Makapuku Forum

Mwenyekiti wa tawi la Simba SC katika Mji Mdogo wa Mchombe, Kata ya Mngeta, Halmashauri ya Mlimba, mkoani Morogoro, Benson Mwakasanga (48) amefariki dunia baada ya kudaiwa kushambuliwa na kundi la watu wasiojulikana usiku wa kumkia leo Julai 25, 2023; akiwa katika mavuno ya mpunga, shambani kwake wilayani Kilombero mkoani humo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Alex Mkama, amethibitisha kutokea kwa tukio, ambapo amesema kuwa tukio hilo limeripotiwa kwa jeshi hilo, na kwamba maafisa wa wake wanakusanya taarifa ili baadaye wazitoe kwa umma.

Akizungumza na Mwananchi Digital leo Julai 25, 2023, Msemaji wa tawi hilo, Supertus Duma, amesema Mwakasanga amekutwa amefariki dunia asubuhi ya leo huku mwili wake ukiwa na majeraha maeneo ya kichwani, kifuani na mikononi hali inayoashiria kuwa kabla ya kifo chake kulikuwa na mapambano.

Duma amesema aliongea naye jana saa 4 usiku wa Julai 24 na kupewa mipango ya kuandaa safari ya Simba Day na saa 5 usiku huo pia aliongea na mtoto.
 
Habari kutoka kwa Kiongozi wa Upinzani nchini Kenya, Raila Odinga, zinasema licha ya juhudi za upatanishi za Rais Samia Suluhu Hassan alipozuru nchi hiyo, Serikali ya Kenya inadaiwa kuvuruga juhudi hizo kwa madai kuwa Rais wa Kenya William Ruto, alimfanya Rais Samia kusubiri kwa usiku mbili kabla ya kuweza kusuluhisha mzozo huo.

Raila ameviambia vyombo vya habari vya kimataifa kuwa Samia alikuwa nchini Kenya wiki mbili zilizopita.

"Kama tulivyoripoti hapo awali, wiki mbili zilizopita (wakati huo Rais Samia inasemekana alikuwa nchini Kenya), Rais Ruto alitangaza hadharani kuwa yuko tayari kufanya mazungumzo na mtu yeyote, akiwemo Kiongozi wa Azimio, ilimradi ajenda hiyo isihusishe kushikana mikono (handshake)," imesema taarifa hiyo.

 

X wangu huyo
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…