Wachezaji watakaotundika daruga wikiendi hii na ijayo.
Philip Lahm - Bayern Munich
Anacheza mechi yake ya mwisho ya kiushindani leo kabla ya kustaafu soka akiwa ametumikia timu hiyo maisha yake yote ya soka. Hajawahi kuhama klabu.
Xabi Alonso - Bayern Munich.
Kiungo huyu fundi wa kukaba, naye anacheza mechi yake ya mwisho leo kabla ya kutundika daruga. Ameshinda kila kitu katika soka.
Fransisco Totti - As Roma.
Maarufu kama El Capitano de la Roma, amechezea klabu yake ya As Roma na hajawahi kuhama, wakati ni ukuta, ameamua kustaafu soka mara baada ya umri kumtupa mkono.
Anaheshimika sana ndani ya Roma kiasi cha mashabiki wake kudai kuwa baada ya Papa anayefatia kwa umaarufu ni Totti.
Dirk Kuyt - Feyernood.
Anastaafu soka mara baada ya safari ndefu ya mafanikio japo sio makubwa sana. Staa huyu wa zamani wa Liverpool atakumbukwa daima kwa aina yake ya mchezo anaocheza wa kutokata tamaa.