Makapuku Forum

WAKATI timu kubwa barani Ulaya zikisuasua kutoa hela za kunasa saini ya nyota wa kimataifa wa Nigeria
Victor Osimhen, inaelezwa Al Hilal imeweka mezani Pauni 120 milioni ili kuipata saini ya straika huyo wa Napoli dirisha hili.
.
Al Hilal imetuma ofa hiyo ikiwa ni siku kadhaa kupita baada ya kumshawishi nyota wa PSG, Kylian Mbappe ingawa aligoma kufanya nao mazungumzo. Pamoja na ofa hiyo ya Al Hilal kwenda Napoli, pia imepanga kumlipa Osimhen mshahara wa Pauni 1 milioni (Sh 3.1 bilioni) wiki.
.
Hata hivyo, licha ya dau la Al Hilal kuonekana kuwa ni kubwa, wataalamu wa mambo wanadai kuna uwezekano mkubwa likakataliwa kwani Napoli inadaiwa kuhitaji kiasi kisichopungua Pauni 170 milioni ili kumuuza.
 
Huh!!
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…