Makapuku Forum

Time will tell
 
1984 - Fernando Torres anazaliwa.

Mshambuliaji wa zamani wa Liverpool, Chelsea, Ac Milan, timu ya taifa ya Spain na kwasasa Atletico Madrid.

Ni zao la akademi ya klabu ya Atletico Madrid.

Akiwa Liverpool alikuwa ni mmoja kati ya washambuliaji bora waliotikisa EPL na kumpa wakati mgumu beki kisiki wa Man Utd Nemanja Vidic wa kumkaba pindi wanapokutana.

Torres ameshinda kila taji isipokuwa taji la ligi tu, katika timu zote alizochezea hakuwahi kushinda ubingwa wa ligi na timu aliyoichezea.

Ametwaa, Kombe la Dunia 2010 pamoja na Ubingwa wa Ulaya kwa timu za Taifa mwaka 2008 na 2012 akiwa na kizazi cha dhahabu cha Spain.
Uefa Europa League, Uefa Champions League, Kombe la FA akiwa na Chelsea.

Kwangu mimi, Torres ni mmoja kati ya washambuliaji mahiri kuwahi kuwashuhudia katika EPL, namkubali sana.

Uhamisho wake kwenda Chelsea ni moja kati ya sajili mbovu kuwahi kufanywa Uingereza kwani Torres alichemsha vibaya sana akiwa Chelsea.
 
1990 - Lev Yashin anafariki Dunia.

Maarufu kama Black Spider kutokana na kupenda kuvaa jezi nyeusi tupu awapo uwanjani.

Ni golikipa wa zamani wa USSR ambaye anatajwa kama golikipa bora wa wakati wote katika historia ya mchezo wa soka kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya takwimu.
 
Inasemekana lakini kwamba Didier alimfanyia uswahili
 
inasemekana alipigwa misumari na Drogba
 
Daima binadamu husema kilichojaa moyoni mwake lakini Mungu anamajibu :


Mithali 16:1-.maandalizi ya moyo ni ya mwanadamu ,na jibu la ulimi hutoka kwa Mungu....2 Matendo ya mwanadamu huonekana kuwa sawa machoni pake lakini Mwenyezi Mungu hupima nia ya mtu.....4 Mwenyezi-Mungu ameumba kila kitu kwa kusudi lake ,hata waovu kwa ajili ya siku ya maangamizi..

PROVERB 16:1-2The preparation of the heart belongs to man But the answer of the tongue is from the LORD....
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…