Makapuku Forum

Makapuku Forum

ANDRE Onana huenda akawa mmoja wa makipa wanne ghali duniani
atakapotua Manchester United katika historia ya mchezo wa soka.
.
Waliomtangulia ni Kepa kwenda Chelsea — Pauni 80m, Alisson kwenda
Liverpool — Pauni 62.5m na Gigi Buffon kwenda Juventus — Pauni 52.5m.
Screenshot_20230719_121053_Instagram.jpg
 
MIKEL Arteta amesema kwamba Declan Rice ataiongezea Arsenal mzuka wa kubeba ubingwa msimu ujao. Kiungo huyo ghali kabisa kwenye historia ya Arsenal juzi Jumatatu alifanya mazoezi ya kwanza na wenzake.
.
Arteta alisema: “Tutakachopata kutoka kwa Declan ni uwezo wake wa kuongoza. Namwona kama tu atakayehamashisha kuweka mambo vizuri na kufanya timu icheze vizuri. Hiyo itaongeza ubora mkubwa. Kwa namna anavyozungumza, kuna kitu ataleta kwenye timu.”
.
Arteta, 41, aliongeza: “Presha ipo kwetu sasa. Baada ya tulichofanya msimu uliopita, watu watataka kuona nini kitafuata na tumefanya usajili muhimu pia. Hakuna kilichotofauti na wengine, lakini ukiwa Arsenal unapaswa kukabiliana na presha.”
.
Usajili wa Rice na ule wa Jurrien Timber na Kai Havertz umeifanya Arsenal kutumia Pauni 200 milioni kwenye dirisha ili la uhamisho wa majira ya kiangazo huko Ulaya.
Screenshot_20230719_121333_Instagram.jpg
 
KOCHA Mkuu wa Chelsea, Mauricio Pochettino anapiga hesabu kunasa huduma ya beki Harry Maguire kabla dirisha hili la kiangazi halijafungwa. Staa huyo wa kimataifa wa England 30, anaweza kuachana na Manchester United dirisha hili baada ya kuvuliwa unahodha na kocha Erik ten Hag ikiwa na maana hayupo kwenye mipango ya Ten Hag.
.
Ishu ya Pochettino kuvutiwa na Maguire ilifichuliwa na Danny Rose, mmoja wa wachezaji wake wa zamani, ambaye alisema: “Nakumbuka tulicheza na Hull uwanjani White Hart Lane (Desemba 2016) na tulishinda 3-0. Mauricio alikuwa kocha wetu na Harry alikuwa kila sehemu. Spurs nadhani walihitaji saini yake. Poch alionekana wazi kuhitaji saini yake. Nilipokuwa nafanya naye mazoezi kwenye kikosi cha England, ilikuwa ngumu sana kupata mpira kutoka kwake. Ni mzuri kiasi hicho.”
Screenshot_20230719_121451_Instagram.jpg
 
SRAIKA Kylian Mbappe jana Jumanne aliripotiwa kuwa na kikao maalumu na rais wa Paris Saint-Ger-main, Nasser Al-Khelaifi kujadili hatima yake.
.
Rais wa PSG Al-Khelaifi alikiri kushtushwa na uamuzi wa mshambuliaji huyo kwamba hawezi kubaki kwenye timu hiyo hadi 2025. Kutokana na hilo, PSG ilimpa Mbappe wiki mbili za kuamua kama anabaki Parc des Princes kwa maana ya kusaini mkataba mpya la basi auzwe kwenye dirisha hili hili la uhamisho wa majira ya kiangazi. Hivyo, Mbappe na Al-Khelaifi walitarajia kukutana jana ana kwa ana ana kwa ajili ya mazungumzo na kuwekana wazi juu ya hatima ya kila upande klabuni hapo.
.
Kuna ripoti zilidai kwamba Mbappe atakwenda kuambiwa hadi kufikia Julai 31 atatakiwa aweke wazi msimamo wake kama atabaki PSG hadi 2025 au milango ifunguliwe ya kupokea ofa ya kupiga bei mwaka huu. Real Madrid bado wanapewa nafasi kubwa ya kunasa saini yake, lakini miamba hiyo ya Bernabeu inaelezwa kwamba haina pesa za kugharimia uhamisho wake baada ya kumtumia mkwanja mrefu kwenye dirisha hili kunasa huduma ya kiungo Jude Bellingham kutoka Borussia Dortmund.
.
Kutokana na hilo, timu za Ligi Kuu England zinaweza kuingia kwenye mchakato wa kunasa saini yake ikiwamo Manchester United, Arsenal na Liverpool abazo zote zimeripotiwa kufuatilia kwa karibu mchakato huo.
Screenshot_20230719_121539_Instagram.jpg
 
Hii hapa safari ya SKUDU hadi kutua Jangwani
.
2016 — Orlando Pirates
2017 — Chippa United (mkopo)
2018 — Orlando Pirates (Thank You)
2019 — Free Agent
2020 — U. Pretoria
2021 — Marumo G
2023 — YANGA

Screenshot_20230719_121636_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom