Makapuku Forum

Sasa mkuu hiyo alama ya kiulizo (?) tunaiondoaje juu ya hayo maji?
 
TUCHUKULIANE

WAGALATIA 6

1 Ndugu zangu mtu akighafilika katika kosa lolote ,ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole ,ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe

2 Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo

3 Maana mtu akijiona kuwa ni kitu ,naye si kitu ,ajidanganya nafsi yake

4 Lakini kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe ,ndipo atakapokuwa na sababu ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu,wala si kwa wenzake

5 Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe

WAPENDWA

Tupendane
Tuonyane
Tatizo la mwenzetu liwe letu siku zote
Tupige magoti tuombe kwa ajili ya wengine
Tuufurahie uumbaji na vyote vilivyomo

HUO NDIO UPENDO WA KWELI

MUNGU ATUSAIDIE KUCHUKULIANA MIZIGO KWA UPENDO

Asante Baba kwa kutuamsha sala ma tunaomba toba kwa yote tuliyokosa kwa mawazo maneno na vitendo tusaidie tushike mwenendo mpya

Tubariki siku ya leo tukatende ya kukupendeza

Bariki kazi za mikono yetu,safari,familia,kazi,mashamba ,masomo na yote tutakayoshiriki leo

Tujenge tupende kusikiliza neno lako na kuliishi

Tusaidie tupende kusikiliza na kujifunza toka kwa wenzetu tusiwe makwazo kwa wengine

Asante Mungu kwakuwa utatenda sawa na mpenzi yako Amen

NAWATAKIA SIKU NJEMA MBARIKIWE SANA
 
Ubarikiwe pia mama pastor
 
Asante mama mtumishi
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…