Makapuku Forum

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema hadi kufikia leo tarehe 25 Machi, 2023 hakuna Wagonjwa wapya wa Marburg walioripotiwa licha ya kupokea tetesi sehemu mbalimbali Mkoani Kagera.

Ummy akiwa Mkoani Geita amesema ugonjwa huo unaendelea kudhibitiwa ambapo ameambatana na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani Dkt. Zabron Yoti na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la UNICEF, Shalini Bahuguna

“Tangu kuanza kwa ugonjwa huu hadi leo tumeendelea kuwa na jumla ya Wgonjwa walewale nane waliothibitika ambapo watano kati yao walifariki na Watatu wanaendelea na matibabu katika vituo vya kutolea huduma vilivyoainishwa.”

Aidha, Ummy amesema Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera na Wadau mbalimbali inaendelea kudhibiti maambukizi ya ugonjwa huu kwa kutekeleza mikakati mbalimbali.

“Miongoni mwa hatua ni kuwaweka sehemu maalumu Watu wote waliohudumia Wagonjwa ambao ni Wanafamilia waliouguza Wagonwja na Watumshi wa Afya waliohudumia Wagonjwa, kwa siku 21 ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa huu kama watabainika na maambukizi.”

Katika kuendelea kudhibiti ugonjwa huo Serikali kupitia Wizara ya Afya imeongeza Wataalamu 6 wa afya ikiwemo Daktari Bingwa Mbobezi wa Magonjwa ya Figo, Daktari Bingwa wa magonjwa ya ndani na Wauguzi waliopata mafunzo maalumu kutoka maeneo mengine ili kusaidiana na Wataalamu wa Afya Mkoani Kagera.
 
Wananchi waliowekwa karantini baada ya kuchangamana na wagonjwa wa Marburg wameongezeka kutoka 193 hadi 205 huku Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akisema hakuna wagonjwa walioongezeka.

Waziri Ummy akiongea na waandishi wa habari katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa leo Machi 25, 2023 amesema kuwa, wataalamu wa afya wanaendelea kufuatilia watu wote waliochangamana na wagonjwa wa Marburg na kuwaweka karantini kwa kipindi cha siku 21 ili kubaini kama wana dalili za ugonjwa huo ambao mtu anaambukiza baada ya kuonyesha dalili.

Amesema kutokana na kiini cha mgonjwa kutokea Kisiwa cha Gozba wametuma timu ya wataalamu kutoka Wilaya ya Muleba ambao watafanya ufuatiliaji kubaini wale wote waliochangamana na mgonjwa huyo ambaye baada ya kutoka kisiwani alikwenda kwenye familia yake Maruku.

Amesema wametuma madatari bingwa wabobezi sita hapa Kagera miongoni mwao wamo daktari bingwa wa magonjwa ya ndani na daktari bingwa wa moyo.
 
Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana, amewataka Waislamu kuzingatia mafundisho ya Mtume Muhammad (SAW) hususan kuhusu kumcha Mungu na tabia njema.

Kinana ameyasema hayo leo Machi 25, 2023 wakati wa hafla ya mashindano ya Quran Tukufu yaliyoandaliwa na Taasisi ya Faraja Foundation ya jijini Dar es Salaam.

""Tunaagizwa na Kuraani, pia tunaagizwa na Mtume wetu (Muhammad - S A.W) kuwa kila Muislamu anapaswa kuzingatia mambo mawili jambo la kwanza 'takwa' (ucha Mungu) na la pili 'akhlaki' tabia njema).

"Kwa hiyo ukizingatia 'takwa' ukazingatia na maadili mema hakuna namna utapotoka, itakuwa hakuna haja hata ya sisi kuwa na wasiwasi kwamba maadili mabaya yanaweza yakatupitia," amesema Kinana.

Aidha, aliwahamasisha Waislamu nchini kuwapeleka watoto wao madrasa wakajifunze imani na maadili ya dini yao na kumjua Mwenyezi Mungu.
 
Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro ameeleza Sh223.9 bilioni zilivyotumika katika kuboresha na kujenga miradi ya maendeleo ndani ya miaka miwili ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari imeeleza Mtatiro ameeleza hayo leo Jumamosi Machi 25, 2023 katika kongamano la wilaya hiyo la kuadhimisha miaka miwili ya uongozi wa Rais Samia aliyeingia madarakani Machi 19 mwaka 2021.

Katika maelezo yake, Mtatiro amesema kati ya Sh223.9 bilioni zilizopelekwa wilayani humo Sh150 bilioni zimetumika katika mradi mkubwa wa umeme wa kilovoti 220 wenye urefu wa kilomita 210 kutoka Songeni hadi Tunduru.

 
Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ameshiriki katika mjadala wa Uongozi na Usimamizi wa Masuala ya Maji katika mkutano wa maji wa Umoja wa Mataifa unaoendelea New York, Marekani.

Mjadala huo ambao uliandaliwa na nchi mbalimbali ikiwemo Tanzania na Afrika Kusini pamoja na mashirika mbalimbali ikiwemo GWP, UNICEF na UNDP, ulihudhuriwa na mgeni rasmi ambaye ni Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa GWPSA na Mwenyekiti mwenza wa jopo la viongozi maarufu kuhusu uwekezaji katika sekta ya maji.

Katika mchango wake, Waziri Aweso alibainisha uongozi imara wa Rais Samia Suluhu Hassan, katika agenda ya kwa kuongeza msukomo na utashi wa kisiasa, kuongeza bajeti ya maji pamoja na kuimarisha taasisi zinazohusiana na usimamizi wa huduma za maji na utekelezaji wa miradi ya maji.

Katika kutekeleza hilo, Tanzania inatekeleza Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji awamu ya tatu yenye thamani ya Dola 6.47 bilioni za Marekani na mwezi Mei 2023 itazindua Programu ya Uwekezaji katika Sekta ya Maji (Tanzania Water Investment Programme 2023-2030).

Kupitia mjadala huo, Tanzania imeongeza wadau mbalimbali wa kushirikiana nao katika hiyo.
 
Raia wa China Zheng Yuan Feng amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza kwa kosa la kumjeruri mmoja wa wafanyakazi wa mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa SGR, Lucy Paulo mwenye fani ya upishi.

Feng ambaye ni mfanyakazi wa Kampuni ya China Railway Construction Corporation Limited (CRCC) ambayo ni moja ya kampuni zinazojenga reli ya kisasa SGR kutoka Mwanza hadi Isaka yenye urefu wa kilomita 341.

Lucy alishambuliwa Machi 18 na Zheng Yuan Feng majira ya saa tatu kasoro asubuhi akiwa katika majukumu yake eneo la jikoni na raia huyo kwa kumtolea lugha chafu na kisha kumpiga na kusababishia majeraha na kupelekwa Hospitali ya Bugando.

Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi, Machi 25, 2023 na Mkuu wa kitengo cha Uhusiano, Shirika la Reli Tanzania (TRC), Jamila Mbarouk imeleeza kuwa Lucy alipatiwa matibabu na kuruhusiwa Jumanne Machi 21 majira ya asubuhi na sasa yupo kambini Fela chini ya uangalizi wa daktari wa kambi.

 
Baadhi ya wakazi wa vijiji vya Kataryo na Wanyere Wilaya ya Musoma wanadaiwa kuiba vyuma na nati za daraja la Mto Suguti vyenye thamani ya zaidi ya Sh21 milioni hivyo kuhatarisha usalama wa daraja na watumiaji.

Daraja hilo la muda lenye thamani ya zaidi ya Sh2 bilioni liliwekwa katika eneo hilo Januari 2020 baada ya kuwepo changamoto ya kuvuka mto huo iliyosababisha athari mbalimbali ikiwemo vifo hasa vya wanafunzi waliokuwa wakivuka mto huo wakati wa kwenda shule na kurudi nyumbani kipindi cha masika.

Akizungumza na Mwananchi Digital, Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini ( Tarura) Wilaya ya Musoma, Joseph Mkwizu amesema wizi huo umeibuka siku za hivi karibuni nakubaini vifaa hivyo vinatumika kwenye mitambo ya wachimbaji wadogo wa madini na kwaajili ya vifaa vya jembe la kukokota na ng'ombe (plau).
 
Polisi mkoani Mtwara wanamtafuta mwanamke mmoja ajulikanaye kwa jina la Rufina Joseph (45), Mkazi wa Mahurunga, Wilaya ya Mtwara ili atumikie adhabu yake ya miaka 30 jela kwa kosa la kusafirisha dawa za kulevya.

Mshtakiwa huyo alihukumiwa kifungo hicho siku ya Jumatano Machi 22, 2023 katika Mahakama ya Wilaya ya Mtwara na Hakimu Lucas Jang'andu baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa mbele yake.

Awali, ilielezwa mahakamani hapo kuwa Mshtakiwa huyo alikamatwa Februari 10, 2022 nyumbani kwake maeneo ya Mahurunga akiwa na bangi gramu 240 ikiwa kwenye ndoo ya lita 10 chumbani kwake.

 
NAGELSMANN ASAKWA CHELSEA
.
Chelsea imeripotiwa ndiyo inayopewa nafasi kubwa ya kumchukua kocha Mjerumani Julian Nagelsmann baada ya kufutwa kazi Bayern Munich. Nagelsmann, 35, alitemwa Ijumaa iliyopita baada ya timu kuwa na mwendo hafifu na tayari imeshamtangaza Thomas Tuchel kuwa kocha wao mpya. Tuchel naye alifukuzwa kazi Chelsea.

 
OFFICIAL: Argentina wametangaza rasmi kufanya mabadiliko ya jina la camp yao ya timu ya taifa Casa de Ezeiza ambayo sasa itajulikana kama Lionel Andres Messi. Sababu kubwa ya kubadilisha jina hilo ni kutoa heshima kwa Mwanasoka Bora wa Dunia.
 
Sports Arena Tz

AZAM INATUPA UGUMU KUITETEA
.
Katika timu ngumu kuzitetea hapa Tanzania, nadhani Azam FC inaongoza. Kila inapoanza msimu inakupa matumaini kama itashindania vilivyo ubingwa wa ligi na mashindano mengine ambayo hushiriki.
.
Utaona inafanya usajili wa wachezaji ambao wanaonekana mahiri kwenye timu zao ambao huaminisha wengi kuwa watawasha moto vilivyo kwenye msimu husika.
.
Watafanya maandalizi kabambe ya kabla ya msimu (pre-season) nje na ndani ya nchi na yanaweza kukuaminisha kuwa Simba na Yanga zitakutana na ushindani mkali katika mbio za ubingwa.
.
Hata hivyo msimu ukishaanza Azam inageuka timu ya kukamia mechi mojamoja na nyingi ucheza pasipo kuonyesha timu kubwa ambayo inakiu na hamu ya kutwaa mataji.
.
Mfano mzuri ni msimu huu zikiwa zimebakia mechi tano tu kumalizika Azam inawania nafasi ya tatu dhidi ya Singida inayoshiriki kwa mara ya kwanza Ligi Kuu msimu huu. Sasa Unapata wapi nguvu za Kuitetea Azam pale watu wanapoikosoa
 
ROBERTINHO KUHUSU DILUNGA
.
“Nafuatilia kwa karibu wachezaji wote wa Simba na wale wa timu nyingine na mwisho wa msimu nitatoa ripoti kwa uongozi itakayokuwa imejumuisha kila kitu.”
.
“Dilunga nimemuona lakini nahitaji muda zaidi kwani amekuja kipindi ambacho mara nyingi tunafanya mazoezi kwa ajili ya mechi husika, tutakuwa naye na mwisho itajulikana nini tutaamua,” alisema Robertinho.
 
Jobless pitia huu uzi
 
Ina kazi ya kuikamia simba na yanga tu😂
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…