda ili kusoma upepo kabla hajapewa nafasi inayoendana na kaliba yake ya kupayuka, kudhalilisha na kutumia maguvu hata panapohitaji diplomasia

Akiachwa hapo atakonda mpaka atapepesuka mwisho tukamuokote MakondekoView attachment 2793723

Sent using Jamii Forums mobile app
Umepaniki broo

Relax

Kunywa maji kwanza

Susha pumzi kisa pandisha kidogo

Aaahaaaa


Makonda ataua watu
 
Badala ya kung'ara na kuwika anaweza kufunikwa na wanazi wa chama asisikike wala asifurukute kabisa.. Kwakuwa hata ndani ya chama ana maadui wa kutosha sana!
Vita vya Panzi furaha Kwa kunguru.
Mama ana sambaratisha makundi kiintelijesia hapa,
Kwa yeye mzanzibari makundi ya Tanganyika Hana faida nayo na za ndani zaidi ni kama vile anatekeleza protocol ya IMF kuwa nchi lazima ikabidhiwe upinzani by All means Necessary.
 
Back
Top Bottom