Makapuku Forum

Makapuku Forum

AZAM FC itashuka uwanjani leo kucheza mchezo wake wa pili wa kirafiki dhidi ya miamba ya soka la Afrika, Esperance Tunis utakaopigwa saa 1:30 usiku.
.
Kocha mkuu wa timu hiyo, Youssouph Dabo alisema mchezo huo utatoa mwanga mzuri wa kikosi hicho hasa katika kipindi hiki ambacho anatengeneza muunganiko wa kiuchezaji kwa mastaa wake wapya.
.
Esperance inaitumia Azam kujiwinda na mchezo wa Julai 27 itakapocheza na Al Ittihad ya Saudi Arabia yenye mastaa wakubwa kama Karim Benzema na N’Golo Kante katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa ya mataifa ya Kiarabu.
Screenshot_20230719_115707_Instagram.jpg
 
“Uwezo wake wa kupambana uwanjani ni mkubwa sana bila kusahau mbinu na uzoefu alionao ndio uliowavutia zaidi Yanga, hivyo umri sio kikwazo. Yanga hawatajutia kuwa naye, sisemi kwa sababu ni meneja wake ila kizuri kinajiuza nina uhakika atafanya makubwa.” Meneja wa Sudi Abdallah.
Screenshot_20230719_120443_Instagram.jpg
 
CHANZO changu makini kutoka ndani ya Simba kimenidokeza sababu zimewashawishi benchi la Ufundi la Simba kufanya usajili wa kushtukiza wa nyota wa zamani wa Azam na Taifa Stars, Shaaban Chilunda.
.
Jambo la kwanza lilioishawishi Simba kumsajili hofu ya majeraha hasa Bocco na Moses Phiri ambayo msimu uliopita yalichangia wakose idadi kubwa ya mechi na hivyo wanaamini kama huyu atakuwa fiti anaweza kuziba. Jambo la pili ni uzoefu alionao wa mashindano ya ndani na mazingira ya soka la Tanzania ambao ameupata kwa kucheza muda mrefu Azam.
Screenshot_20230719_120858_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom