Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,081
- 464,013
Jeshi la Polisi Mkoa wa Manyara limebaini mbinu mpya wanazotumia Wahalifu kusafirisha dawa za kulevya aina ya mirungi Wilayani Babati Mkoani Manyara.
RPC wa Manyara George Katabazi amesema January 16 mwaka huu Mwanaume mmoja alikamatwa akiwa na bunda 20 za mirungi sawa na Kilo 10 akiwa amezifunga kifuani na tumboni kwa huku Mtuhumiwa mwingine wa Kike alikamatwa akiwa na bunda 25 sawa na Kilo 12 za dawa hizo za kulevya (Mirungi) akiwa amezifunga mapajani.
Katika hatua nyingine Polisi Mkoa wa Manyara kwa kushirikiana na Mahakama ya Mwanzo Wilaya ya Simanjiro imemuhukumu Lalahe Karoli kifungo cha miaka 30 kwenda Jela kwa kosa la Kumbaka Mwanafunzi wa darasa la saba.
RPC Katabazi amewaomba Wananchi wa Mkoa wa Manyara kuendelea kufichua uhalifu na wahalifu pamoja na kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi .
RPC wa Manyara George Katabazi amesema January 16 mwaka huu Mwanaume mmoja alikamatwa akiwa na bunda 20 za mirungi sawa na Kilo 10 akiwa amezifunga kifuani na tumboni kwa huku Mtuhumiwa mwingine wa Kike alikamatwa akiwa na bunda 25 sawa na Kilo 12 za dawa hizo za kulevya (Mirungi) akiwa amezifunga mapajani.
Katika hatua nyingine Polisi Mkoa wa Manyara kwa kushirikiana na Mahakama ya Mwanzo Wilaya ya Simanjiro imemuhukumu Lalahe Karoli kifungo cha miaka 30 kwenda Jela kwa kosa la Kumbaka Mwanafunzi wa darasa la saba.
RPC Katabazi amewaomba Wananchi wa Mkoa wa Manyara kuendelea kufichua uhalifu na wahalifu pamoja na kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi .