Makapuku Forum

Makapuku Forum

Yaani!!!.....sijui tuna shida gani!!!
Historia yetu imewazima na kuwasahau watu wengi sana katika Taifa hili eti tu labda walitofautiana na Waasisi wa Taifa hili kipindi hiko.

Mchango wa Oscar Kambona umesahaulika kabisa. Bila Kambona, mwalimu asingeendelea kuwa Rais wakati Jeshi lilipoasi Mwaka 1964 na Mwalimu kuamua kujificha zake Kigamboni akishindia mapapai.

Ni aibu sana kwa Taifa kuwasahau watu wa aina ya Kambona, Jumbe na wengineo.
 
Historia yetu imewazima na kuwasahau watu wengi sana katika Taifa hili eti tu labda walitofautiana na Waasisi wa Taifa hili kipindi hiko.

Mchango wa Oscar Kambona umesahaulika kabisa. Bila Kambona, mwalimu asingeendelea kuwa Rais wakati Jeshi lilipoasi Mwaka 1964 na Mwalimu kuamua kujificha zake Kigamboni akishindia mapapai.

Ni aibu sana kwa Taifa kuwasahau watu wa aina ya Kambona, Jumbe na wengineo.
Kama walivyomsahau sokoine huwezi amini
 
Ni kweli kabisa, Che Guevara ni mzaliwa wa Argentina lakini kwa mchango wake mkubwa alioufanya nchini Cuba, amezikwa huko Cuba kwa heshima zote.

Hii ni kudhihirisha watu wanajali na kuthamini nini umewafanyia na hawajali umetokea taifa gani?

Huku kwetu Dunia ya tatu, Watanganyika na Wazanzibar wamemfuta kwenye historia yao, kiongozi wa Mapinduzi mataukufu ya Zanzibar, Field Marshall John Okello eti kisa ni Raia wa kigeni, Ujinga ulioje??

Wanatuaminisha Karume ndio baba wa mapinduzi yale ya Januari 12 mwaka 1964. Upumbavu ulioje??
Tena ni upumbavu uliotukuka!!
 
1928 - Didi anazaliwa.

Ni mwanasoka wa zamani wa timu ya taifa ya Brazil.

Ameshinda Kombe la Dunia akiwa na Brazil mara mbili, Mwaka 1958 na mwaka 1962.

Katika mashindano ya kombe la dunia la mwaka 1958 yalifanyika pale Sweden, Didi alichaguliwa kuwa Mchezaji bora wa Mashindano hayo. Brazil hiyo ilikiwa na kijana wa miaka 17 aliyeiteka Dunia, alikuwa ni Pele.
Jana Dida na leo Didi!
 
Back
Top Bottom