NUKUU NO 3#
Ziara yangu ya Tanzania imekuwa ni tukio la kunifurahisha
Lakini kwa vile Ziara yangu sasa inanichukua katika nchi nyingine, siwezi kusahau jambo jingine kuhusu Africa ambako mamilioni ya wanaume, wanawake na watoto hawana huduma nzuri za afya na Elimu.
Maneno haya yalisemwa na aliyekuwa kiongozi wa kanisa katoriki Duniani Papa John Paul wa pili. Alipokuwa akihitimisha Ziara yake ya siku tano nchini, ambapo alitoa mwito kwa mataifa mbali mbali Duniani kuungana na Africa kubolesha maisha ya watu hasa masikini
Alikuwa akizungumza katika uwanja wa kimataifa Kilimanjaro (KIA) mbele ya aliyekuwa waziri mkuu na makamu wa kwanza wa Rais, Joseph Warioba alikwenda kumuaga uwanjani hapo, September 5,1990.
Alizaliwa Mei 18,1920 na kufariki Dunia April 2,2005