Makapuku Forum

Makapuku Forum

Magazeti ya leo August 12, 2023.
Screenshot_20230813_070338_Opera%20Mini.jpg
 
NAHODHA wa Manchester City, Kevin De Bruyne ametumia Pauni 130,000 ( Sh 414 milioni) kuwanunulia simu aina ya iPhones kikosi kizima cha mastaa wenzake katika timu hiyo ya Etihad.
.
De Bruyne amegawa zawadi hiyo ya simu kwa wachezaji 26 kwenye kikosi cha kwanza cha Man City kabla ya mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu England dhidi ya Burnley uliofanyika uwanjani Turf Moor, juzi Ijumaa na kushinda mabao 3-0.
.
Simu hizo za iPhones kila moja iligharimu Pauni 5,000 (Sh 16milioni) na makava yake yamewekewa ubunifu wa kuandikwa majina ya wachezaji na nembo ya klabu.
.
De Bruyne mwenye umri wa miaka 32, amempa simu moja Kocha Pep Guardiola. Kiungo huyo wa Kibelgiji ameamua kufanya hivyo akiiga kile kilichowahi kufanywa na Lionel Messi ambaye aliamua kuwapa zawadi ya simu aina ya iPhone 14 pro max watu 35 waliokuwa wakiunda timu ya Argentina iliyobeba Kombe la Dunia 2022.
Screenshot_20230813_085305_Instagram.jpg
 
CHELSEA ipo tayari kutoa zaidi ya Pauni 115 milioni (Sh 367bilioni) kwenda Brighton ili kuipata huduma ya kiungo wa timu hiyo na Ecuador, Moises Caicedo, 21, katika dirisha hili la usajili baada ya wakala wa staa huyo kuiambia kwamba mchezaji anataka kujiunga nao na sio timu nyingine.
.
Mabosi wa Chelsea wanawasilisha ofa mpya ikiwa ni siku chache tangu Liverpool iripotiwe kutuma ofa ya Paunj 111 milioni ambayo ilikubaliwa na Brighton, lakini Caicedo mwenyewe aliikataa akidai kwamba anaitaka Chelsea.
.
Awali, Chelsea ilitajwa kuwa kwenye harakati za kutaka kumsajili Declan Rice kabla ya kuangukia kwa Caicedo na harakati zote hizi inazifanya ili kuziba pengo lililoachwa na kiungo N’Golo Kante aliyetimkia Saudi Arabia. Ikiwa matajiri hao wa Jiji la London watafanikisha mchakato wa kuipata huduma ya Caicedo, basi atakuwa mchezaji ghali zaidi kuwahi kusajiliwa kwenye Ligi Kuu England.
Screenshot_20230813_085530_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

TANGAZO, huku sio Marekani walipojaa Mabishoo tu! Huku ni Uarabuni walipo vyaboli wengi tu, Ronaldo anaweka mbili kambani kwenye fainali wakiwa pungufu, anabeba kiatu cha dhahabu na kombe linaenda Riyadh kwa mara ya kwanza kwenye historia ya klabu.

GOAT for a reason, hakuna maelekezo mapya Masela wote wapo kwa Bishoo wa mpira, ni kidari kweli sio kile cha kutaka upate bahati ya kutoka na Bongo Movies

Screenshot_20230813_090707_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

Kila anachokifanya Tajiri MO kwenye page zake inawachanganya sana watu, MO anaweza kuja Insta na kulalamikia kitu na wote wakaamini Simba sio shwari lakini MO anatoa mzigo mfukoni analeta wachezaji ndani ya Simba, hapo ndipo anawachanganya zaidi.

Mpaka sasa kuna MO wawili, kuna MO wa Instagram na Twitter, huyo ni MO tofauti na wa taasisi, huyu wa mitandaoni ataandika anachotaka na atavuruga anavyotaka ila MO Taasisi ana watu ambao wanafanya maamuzi on behalf ambao hawana shida na MO wa Instagram na Twitter.

Huyu MO wa mitandao ya Kijamii ana msaada mkubwa sana kwa Simba, MO huyu ataileta attention kwake hata pale timu ikicheza vibaya ama kuna kitu hakipo sawa, kumjadili yeye unaipa nafasi timu kurecover na kuendelea! MO wa Insta anampa nafasi MO wa taasisi utulivu wa kufanya vitu.

MO wa Insta ananikumbusha Tajiri wa PAOK aliyetoa silaha uwanjani tena hadharani, stori haikuwa tena timu kupoteza bali tukio la Tajiri, ananikumbusha Perez alivyoona mambo hayaendi kabisa akajiuzulu 2006 akaitoa pressure kwenye timu akaondoka nayo.

Nguvu za kutomuelewa Tajiri zihamishiwe kwenye suala la kwanini mchakato haukamiliki wa mabadiliko, zihamie kwanini watu hawanunui merchandise za klabu na hawalipii card! MO anaeleweka hata pale ambapo Mashabiki hawataki kueleweka kwa kutimiza wajibu wao! Kuna ubaya anapiga na kulipa?

The game of spinning! Tajiri MO ananikumbusha Matajiri na dunia yao! Matajiri wengine hufanya wenyewe na wengine hutuma watu kufanya kwa niaba yao! Dunia ya kitaasisi inahitaji akili sana kuielewa.
 
Jeshi la Polisi Tanzania limesema linawafuatilia ili liwakamate Watuhumiwa walioandaa na kutoa maneno ya uchochezi kama Jeshi hilo lilivyoeleza jana kupitia kwa IGP Camilius Wambura ambapo kazi hiyo inaendelea kufanyika kwa mujibu wa sheria.

“Hadi sasa Jeshi la Polisi limefanikiwa kuwakamata Boniface Anyasile Mwabukusi na Mpaluka Said Nyagali maarufu kama Mdude na mahojiano nao yanaendelea”

“Jeshi la Polisi lilifanikiwa kuwakamata wawili hao maeneo ya Mikumi Mkoani Morogoro majira ya saa nane na nusu usiku Agosti 12, 2023”

Itakumbukwa jana Kamanda wa Polisi Tanzania, IGP Camilius Wambura aliwataka wanaoandaa maandamano Nchi nzima ili kuiangusha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya awamu ya sita kabla ya mwaka 2025 wakome na wasitishe uchochezi huo na kusisitiza kuwa huo ni uhaini na hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Screenshot_20230813_091004_Instagram.jpg
 
Jeshi la polisi Mkoani Mwanza linamshikilia Said Mfaume (32) ambaye ni Mtaalamu wa IT na Mkazi wa Arusha kwa kumchoma na kumjeruhi Mpenzi wake aitwaye Faudhia Juma (34) Mkazi wa Singida kwa kumchoma kisu katika maeneo mbalimbali ya mwili wake kisha na yeye kujaribu kujiua kwa kujichoma kisu tumboni hadi utumbo ukaning’inia akiamini kuwa Mpenzi wake amefariki kumbe bado yupo hai.

Kamanda wa Polisi Mwanza, Wilbroad Mutafungwa amesema tukio hilo lilitokea Aug 6, 2023 saa mbili asubuhi katika nyumba ya kulala wageni baada ya kuzuka ugomvi baina yao uliotokea baada ya Faudhia kukataa kuolewa na Mtuhumiwa huyo ambaye alikuwa ameshatoa mahari kwa Mama wa Faudhia huyo bila Msichana huyo kuridhia kuolewa “Baada ya Said ya kukutana na Faudhia na kujaribu kumweleza mipango ya ndoa akakataa na akatoweka Singida na kusema anakwenda kutafuta maisha”

“Said alipojua Mpenzi wake ametoroka akafanya ufuatiliaji kwa kutumia simu ya mkononi kwakuwa ni Mtaalamu wa IT na akajua Faudhia yupo Mwanza akafika Mwanza na kumuita Faudhia Gesti kisha kumchoma kisu na yeye akajichoma kisu tumboni hadi utumbo kuning’inia, pia Said tumemkuta akiwa na sumu kwenye begi”

“Kwa sasa Wapenzi hawa wawili wanaendelea na matibabu, Said anaendelea na matibabu akiwa chini ya uangalizi wa Polisi, uchunguzi ukikamilika atafikishwa Mahakamani”
Screenshot_20230813_091131_Instagram.jpg
 
Utawala wa kijeshi wa Burkina Faso ambao unaunga mkono kitendo cha Wanajeshi wa Niger kumpindua Rais wao, umesitisha matangazo ya mojawapo ya kituo kikubwa cha redio nchini humo baada ya kurusha mahojiano yanayochukuliwa kuwa "matusi" kwa Viongozi wa kijeshi wa Niger.

@DW_Kiswahili imeripoti kuwa Redio Omega iliamuriwa kuacha mara moja kurusha matangazo yake hadi pale patakapotolewa tangazo jingine, Waziri wa Habari wa Burkina Faso, Rimtalba Jean Emmanuel Ouedraogo, amesema uamuzi huo umechukuliwa kwa maslahi mapana ya Taifa.

Kituo hicho ambacho ni sehemu ya Shirika la Utangazaji la Omega linalomilikiwa na Mwandishi wa Habari na Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje wa Burkina Faso, Alpha Barry, kilisitisha matangazo yake muda mchache tu baada ya tamko hilo la Serikali.

Kosa la kituo hicho lilikuwa ni kurusha mahojiano yake na Ousmane Abdoul Moumouni, Msemaji wa kundi linaloendesha kampeni ya kumrejesha madarakani Rais Mohamed Bazoum madarakani nchini Niger, kauli yake imetafsiriwa kuwa matusi kwa utawala mpya wa Niger.
Screenshot_20230813_091422_Instagram.jpg
 
Jeshi la Polisi Mkoani Iringa limemkamata Jacob Mhanga (54) Mkazi wa kijiji cha Utiga Mkoani Njombe akiwa na meno saba ya Tembo katika nyumba ya kulala wageni.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Allan Bukumbi amesema Mtuhumiwa huyo alikutwa katika nyumba ya kulala wageni katika kijiji cha Mbalamaziwa Kara ya Kisanga Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa na atafikishwa Mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika

Vilevile Polisi kwa kushirikiana na Askari wa Uhifadhi na kupitia taarifa fiche kutoka kwa raia wema lilimkamata Mathias Malenga (37) Mkazi wa Kijiji cha Image Kata ya Image Wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa akiwa na silaha mbili moja shotgun ambayo haina namba na nyingine ni gobore ndani ya nyumba yake na Mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani upelelezi ukikamilika.
Screenshot_20230813_091612_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

Kila anachokifanya Tajiri MO kwenye page zake inawachanganya sana watu, MO anaweza kuja Insta na kulalamikia kitu na wote wakaamini Simba sio shwari lakini MO anatoa mzigo mfukoni analeta wachezaji ndani ya Simba, hapo ndipo anawachanganya zaidi.

Mpaka sasa kuna MO wawili, kuna MO wa Instagram na Twitter, huyo ni MO tofauti na wa taasisi, huyu wa mitandaoni ataandika anachotaka na atavuruga anavyotaka ila MO Taasisi ana watu ambao wanafanya maamuzi on behalf ambao hawana shida na MO wa Instagram na Twitter.

Huyu MO wa mitandao ya Kijamii ana msaada mkubwa sana kwa Simba, MO huyu ataileta attention kwake hata pale timu ikicheza vibaya ama kuna kitu hakipo sawa, kumjadili yeye unaipa nafasi timu kurecover na kuendelea! MO wa Insta anampa nafasi MO wa taasisi utulivu wa kufanya vitu.

MO wa Insta ananikumbusha Tajiri wa PAOK aliyetoa silaha uwanjani tena hadharani, stori haikuwa tena timu kupoteza bali tukio la Tajiri, ananikumbusha Perez alivyoona mambo hayaendi kabisa akajiuzulu 2006 akaitoa pressure kwenye timu akaondoka nayo.

Nguvu za kutomuelewa Tajiri zihamishiwe kwenye suala la kwanini mchakato haukamiliki wa mabadiliko, zihamie kwanini watu hawanunui merchandise za klabu na hawalipii card! MO anaeleweka hata pale ambapo Mashabiki hawataki kueleweka kwa kutimiza wajibu wao! Kuna ubaya anapiga na kulipa?

The game of spinning! Tajiri MO ananikumbusha Matajiri na dunia yao! Matajiri wengine hufanya wenyewe na wengine hutuma watu kufanya kwa niaba yao! Dunia ya kitaasisi inahitaji akili sana kuielewa.
Ni kweli kabisa hasa Mo wa linkedin anaandika madini tupu ,full kutoa elimu ya uwekezaji
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom