Makapuku Forum

Makapuku Forum

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amesema idadi ya kuku wa kisasa waliopo nchini ni wengi ikilinganishwa na kuku wakienyeji.

Kuku wa kisasa wapo milioni 52.8 huku wakienyeji wakiwa milioni 45.1, pia Ulega amesema idadi ya kuku nchini inazidi kuongezeka ambapo mwaka wa fedha 2021/2022 jumla ya kuku nchini ilikuwa milioni 92.8 imeongezeka hadi milioni 97.9 mwaka wa fedha 2022/2023.

Ulega ameyasema hayo leo bungeni Jumanne Mei 2, 2023 wakati akisoma mapendekezo ya bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa Fedha 2023/2024.

Screenshot_20230502_150819.jpg
 
Rais Samia Suluhu Hassan ameipongeza timu ya Yanga kutinga nusu fainali Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kuiondosha Rivers United ya Nigeria kwa mabao 2-0.

“Pongezi kwa Klabu ya Yanga kwa kutinga Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho (CAF Confederation Cup), na kila la kheri katika maandalizi mliyoanza sasa kwa mchezo ujao. Mmeandika historia jalili. Mmetuheshimisha sana. Hamasa yangu inaendelea, na sasa imeongezeka. Kaifanyeni kazi.” Ameandika Rais Samia katika mitandao yake ya kijamii.

Yanga inatarajiwa kucheza nusu fainali dhidi ya Marumo Gallants ya Afrika Kusini iliyofika hatua hiyo baada ya kuiondosha Pyramid ya Misri kwa mabao 2-1.

Screenshot_20230502_151006.jpg
 
Utata umeibuka katika familia ya Wilson Bulabo (35) na Hellena Robert baada ya mtoto wao, Mabirika Wilson (8) aliyefariki na kuzikwa nyumbani kwao katika kijiji cha Salong'we kata ya Mwamabanza wilayani Magu mkoani Mwanza kupatikana akiwa hai katika kijiji cha Mwangika wilayani Kwimba mkoani hapa.

Mtoto huyo anayedaiwa kufariki kwa ugonjwa wa Malaria Aprili 16, mwaka huu na kuzikwa Aprili 17,2023 alikutwa na wachugaji wa ng'ombe akizurura kwenye majaruba yaliyoko kijiji cha Mwangika.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Wilbroad Mutafungwa, wachungaji hao baada ya kubaini kuwa mtoto huyo hana uangalizi walimuhoji akajitambulisha kuwa anaitwa Mabirika Wilson na nyumbani kwao ni kijiji cha Salong'we kilichopo Wilaya ya Magu.

Alisema baada ya familia kudai hivyo, Polisi iliomba kibali cha kufukua kaburi lililopo katika familia hiyo kutoka Mahakama ya wilaya ya Magu na kufanya utambuzi ambapo baba, Wilson Bulabo (35) na mama wa mtoto huyo, Helena Robert (33) wamedai mwili uliomo siyo wa mtoto wao.
Screenshot_20230502_151110.jpg
 
Waziri wa Kazi, Ajira na Uhusiano wa Viwanda Nchini Uganda, Charles Okello Engola ameuawa asubuhi hii kwa kupigwa risasi na Mlinzi wake (Bodyguard), Spika wa Bunge la Uganda Anitha Among amethibitisha Bungeni leo.

Tukio hilo limetokea asubuhi hii ambapo imeripotiwa kuwa Waziri Okello alikuwa anatoka nyumbani kwenda kazini ambapo ghafla Mlinzi wake alimpiga risasi kisha akaanza kupiga risasi juu huku akikimbiakimbia Mtaani, Majirani wamesema Mlinzi huyo alisikika akisema hajalipwa mshahara kwa muda mrefu licha ya kufanya kazi na Waziri huyo.

Inaripotiwa kuwa Mlinzi huyo baadaye aliingia Saluni moja iliyopo Jirani na nyumba ya Waziri kisha akawataka waliokuwa ndani kutoka nje na akajifungia na kujipiga risasi na kufariki pia.
View attachment 2607239
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣😅
 
KISINDA: NITAWAPA UBINGWA YANGA
.
Winga machachali wa Yanga, Tuisila Kisinda raia wa Congo, amewaambia mashabiki wa timu hiyo kuwa wasipaniki kwa kufikia hatua ya Nusu Fainali kwani ana uzoefu wa kuchukua kombe hilo msimu uliopita alipokuwa RS Berkane na amasisitiza watafanya kazi ya maana kubeba taji hilo.
.
“Sidhani kama Malumo ina timu ya kutisha kama inavyozungumzwa, hata ukiangalia mechi walizocheza kwenye ligi hawachezi vizuri kabisa.
.
“Lakini pia kwa sasa Yanga wana mimi nina uzoefu na mashindano haya na sehemu kubwa ya wachezaji wenzangu ni Wazoefu, lazima tuwafunge tu kwa maana tunataka ubingwa.” alisema Kisinda.
Screenshot_20230502_152131.jpg
 
WAARABU WAMSAKA ROBERTINHO
.
Simba imeacha gumzo kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, ni ubora wao uwanjani na sasa kama kuna mtu anayesakwa ni kocha wao Robert Olivieira ‘Robertinho’.
.
Mezani kwa Robertinho ofa mbili kubwa ambazo inategemea na akili kubwa ya mabosi wa Simba na uamuzi wa kocha huyo raia wa Brazil. Tuanze na Misri klabu ya Al Ittihad, inayoshiriki ligi kuu nchini humo imempigia simu kocha huyo ikitaka huduma yake baada ya kuona hesabu zao za kuingia ndani ya klabu tatu za juu kuwa na mashaka.
.
Al Ittihad sasa inafundishwa na kocha wa zamani wa Simba, Zolan Maki ambaye kabla ya kutua huko alitokea hapa nchini wakiona bado hawajakubali mwendo wa kocha wao huyo raia wa Serbia. Katika mechi zao tano za mwisho Al Ittihad imeshinda mechi moja na kupoteza tatu huku wakitoa sare moja hatua ambayo imewatisha mabosi wa klabu hiyo wakianza mchakato wa siri.
.
Akizungumzia jana kwa kifupi Robertinho licha ya kukiri ofa kuwa nyingi kwake alisema kwa sasa anataka kuitumika Simba kuhakikisha anatengeneza timu tishio Afrika.

Screenshot_20230502_152225.jpg
 
BARCA RUKSA UEFA
.
Barcelona imepata ruhusa ya kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao. Kulikuwa na ripoti kwamba Shirikisho la Soka la Ulaya, UEFA likawazuia Barcelona kushirki kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao kutokana na kufanyiwa uchunguzi kuhusiana na sakata la Negreira.
.
Lakini, ripoti mpya zinafichua kwamba Barca sasa imepewa ruhusa ya kucheza kwenye michuano hiyo ya msimu ujao. Barca ilishtakiwa kwa madai ya kutoa rushwa kwa aliyekuwa makamu wa rais wa kamati ya waamuzi wa Hispania.
Screenshot_20230502_152344.jpg
 
LAMPARD HAJUTI
.
Kocha wa muda wa Chelsea, Frank Lampard amesema wala hajutii uamuzi wake wa kurudi kuinoa timu hiyo yenye maskani yake Stamford Bridge. Kocha Lampard ameshuhudia vichapo vitano katika mechi tano alizoiongoza Chelsea tangu aliporudi kufanya kazi kwenye kikosi hicho.
.
Usiku wa leo Jumanne timu yake itakuwa na shughuli pevu itakapokwenda kukipiga na Arsenal katika mchakamchaka wa Ligi Kuu England.

Screenshot_20230502_152435.jpg
 
ANCELOTTI UHAKIKA BRAZIL
.
Rais wa Shirikisho la Soka la Brazil Ednaldo Rodrigues ameripotiwa kuwa na uhakika mkubwa wa kumchukua kocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti kwenda kuinoa timu ya taifa ya nchi hiyo.
.
Ancelotti ni chaguo la kwanza la makocha wanaopigiwa hesabu za kwenda kukinoa kikosi cha Selecao baada ya Tite kuachia ngazi zilipomalizika fainali za Kombe la Dunia 2022 huko Qatar.
Screenshot_20230502_152534.jpg
 
RASHFORD MSAADA!!
.
Staa wa Manchester United, Marcus Rashford ameripotiwa kumpangisha kwa gharama za chini beki Wes Brown baada ya kuripotiwa kufirisika. Brown, 43, aliyewahi kuichezea Man United ametangazwa mufilisi baada ya kuwa na deni kubwa la kodi na kampuni za magari.
.
Ukiweka kando msaada wa makazi ambao Rashford ameutoa, wachezaji wengine wa zamani wa Man United, ambao wamekuwa wakimpa sapoti Brown ni Wayne Rooney na Michael Carrick.
Screenshot_20230502_152638.jpg
 
ARTETA ATANGAZA VITA YA UBINGWA
.
Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta amesema tena kwa msisitizo hakuna hata mmoja kwenye kambi yake ambaye amekata tamaa kwenye mchakamchaka wao wa kufukuzia ubingwa wa Ligi Kuu England msimu huu.
.
“Kwa sasa ubingwa haupo kwenye mikono yetu. Kilichopo kwenye mikono yetu ni kujaribu kushinda kila mechi zilizobaki na mengine tutaiachia Man City. Sina kazi ya kuamsha ari ya wachezaji, wenyewe watawasha moto tu kwenye mechi hiyo. Ni ngumu kuitabiri Chelsea, lakini sisi tumejiandaa kushinda hiyo mechi.”
.
Arsenal ushindi wowote kwenye mechi hiyo dhidi ya Chelsea utawarudisha kileleni kwenye msimamo wa ligi licha ya kwamba watakuwa wamecheza mechi mbili zaidi ya mahasimu wao kwenye mbio za ubingwa huo, Man City.

Screenshot_20230502_152733.jpg
 
KOCHA ROBERTINHO:
.
“Tunarudisha kila nguvu yetu sasa kwenye mechi za hapa nyumbani, nimewaambia wachezaji wanatakiwa kuinua vichwa vyao hili limepita sasa tutawafariji mashabiki wetu kama tutashinda mechi zetu zilizosalia na tumefurahishwa na mapokezi.”
Screenshot_20230502_152225.jpg
 
Shirikisho la Soka nchini TFF limeusogeza mbele mchezo wa ASFC kati ya Simba SC na Azam FC uliokuwa kuchezwa Nangwanda Sijaona Mtwara Jumamosi Mei 6 hadi Jumapili Mei 7.

Aidha mchezo wa Singida BS dhidi ya Yanga nao umesogezwa mbele mpaka hapo utakapo pangiwa tarehe mpya .

Screenshot_20230502_152927.jpg
 
Aliyekuwa Bondia wa ngumi za kulipwa nchini Ibrahim Najum amezikwa jana katika makaburi ya Kikusya, Kyela mkoani Mbeya

Najum alianguka ulingoni jumapili iliyopita baada tu ya kumalizika kwa pambano lake la raundi nne dhidi ya Bondia wa Dodoma Laurent Segu, na kuwahishwa Hosptali ambapo inaarifiwa alifanyiwa upasuaji mdogo wa kichwa hadi asubuhi hali yake ilizidi kuimarika kabla ya kufikwa na umauti kesho yake mchana

Screenshot_20230502_153025.jpg
 
Legend @amrikiembatz kwenye HiliGame ya @cloudsfmtz

"Sasa hivi Azam inaweza ikaingia katika mechi hakuna yoyote ( Wachezaji) anayejua kilichokuwa kikiendelea katika timu , wachezaji bado wageni wengine ni wadogo hawana ile tamaduni ya timu "

" Ninachokiona mimi Azam FC wana maadui mule mule ndani ambao wanazisaidia timu za K/koo ( Simba na Yanga) kufanya vizuri "

" Mambo mengi ya Azam yanavuja mapema, wanapaswa kukaguana kuona ni nani anatutumikia sisi lakini yupo kuhakikisha furaha yake ya moyoni haipotei "

Unakubaliana na Amri Kiemba ?

Screenshot_20230502_153120.jpg
 
ANCELOTTI UHAKIKA BRAZIL
.
Rais wa Shirikisho la Soka la Brazil Ednaldo Rodrigues ameripotiwa kuwa na uhakika mkubwa wa kumchukua kocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti kwenda kuinoa timu ya taifa ya nchi hiyo.
.
Ancelotti ni chaguo la kwanza la makocha wanaopigiwa hesabu za kwenda kukinoa kikosi cha Selecao baada ya Tite kuachia ngazi zilipomalizika fainali za Kombe la Dunia 2022 huko Qatar.
View attachment 2607286
Sidhani kama litawezekana hili
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom