Makapuku Forum

Makapuku Forum

2001 - George Bush anapitisha mpango wa kuanzisha idara ya kushughulika na Usalama wa ndani wa Nchi hiyo.

Bush alikuwa ni Rais wa Marekani aliyehudumu kwanzia mwaka 2000 - 2008.
IMG_20161008_082621.jpeg
IMG_20161008_082632.jpeg
 
1928 - Didi anazaliwa.

Ni mwanasoka wa zamani wa timu ya taifa ya Brazil.

Ameshinda Kombe la Dunia akiwa na Brazil mara mbili, Mwaka 1958 na mwaka 1962.

Katika mashindano ya kombe la dunia la mwaka 1958 yalifanyika pale Sweden, Didi alichaguliwa kuwa Mchezaji bora wa Mashindano hayo. Brazil hiyo ilikiwa na kijana wa miaka 17 aliyeiteka Dunia, alikuwa ni Pele.
 
1967 - Mwanamapinduzi Ernesto Che Guevara anakamatwa yeye pamoja na wafuasi wake huko Bolivia.

Alikamatwa na wanajeshi wa Bolivia kwa msaada wa CIA. Aliteswa vibaya sana kabla ya kuuwawa kikatili siku moja baadae.
1475904881539.jpg
1475904887938.jpg
Best ake fidel Castro...Mwanaharakati huyu mwanamapinduzi akumbukwe Daima na waliomuua damu yake iwe juu yao.
 
1968 - Zvonomir Boban anazaliwa.

Ni mwanasoka wa zamani wa Ac Milan na timu ya taifa ya Croatia.

Alisifika sana kwa umakini wake kupiga pasi za mwisho zenye macho na utulivu wake mkubwa uwanjani.

Haruna Moshi akaiga jina lake.
 
1928 - Didi anazaliwa.

Ni mwanasoka wa zamani wa timu ya taifa ya Brazil.

Ameshinda Kombe la Dunia akiwa na Brazil mara mbili, Mwaka 1958 na mwaka 1962.

Katika mashindano ya kombe la dunia la mwaka 1958 yalifanyika pale Sweden, Didi alichaguliwa kuwa Mchezaji bora wa Mashindano hayo. Brazil hiyo ilikiwa na kijana wa miaka 17 aliyeiteka Dunia, alikuwa ni Pele.
1475905082121.jpg
1475905090281.jpg
Wa kitambo..mhhh
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom