Makapuku Forum

Makapuku Forum

Utafiti unaonyesha kuwa watoto huanza kugundua kejeli wakiwa na umri wa miaka 5 hadi 6, lakini mara nyingi huichukulia kwa maana halisi mwanzoni.

Wanaweza kudhani msemaji anadanganya au anajaribu kuwafanyia jambo zuri kwa kutumia kejeli.

Kwa miaka 7 hadi 10, wanaanza kuelewa ucheshi wa kejeli na kutambua kuwa inaweza kutumika kama dhihaka au ukosoaji tu wa kirafiki.

Uwezo wao wa kutambua kejeli huimarika kadri wanavyoendelea kujifunza/kuongeza ujuzi wa lugha, huruma, na uwezo wa kuzingatia vizuri mtazamo wa mtu mwingine.
Screenshot_20250616_143519_InstaPro2%20.jpg
 
Tafiti kadhaa zimeonyesha baadhi ya aina za nyani, kama sokwe, huonyesha tabia zinazofanana na “kuchepuka” kimapenzi.

Moja ya tabia hizo ni kuzuia kutoa milio ya kimapenzi, wakati wa kujamiiana ili kutowajulisha nyani wengine (hasa wale wa cheo cha juu) kuhusu tendo linaloendelea.

Katika baadhi ya matukio yaliyochunguzwa, nyani wa daraja la chini na majike huamua kunyamaza kimya kimya wakati wa kujamiiana ili wasigundulike na nyani wa daraja la juu, ambao wanaweza kuingilia, kulipiza kisasi au kuzuia uhusiano huo kuendelea.
Screenshot_20250616_143827_InstaPro2%20.jpg
 
Binadamu tunajulikana kwa kufuga wanyama kama mbwa, ng’ombe, farasi, n.k.

Kuna baadhi ya jamii ya ‘Siafu’ kama ‘Fungus-Farming Ants’ hulima uyoga kwaajili ya chakula mfano sawa na kilimo kwa binadamu.

‘Aphid-Herding Ants’ hawa hufuga ‘Aphids’ (vidukari) na huweka ulinzi dhidi ya wadudu baadae na huwakamua hao ‘Aphids’ kupata asali ambayo hutumia kwaajili ya chakula.
Screenshot_20250616_144109_InstaPro2%20.jpg
 
Baada ya tamko la Familia ya aliyekuwa Rais wa Zambia Edgar Lungu ambalo yalikuwa ni maagizo yake ya kwamba mpinzani wake wa kisiasa na Rais wa sasa Hakainde Hichilema hapaswi kufika popote karibu na mwili wake familia imefikia makubaliano na serikali juu ya mazishi ya Kiongozi Huyo na mpango wa mazishi umekamilika.

Baada ya Mazungumzo ya muda mrefu baina ya familia ya Lungu wamekubaliana kwamba Mwili wa Rais huyo wa zamani utasafirishwa kutoka Afrika Kusini kwenda mji mkuu wa Zambia, Lusaka siku ya Jumatano wiki hiii kwa ndege binafsi ya kukodi, na baada ya kuwasili utapokelewa na familia na kisha kutakuwa na heshima kamili ya Kijeshi na baada ya hapo utasafirishwa kwenda kwenye makzi yake mjini Lusaka.

Aidha wananchi wa Zambia watapata nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho kwanzia alhamis na zoezi hilo litakamilika siku ya jumamosi ambapo Mazishi ya Kitaifa yatafanyika jumapili Juni 22, 2025 na maombolezo yatakamilika jumatatu ambapo mapaka sasa bado haijajulikana endapo atazikwa katika eneo rasmi la mazishi ya Rais au katika makazi yake binafsi.

Hata hivyo msemaji wa familia Makebi Zulu katika mazungumzo yake na vyombo vya habari akiwa pamoja na Katibu wa Baraza la Mawaziri la Zambia Patrick Kangwa amesema familia hiyo imeomba radhi kwa usumbufu na maumivu ambayo mazungumzo ya muda mrefu yamesababisha ambapo amesema wamefanya kila linalowezekana kuhakikisha wanaheshimu matakwa ya kibinafsi ya Rais wa zamani.

Sambamba na hilo kwa upande wa serikali Katibu Mkuu wa serikali Patrick Kangwa amewashukuru wananchi wa Zambia kwa uvumilivu wao wakati huu mgumu ambapo kwa upande wa familia umesisitiza kuwa wanaamini kuwa Serikali haitakwenda kinyume na makubaliano yao.
Screenshot_20250616_144233_InstaPro2%20.jpg
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeahirisha kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu hadi Julai 1, 2025 kwa ajili ya kusubiri Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kupitia jalada la kesi hiyo ili kuona kama iende Mahakama Kuu au hapana.

Hatua hiyo inatokana na Upande wa Mashtaka kuomba ahirisho mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Franko Kiswaga ambapo Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga alisema jalada la kesi hiyo lipo kwa DPP analipitia kisha atatoa taarifa kuhusu upelelezi ulipofikia na kama kesi hiyo iende Mahakama Kuu au hapana.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Kiswaga ameahirisha kesi hiyo hadi Julai 1, 2025 ambapo kesi hiyo iliitishwa leo kwa ajili ya kutajwa.

Lissu anadaiwa kutenda kosa hilo Aprili 3, 2025 ndani ya Jiji la Dar es salaam kuwa siku hiyo kwa nia ya uchochezi aliushawishi umma kuzuia kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, huku akitamka na kuandika maneno kumshinikiza kiongozi Mkuu wa Serikali ya Tanzania.

Juni 2, 2025, upande wa mashtaka uliieleza Mahakama kuwa jalada la upelelezi lilikuwa limeshawasilishwa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), lakini baada ya DPP kulipitia alibainisha kuwa kuna jambo ambalo bado lilikuwa halijakaa sawa hivyo alilirejesha tena kwa wapelelezi kufanyia kazi eneo hilo.

Kutokana na taarifa hiyo, kiongozi wa Jopo la waendesha mashtaka, Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga aliomba Mahakama itoe ahirisho mpaka tarehe nyingine.
Screenshot_20250616_144353_InstaPro2%20.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom