Muziki: It is Almost Furahiday
Habari Makapuku wenzangu, poleni na mihangaiko ya siku nzima na kama kawaida, kesho ni siku nyingine tena na kama jua halikung'aa leo basi nani anayajua ya kesho.
Karibuni tena katika ka-kipengele kafupi ka muziki na hasa tukijikita kwenye utamu wa gitaa. ndiyo, tunaangalia udonoaji wa gitaa katika muziki/wimbo ambao bahati mbaya sana huwa nauchagua (labda wakati mwingine unaweza kupendekeza wimbo ambao unadhani gitaa linasikika vizuri na tukauangalia pamoja)
Hongera Timu ya Taifa ya Vijana, kazi nzuri na n9i ninyi wenyewe ndo mtaamua hatma yenu katika soka.
Leo tupo Africa Mashariki na tunasogea kwa majirani na watani zetu waKenya. Hapo tunamkuta mwanamuziki maarufu kwa nyimbo za kiharakati na hasa mapambano dhidi ya rushwa na ulevi wa madaraka.
Anaitwa Eric Wainaina, inawezekana huyu ndiye akawa ni mwanamuzi mwenye mafanikio makubwa zaidi katika EAC (siongelei mafanikio ya kifedha, mafanikio ya kimuziki ni zaidi ya mwanamuziki kumiliki fedha- fiat money etc), keshafanya muziki na wanamuzi wakubwa duniani akiwemo Baaba Maal, Angelique Kidjo na Chakachaka.
Keshatumbuiza katika tamasha la World Cup 2010 (yote ufunguzi na ufungaji). Mshindi wa tuzo za Kora na kashiriki matamasha kadhaa maarufu duniani ikiwemo Sauti za Busara.
Huyu ndiye Eric Wainaina, ambaye hupiga gitaa na muziki wake ni mchanganyiko wa Benga muziki asili ya Kenya na ladha za EAC hususani pande za Kongo.
Anajulikana zaidi kwa wimbo wake Nchi ya KItu Kidogo, wimbo ambao ulimpa nafasi ya kufanya kazi na UN na mashirika yake katika harakati za kupambana na Rushwa.
Ninapenda anavyopiga gitaa lake na ninakushirikisha usiku huu kumsikiliza katika wimbo wake wa Nchi ya Kitu Kidogo