Makapuku Forum

Makapuku Forum

f83937be3285fafda195efef3cd5ac45.jpg

I can't believe
.....
 
Kifo kifooo...kifo hakina huruma
Enzi hizo Dr alitamba na demu wake wa kizungu(Mama Kally Ongala)
Mwanawe Kali Ongala nakumbuka alivyoisaifia Yanga kutamba kwenye Klabu Bingwa Afrika Mashabiki huko Kampala sijui mwaka 1999 maana nilikuwa kadogooo....Yanga iliondoka na ndio huku Kali(Siku hizo sijui kocha Wa Maadui) aling'ara vilivyo
......
Yanga ya mwaka 1993 iliyoshiriki Kombe la Chalenji huko Kampala ilikuwa na Edward Edibily Jonas Lunyamila ambapo alikuwa gumzo sana unaambiwa magari ya huko mengi yaliandikwa Jina la staa huyo baada ya kumfunika staa wa kiganda Majid Musisi.

Yanga ilikuwa na akina Keneth Mkapa, Said Mwamba Kizota na mastaa wengineo.
 
Yanga ya mwaka 1993 iliyoshiriki Kombe la Chalenji huko Kampala ilikuwa na Edward Edibily Jonas Lunyamila ambapo alikuwa gumzo sana unaambiwa magari ya huko mengi yaliandikwa Jina la staa huyo baada ya kumfunika staa wa kiganda Majid Musisi.

Yanga ilikuwa na akina Keneth Mkapa, Said Mwamba Kizota na mastaa wengineo.
841ace79cd4fdfaee48cad9ab6af80ff.jpg
Hiki kikosi sijawahi kukishuhudia kikicheza
Zaidi nasikia tu simulizi japo nimewahi kuwashuhudia baadhi tu hasa Kizota na Lunyamila
.....
 
Oscar Kambona alikuwa ni mmoja kati marafiki wakubwa watatu almaarufu kama 3K. Yaani Kambarage, Kawawa na yeye mwenyewe Kambona.

Oscar Kambona alikuwa ni mmoja mwa miongoni mwa marafiki watatu walioshibana ambao walijulikana kama 3K. Yaani Kambarage, Kawawa na Kambona.

Yeye alikuwa ni msomi haswa na mjanja mjanja yaani mtoto wa mjini.

Tofauti na Kawawa ambaye yeye alikuwa ni mtu wa kukubali kila alichoambiwa na Nyerere.

Oscar Kambona aliombwa na Nyerere arudi nyumbani kutoka Uingereza ili waje kujenga Nchi na haishangazi Oscar akawa Waziri wa Kwanza kabisa wa Mambo ya Nje na Ulinzi.

Ujanja na akili za Oscar zilimuogopesha Nyerere akawa yuko makini nae na hata alipoamua kujiuzulu Uwaziri Mkuu na kumuachia Kawawa nchi kwa mmoja ili yeye akajenge chama mikoani aliamua amuachie Kawawa maana angemuachia Kambona asingekuja kupata tena madaraka yake.

Januari 20 mwaka 1964 Jeshi lilipoasi na kutaka kumpindua Nyerere, ni Oscar Kambona ndiye aliyezima maasi ya jeshi wakati ambapo Nyerere na Kawawa walikuwa Mafichoni huko Kigamboni kwa siku mbili wakishindia mapapai.

Baada ya hali kutulia, Kambona alimwambia Nyerere arudi aongoze nchi na kweli mwalimu akarudi akaendelea kutawala na akalivunja jeshi ndipo JWTZ ilipozaliwa Septemba 1 mwaka 1964.

Nyerere kuanzia tukio hilo akaanza kukosa amani na Oscar na kuanza kumpotezea mdogomdogo katika mambo yake muhimu.

Ilipofika mwaka 1967, Mwalimu akaja na wazo la sera ya Ujamaa huku akitambulisha Azimio la Arusha, ni kupitia sera hii Oscar Kambona akampinga hadharani Mwalimi Nyerere juu ya muundo wa sera na itikadi za Ujamaa akidai kwamba Nchi badala ya kupiga hatua mbele, badala yake itapiga maendeleo nyuma. Vilevile alipinga sera ya mfumo wa chama kimoja na uanzishwaji wa Vijiji vya Ujamaa. Hivyo Oscar akasema haungi mkono sera hiyo. Akatofautiana rasmi na Nyerere.

Nyerere akamuamishia Oscar katika wizara ya maendeleo vijijini ili kupunguza nguvu ya Oscar. Lakini asikuambie mtu, Oscar akaanza kuwa maarufu kila alipotembelea katika ardhi hii ya Tanzania. Style yake ya kunyoa ilikua maarufu kipindi hiko na ikawavutia walio wengi, ilijulikana kama Kambona style.

Baada ya Umaarufu kuwa mkubwa Oscar aliutaka Urais jambo ambalo Nyerere hakuliafiki hivyo akapewa masaa 24 asiwepo Nchini vinginevyo angekamatwa na kuwekwa kizuizini.

Oscar akatoroka kupitia Kenya na baadae Uingereza ambapo akiwa huko akawa anaratibu mipango ya kumpindua Nyerere Oktoba mwaka 1969 katika Jaribio la pili kati ya Majaribio matatu ya Kumpindua Nyerere kwani alikuwa anatuma pesa kwa akina Bibi Titi Mohamed lakini mpango huo ukakwama na akina Bibi Titi wakakamatwa na kuwekwa Kizuizini kwa amri ya Rais.

Oscar akajichimbia Uhamishoni Uingereza huku nchini akionekana kama Mhaini na Msaliti hivyo historia yake ikaanza kufutwa na kutungiwa nyimbo za kumdhalilisha kwamba ameolewa huko Uingereza. Nyimbo hizo zilikuwa zikiimbwa hukoMashuleni na hata Jeshini JKT.

Mwaka 1992 Oscar Kambona alirudi nyumbani lakini akiwa ameshazeeka, aliyekuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Ndani Agustino Mrema akatangaza atamkamata ili akajibu kesi yake ya Uhaini, lakini Mwalimu Nyerere akasema muacheni nimeshamsamehe.

Alikaa mpaka mwaka 1997 kabla ya kushikwa na maradhi akarudi Uingereza kutibiwa na kufariki kabla ya mwili wake kurudishwa nyumbani ni kwenda kuzikwa kwao huko Songea.

Huo ndio ukawa mwisho wa Oscar Kambona, mmoja kati ya wasomi wa kwanza kabisa nchini pamoja na waasisi wa Muungano.

Hivyo yoyote aliyejaribu kupambana na Mwalimu alipotezwa, kuanzia yeye mpaka historia yake. HISTORIA yake imefunikwa na watawala.

Ni mmoja kati ya wanasiasa bora kuwahi kutokea nchi hii ambao hawakuwahi kuwa Marais kando ya Mark Mwandosya, Salim Ahmed Salim na Edward Sokoine.

Adui wa Nyerere alifanywa adui wa Taifa.
Historia kuntu kabisa, Asante musollin
 
Kifo kifooo...kifo hakina huruma
Enzi hizo Dr alitamba na demu wake wa kizungu(Mama Kally Ongala)
Mwanawe Kali Ongala nakumbuka alivyoisaifia Yanga kutamba kwenye Klabu Bingwa Afrika Mashabiki huko Kampala sijui mwaka 1999 maana nilikuwa kadogooo....Yanga iliondoka na ndio huku Kali(Siku hizo sijui kocha Wa Maadui) aling'ara vilivyo
Yanga walimchukua kutokea Abajalo ya Sinza
......
Chini ya kocha Rauli Shungu
 
Yanga ya mwaka 1993 iliyoshiriki Kombe la Chalenji huko Kampala ilikuwa na Edward Edibily Jonas Lunyamila ambapo alikuwa gumzo sana unaambiwa magari ya huko mengi yaliandikwa Jina la staa huyo baada ya kumfunika staa wa kiganda Majid Musisi.

Yanga ilikuwa na akina Keneth Mkapa, Said Mwamba Kizota na mastaa wengineo.
yanga hii nahisi ndio iliimbwa na Pepe kale
841ace79cd4fdfaee48cad9ab6af80ff.jpg
Hiki kikosi sijawahi kukishuhudia kikicheza
Zaidi nasikia tu simulizi japo nimewahi kuwashuhudia baadhi tu hasa Kizota na Lunyamila
.....
 
Yanga ya mwaka 1993 iliyoshiriki Kombe la Chalenji huko Kampala ilikuwa na Edward Edibily Jonas Lunyamila ambapo alikuwa gumzo sana unaambiwa magari ya huko mengi yaliandikwa Jina la staa huyo baada ya kumfunika staa wa kiganda Majid Musisi.

Yanga ilikuwa na akina Keneth Mkapa, Said Mwamba Kizota na mastaa wengineo.
Majid Mussisi. SC Villa

Jackson Mayanja. Express

Wawe timu ya taifa beki no 2au 3 kazi unayo
 
841ace79cd4fdfaee48cad9ab6af80ff.jpg
Hiki kikosi sijawahi kukishuhudia kikicheza
Zaidi nasikia tu simulizi japo nimewahi kuwashuhudia baadhi tu hasa Kizota na Lunyamila
.....
Nimekisikia tu, huyo Constantine Kimanda alikuwa ni Mkongomani, unaambiwa ni beki wa kati wa aina yake.

Said Nassoro Mwamba Kizota enzi hizoakicheza kama Straika, baada ya kasi kupungua akarudi kucheza Sentahafu ambapo hapo ndipo alipopewa jina la Kizota kutokana na aina yake ubabe na undava hali iliyofanya kuogopwa sana na Washambuliaji wengi.

Ikumbukwe Said Mwamba Kizota alipewa jina hilo la Kizota kama utani kutokana na eneo la Kizota lililopo Dodoma ambalo lilikuwa linaogopwa na viongozi wengi waliokuwa wanafanua makosa enzi ya utawala wa Jk Nyerere kwani hapo ndipo ofisi za chama zilipokuwa hivyo ukifanya kosa unaitwa Kizota mjini Dodoma ili uhukumiwe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom