
ZABURI 121
1.Nitayainua,macho yangu niitazame milima ,Msaada wangu utatoka wapi?
2.Msaada wangu u katika Bwana ,Aliyezifanya mbingu na nchi.
3.Asiuache mguu wako usogezwe,Asisinzie akulindaye
4.Naam,hatasinzia wala hatalala usingizi,yeye aliye mlinzi wa Israel.
5.BWANA ndiye mlinzi wako,BWANA ni uvuli mkono wako wa kuue.
6.Jua halitakupiga mchana,wala mwezi wakati wa usiku.
7.BWANA atakulinda na mabaya yote,Atakulinda nafsi yako.
8.BWANA atakulinda utokapo na uingiapo,Tangu sasa na hata milele.
TUOMBE
Asante Baba kwa ulinzi wako,toka asubuhi mpaka muda huu.
Tunaomba malaika walinzi wazunguke vitanda vyetu,tulaze salama na utuamshe salama tena kesho asubuhi.
Ponya wagonjwa,fariji wafiwa ,watie nguvu wajane na yatima nawakumbuke waluovunjika moyo kuwa lipo tumaini kwako.
Tunakuomba utufunike kwa damu takatifu inenayo mema.
Asante Baba kwakuwa utatenda sawa na mapenzi yako.
Tunaomba na kushukuru
Amen
USIKU MWEMA
