Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mtumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, Mkoa wa Morogoro, idara ya maendeleo ya jamii, Mereciana Calvin (42), ameuawa nyumbani kwake eneo la Mamboya huku shingoni akiwa na majeraha ya kukatwa na kitu chenye ncha kali.

Akitoa taarifa ya mauaji hayo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Hassan Omary alisema uchunguzi unaonyesha mtumishi huyo aliuawa Julai 17, mwaka huu saa 3:30 usiku na mwili ulikutwa sebuleni kwake jana asubuhi.

Alisema pamoja na mtumishi huyo kuuawa, pia baadhi vitu viliibwa ndani mwake, ikiwemo televisheni, godoro na simu ya mkononi aliyokuwa akiitumia.

Kutokana na tukio hilo, alisema Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi wa usalama Wilaya na Mkoa wanaendelea na uchunguzi, ikiwa ni pamoja na kuwasaka waliohusika kutekeleza mauaji hayo.

Naye Mkuu wa Wilaya hiyo, Shaka Hamdu Shaka alisema tukio hilo ni la kusikitisha na lazima vyombo vya ulinzi na usalama vifanye kazi usiku na mchana ili kubaini chanzo cha mauaji hayo na wote waliohusika ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

"Ni tukio baya ambalo haliwezi kufumbiwa macho, nina imani na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama, najua kupitia wataalamu wao watachunguza vizuri na watatoa majibu kuhusu tukio hili ambalo linaonekana wazi kuwa ni la kupanga," alisema Shaka.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Kisena Mabuba alisema baada ya tukio hilo mwili wa Mereciana ambaye pia alikuwa mratibu wa Ukimwi wa Halmashauri umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro na taratibu za mazishi zinafanywa.

Screenshot_20230719_114804_Instagram.jpg
 
Jeshi la Polisi nchini, limetoa wito wa kufika ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) kwa Makamu Mwenyekiti Chadema Tanzania Bara, Tundu Lissu, kwaajili ya kufanya mahojiano ikiwa ni hatua ya kukamilisha upelelezi kuhusiana na kile kinachodaiwa matamshi yasiyo na staha ya mwanasiasa huyo, mitandaoni.

Sehemu ya wito huo inasomeka: “Ofisi hii inafanya uchunguzi kuhusiana na maneno uliyotumia yasiyo na staha kumjibu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kusambaa kwenye mitandao ya kijamii kuanzia Julai 15, 2023.”

Aidha, wito huo ambao umesainiwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi, Joseph Mfungamara, umeeleza kuwa: “Ili tuweze kukamilisha uchunguzi wetu, ofisi hii inakutaka ufike ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai, Makao Makuu Ndogo Dar es Salaam siku ya Alhamisi Juali 20, 2023 saa 3:00 asubuhi bila kukosa kwaajili ya mahojiano.”

Hata hivyo, Lissu ambaye hajaonyesha ama kukataa au kukubali wito huo wa Polisi, ametumia ukurasa wake wa Twitter, kuhoji aina ya staha inayotakiwa kutumika pale mtu anapohoji juu ya sakata la mkataba wa bandari, huku akiwa ameambatisha barua ya wito huo.

(Imeandikwa na Mwandishi wetu).

Screenshot_20230719_114912_Instagram.jpg
 
Mtumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, Mkoa wa Morogoro, idara ya maendeleo ya jamii, Mereciana Calvin (42), ameuawa nyumbani kwake eneo la Mamboya huku shingoni akiwa na majeraha ya kukatwa na kitu chenye ncha kali.

Akitoa taarifa ya mauaji hayo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Hassan Omary alisema uchunguzi unaonyesha mtumishi huyo aliuawa Julai 17, mwaka huu saa 3:30 usiku na mwili ulikutwa sebuleni kwake jana asubuhi.

Alisema pamoja na mtumishi huyo kuuawa, pia baadhi vitu viliibwa ndani mwake, ikiwemo televisheni, godoro na simu ya mkononi aliyokuwa akiitumia.

Kutokana na tukio hilo, alisema Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi wa usalama Wilaya na Mkoa wanaendelea na uchunguzi, ikiwa ni pamoja na kuwasaka waliohusika kutekeleza mauaji hayo.

Naye Mkuu wa Wilaya hiyo, Shaka Hamdu Shaka alisema tukio hilo ni la kusikitisha na lazima vyombo vya ulinzi na usalama vifanye kazi usiku na mchana ili kubaini chanzo cha mauaji hayo na wote waliohusika ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

"Ni tukio baya ambalo haliwezi kufumbiwa macho, nina imani na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama, najua kupitia wataalamu wao watachunguza vizuri na watatoa majibu kuhusu tukio hili ambalo linaonekana wazi kuwa ni la kupanga," alisema Shaka.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Kisena Mabuba alisema baada ya tukio hilo mwili wa Mereciana ambaye pia alikuwa mratibu wa Ukimwi wa Halmashauri umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro na taratibu za mazishi zinafanywa.

View attachment 2692906
Huu msiba unenisikitisha sana, mdada alikua poa sana
 
Bilionea Elon Musk ametangaza katika ukurasa wake wa Twitter kuwa kampuni yake ya Starlink, imezindua huduma ya internet yenye kasi, inayotumia satelaiti nchini Kenya, na kwamba kwa uzinduzi huo, mteja ataweza kupata huduma hiyo bila kujali mipaka ya nchi hiyo.

Kabla ya uzinduzi huo nchini Kenya, wakati fulani Tanzania ilipokea maombi ya kampuni hiyo kuja kuwekeza nchini, huku wadau wakisema itachochea uchumi wa kidijitali na itakuwa nafuu na yenye kasi.

Taarifa hizo zinasema, huenda hadi kufika Machi 2023 teknolojia hiyo inayomilikiwa na Kampuni ya SpaceX itakuwa imeingia nchini.

Kwenye tovuti yao rasmi, Starlink ilitangaza mpango wao wa kuleta huduma hizo nchini kati ya Januari na Machi 2023, kama wangeruhusiwa na Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA).

Hata hivyo, akizungumza na katika mahojiano maalum na Mwananchi Digital Februari mwaka huu, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye; alisema Tanzania ipo tayari kuipokea internet ya Elon Musk 'Starlink', na kwamba wanasubiri wawasilishe nyaraka tu.

Screenshot_20230719_115006_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom