Makapuku Forum

3. Man Utd Vs Man City ( Manchester Derby )

Mechi hii inawakutanisha mahasimu wawili wa jijini Manchester ambapo walikutana kwa mara ya kwanza 1881.
Manchester United ndio ambao wana mafanikio zaidi dhidi ya City.
Upinzani wa mechi hii ulikuja kushika kasi mara baada ya Tajiri wa kiarabu Sheikh Mansour kuinunua timu hiyo mwaka 2008 na kuanza kuleta upinzani.





 
Zinapo kutana hizi timu huwa wanakamiana sana
 
Ngoja nione no 1,nilijua Kati cit na United au arsenal na Tottenham watachuana kwenye no 1
 
2. Arsenal Vs Tottenham Hotspur ( North London Derby )

Wapinzani wa Kaskazini ya London, ni moja kati ya mechi zenye mvuto zaidi katika ligi ya EPL. Japokuwa Arsenal ndio huwa anatawala kwa kushinda katika mechi hii ila miaka ya karibuni hali imebadilika Spurs nao wamekuwa moto wa kuotea mbali.

Mechi hii huwa haina uhasama mkubwa wa mashabiki ukilinganisha na mechi nyingine. Ila mwaka 2002, Nahodha Sol Campbell alipohama kutoka Spurs kwenda Arsenal alileta dhahama kubwa kiasi cha kuitwa Yuda na mashabiki wa Spurs.




 
Moja ya derby ambayo siku hizi inapoteza mvuto kiukweliii sijui labda kwa sababu siku hizi mambo ya mpira pesa inasumbua ila yote sawa kipindi kile ilikuwa tamu aiiseeeh ukifatiliaa

Kipindi cha 1894 ambao huu mwaka hawa sunderland walioshuka daraja na moyes wao
ndo walinyakuwa makwapa kwa kubeba ndoo huku derby ya kwanza liverpool anakula bao 3 nunge ....daaaaah bwanaabwaaanaa ukifatiliaa japo ilikuwa black and white na mijeziii mikubwa watu walikuwa wanajituma
Licha ya kuwa Neville ndo anarekodii nzuri ya kicheza derby hii mara nyingi ila huwez kuwaacha hawa watu...





Hizo pipooo zilikuwa hatariii..apa tunamzungumzia tom wyllie,John Heydn,kevin shedy peter Beardsley na wengineo kibao



 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…