Kumekucha
Dmitry Medvedev Mkuu wa Baraza la Usalama wa Taifa la Russia ametahadharisha kuwa, oparesheni ya nchi kavu ya Israel itafuatiwa na taathira nzito na za umwagaji damu.
Shirika la habari la IRNA limeripoti kuwa, Dmitry Medvedev leo Ijumaa ameandika katika mtandao wa Telegram kwamba: Msijidanganye. Oparesheni hiyo itaambatana na matokeo mabaya sana na umwagaji damu mkubwa. Medvedev ameendelea kuandika: Nchia za Magharibi zimeichoka sana Ukraine na sasa zinaiunga mkono Israel.
Wanamapambano wa Palestina katika kujibu jinai za Wazayuni mkabala wa raia wa Palestina, tangu tarehe 7 mwezi huu wa Oktoba wameanzisha oparesheni kwa jina la Kimbunga cha Al Aqsa kuanzia Ukanda wa Ghaza dhidi ya ngome na vituo vya utawala wa Kizayuni katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu; oparesheni ambayo iliambatana na kufeli taarifa za kijasusi za utawala huo na kuwashangaza wanajeshi na watawala wa utawala ghasibu wa Israel.
Dmitry Medvedev Mkuu wa Baraza la Usalama wa Taifa la Russia ametahadharisha kuwa, oparesheni ya nchi kavu ya Israel itafuatiwa na taathira nzito na za umwagaji damu.
Shirika la habari la IRNA limeripoti kuwa, Dmitry Medvedev leo Ijumaa ameandika katika mtandao wa Telegram kwamba: Msijidanganye. Oparesheni hiyo itaambatana na matokeo mabaya sana na umwagaji damu mkubwa. Medvedev ameendelea kuandika: Nchia za Magharibi zimeichoka sana Ukraine na sasa zinaiunga mkono Israel.
Wanamapambano wa Palestina katika kujibu jinai za Wazayuni mkabala wa raia wa Palestina, tangu tarehe 7 mwezi huu wa Oktoba wameanzisha oparesheni kwa jina la Kimbunga cha Al Aqsa kuanzia Ukanda wa Ghaza dhidi ya ngome na vituo vya utawala wa Kizayuni katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu; oparesheni ambayo iliambatana na kufeli taarifa za kijasusi za utawala huo na kuwashangaza wanajeshi na watawala wa utawala ghasibu wa Israel.