Makapuku Forum

HAPPY BIRTHDAY MAKAPUKU FORUM


Nawasalimu katika upendo na amani
Leo ni miezi miwili toka Makapuku forum ianze na naomba nichukue nafasi hii kuwashukuru wote,
Shukrani za dhati ziwafikie Makapuku wote popote pale mlipo maana natambua ya kwamba bila nyie basi tusingeweza kufikia hapa tulipo. Najua wote tuna majukumu mengi ila hayo majukumu hayajawa kikwazo katika kufanikisha hili.

Vilevile nasema asante kwa ushirikiano na upendo ambao tumekuwa tukiuonyesha pamoja na sapoti ambayo tumekuwa tukipeana mpaka hatimae tumepata heshima kubwa katika jamii inayotuzunguka.


Mafanikio
Kwa miezi miwili ambayo hii thread imekuwa hewani tumeweza kuwa katika thread ambazo zinafanya vizuri zaidi hapa Jamii forum. Wote mtakuwa mashahidi kuwa hii thread ina views za kutisha na reply 48k ndani ya miezi miwili tu, na kwa matokeo haya tumezigaragaraza zile thread za miaka nenda rudi.
Mafanikio mengine ni idadi ya Makapuku kuzidi kuongezeka siku hadi siku, hii ni fahari kubwa sana kwetu kuona kuwa tunakubalika na watu wanapenda kuwa pamoja nasi, na napenda kuchukua nafasi hii kuwakaribisha wote wanaopenda kujiunga nasi, na kwa moyo mkunjufu nawaambia ya kuwa milango ipo wazi.
Mafanikio mengine tuliyopata ni pamoja na na idadi ya Makapuku katika orodha mbali mbali kuzidi kufanya vizuri.
Tunaongoza kwenye Most points na Most likes pia na nna imani very soon tutakuwa kwenye Most messages.

Mwisho napenda kusisitiza tuishi kwa UPENDO pia kusameheana na kuchukuliana, kukaa pamoja watu wengi sio kitu rahisi hivyo kwa namna moja au nyingine ni lazima kuna sehemu inatokea tunatofautiana basi tusameheane na tusonge mbele.Tuzidishe upendo pamoja na kupeana sapoti kila mahali tunapokutana kwasababu najua hatuishii hapa tu


Happy Birthday Makapuku forum

Tag wote mpaka msg hii iwafikie Makapuku wote kutoka pande mbali mbali za dunia


Nawapenda wote

Jimena
 
Umoja huu udumu. Bila shaka hata hao wakongwe wanajua kuwa makapuku is a force to be reckoned with. Tusonge mbele!
 
Nasi twakupemda
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…