Mpiga Kinubi maarufu Mwanadada Siobhan Brady leo July 25, 2023 ameweka rekodi ya Dunia ya Guinness juu ya Mlima Kilimanjaro futi 19,000 kwa kupiga kinubi (kifaa kinachoheshimika nchini Ireland) kwa muda wa dakika 34 akiwa kileleni na kuvunja rekodi ya kupiga kinubi kwa muda wa dakika 18.
Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa @gersonmsigwa ametoa taarifa hiyo leo ambapo amesema awali Siobhan alipiga kinubi akiwa futi 16,000 katika Mlima Himalaya nchini India mwaka 2018.
Rekodi hii inaitwa “Guinness World Record for the Highest Harpist Concert” na imerekodiwa na kituo runinga cha Kimataifa kiitwacho National Geographic na sasa Kamati ya Dunia ya Guinness inasubiriwa kuthibitisha rekodi hiyo.
View attachment 2699310