Nov 05, 2023 06:50 UTC
Shirika la Habari la Mehr limeripoti habari hiyo na kuongeza kuwa, mashambulio ya anga ya utawala wa Kizayuni dhidi ya maeneo tofauti ya raia katika Ukanda wa Ghaza yanaendelea huku mizinga ya jeshi la utawala huo ikiteketeza kwa moto maeneo tofauti ya eneo hilo.
Shirika hilo limezinukuu Kataib za al Qassam, Tawili la Kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS zikisema kuwa zimefanikiwa kuangamiza wanajeshi watano wa utawala wa Kizayuni huko kaskazini magharibi mwa mji wa Ghaza. Taarifa ya al Qassam imesema: Wanajeshi watano wa adui wameangamizwa katika mtego waliokuwa wamekewa na wanamapambano wetu kwenye nyumba moja na wengine kadhaa wamejeruhiwa. Tumewashambulia vikali kwa maroketi, wanajeshi Wazayuni.