Makapuku Forum

Makapuku Forum

LUIS JOSE MIQUISSONE ::
.
“Kama nitarudi Tanzania nitakuja kucheza Simba, siwezi kwenda klabu nyingine nisikilize mimi. Nimesikia mambo mengi kwenye mitandao lakini muda utaongea. Nikisema nizungumze kiundani zaidi yanaweza kutafsiriwa tofauti.”
Screenshot_20221229_045253_OGInsta%2B.jpg
 
BEKI KISIKI ATUA MAZOEZINI YANGA
.
Baada ya beki wa kati Abdallah Shaibu ‘Ninja’ kumaliza mkataba wake wa mkopo Dodoma Jiji, amerejea Yanga na leo anaanza rasmi mazoezi na wenzake kwenye Uwanja wa Avic Town.
.
Ninja alikuwa aungane na wenzake jana Jumanne, lakini ilishindikana ambapo timu hiyo ilifanya mazoezi ya gym na leo itafanya ya uwanjani ambapo ndipo ataungana nao rasmi kuanza kukiwasha, ikijiandaa na mechi dhidi ya Mtibwa Sugar itakayopigwa Manungu, Jumamosi.
Screenshot_20221229_045344_OGInsta%2B.jpg
 
MUDATHIR SIMBA SC
.
Simba inaendelea kushusha majembe usajili wa dirisha dogo, tayari wamemalizana na kiungo Mudathir Yahya anayemudu kucheza nafasi mbili, namba sita na nane uwanjani, akiwa Mchezaji huru baada ya kuachana na Azam FC kabla msimu haujaanza.
.
Chanzo cha kuaminika ndani ya klabu hiyo kimethibitisha kuwa staa huyo muda wowote atatangazwa ndani ya Simba ambayo ina mastaa sita eneo la kiungo mkabaji.
Screenshot_20221229_045832_OGInsta%2B.jpg
 
Ronaldo mbioni kufanyiwa vipimo vya afya Uarabuni
.
Matajiri wa Saudi Arabia, Al Nassr tayari wameshapanga hadi siku ya vipimo vya afya kwa ajili ya kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Ureno, Cristiano Ronaldo, 37.
.
Inadaiwa kuwa Ronaldo atawasili Saudia siku chache zijazo kwa ajili ya vipimo kabla hajasaini mkataba wa miaka miwili utakaomwezesha kukunja Pauni 175 milioni kwa mwaka.
.
Ronaldo kwa sasa ni mchezaji huru baada ya mkataba wake na Man United kusitishwa. Al Nassr ndio timu pekee ambayo ina zaidi ya asilimia 80 za kumnasa Ronaldo kutokana na ofa ambayo imeiweka mezani. Awali, mwenyewe alikuwa akitamani kuendelea kucheza soka la ushindani barani Ulaya lakini hadi sasa hakuna timu iliyoonyesha kumtaka.
.
Screenshot_20221229_050436_OGInsta%2B.jpg
 
BERKANE YATENGA BILIONI 1.2 KWA MAYELE
.
Taarifa kutoka ndani ya Yanga ni kwamba mabosi wa juu wa klabu hiyo juzi walinasa taarifa nzito wakipata uhakika kwamba mshambuliaji wao Fiston Mayele anatakiwa na klabu bingwa mtetezi wa Kombe la Shirikisho Afrika, RS Berkane.
.
Berkane inasaka straika hatari anayejua kufunga na akili yao imetua kwa Mayele walianza kuwashawishi watu wa karibu wa nyota huyo ili avunje au kununua mkataba wake kisha wampe pesa ndefu ambayo ataishangaa.
.
Mayele ametengewa kiasi cha Dola 550,000 (Sh 1.2 bilioni) kama atakubaliana kuvunja mkataba wake na Yanga ili atue haraka nchini Morocco. Pamoja na Mayele kueleza anataka kupata changamoto mpya ila Dili hili linaweza kuwa gumu kutokana na vigogo wa Yanga kuwa na rekodi ya kukaza kumuachia mchezaji.
Screenshot_20221229_050547_OGInsta%2B.jpg
 
Erling Halaand, mabao 20 na assists tatu! Mchezo uliotamatika hivi punde ni wao City dhidi ya Leeds, amerudi kambani mara mbili.
Screenshot_20221229_050923_OGInsta%2B.jpg
 
Pep Guardiola kwa timu za EPL wasipokuwa makini nae ataigeuza kuwa Farmer’s League, anazidi kudhihirisha ubora wake na City, Arsenal watuepushe na kikombe hiki
Screenshot_20221229_051012_OGInsta%2B.jpg
 
Wachezaji wa England na mzimu wa majeraha kwenye umri mdogo sana

Theo Walcott yalimkumba, Jack Wilshere na hata Marcus Rashford, hivi sasa Reece James anapambana.
Screenshot_20221229_051105_OGInsta%2B.jpg
 
Wakala wa Cristiano Ronaldo, Jorge Mendes amesitisha maongezi na Al Nassr ya Saudi Arabia baada ya kupokea ofa kutoka timu ya Ulaya inayoshiriki kwenye ligi ya mabingwa.

Screenshot_20221229_051201_OGInsta%2B.jpg
 
Kwa mujibu wa Mwandishi @fabriziorom ni kuwa tayari nyota Cody Gakpo yupo jijini Liverpool kwa ajili ya kukamilisha vipimo vya afya ili nyota huyo asaini kandarasi na ikiwezekana awepo kwenye mchezo unaoafuata wa Liverpool.
Screenshot_20221229_051300_OGInsta%2B.jpg
 
Kwa mujibu wa Mwandishi Nizaar Kinsalla ni kuwa Chelsea wapo tayari kulipa kiasi cha Pauni Million 105 kwa ajili ya kuinasa saini ya kinda Enzo Fernandes kutoka Benfica ya Ureno, ambapo hiyo ndio ada yake ya uhamisho kwa mujibu wa mkataba.
Screenshot_20221229_051704_OGInsta%2B.jpg
 
Kwenye mechi ya Champions League Man United dhidi ya Milan, Giggs alimchezea faulo mbaya Kaka na ghafla Mbrazil alisimama na kumkaba Giggs kisha wakawekwa sawa.

Giggs baada ya mchezo akashangaa wakati wanaelekea vyumbani mbele yake kuna Gatusso na Kaka, kumbe Kaka alikuwa anamsubiri Giggs ili amwombe tu msamaha kwa kilichotokea uwanjani japo ndie yeye aliyetendewa kosa.

Football is more than a game
Screenshot_20221229_051819_OGInsta%2B.jpg
 
Dennis Zakaria yupo kwa mkopo Chelsea akitokea Juventus, moja kati ya kiwango bora ameonesha ni mechi ya jana dhidi ya Bournemouth, alkuwa super kwenye kila kitu.

Wiki chache nyuma kulikuwa na taarifa huenda Chelsea wangemrejeshe Turin lakini nadhani ameonesha thamani yake.
Screenshot_20221229_051924_OGInsta%2B.jpg
 
MSHAMBULIAJI mpya wa Singida Big Stars, Ibrahim Ajib juzi aliuteka Uwanja wa Jamhuri wakati timu hiyo ikiibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Dodoma Jiji.
Ajib hakucheza aliwasili uwanjani na kuelekea jukwaa kuu huku mashabiki wakimshangilia muda wote na yeye alikuwa akiwapungia.

Mara baada ya mchezo kumalizika mashabiki wengi walikuwa wakiomba kupiga naye picha lakini mshambuliaji huyo alikimbilia kwenye basi la timu hiyo na kuondoka na wachezaji wenzake.

Akiwa jukwaa kuu muda wote alikuwa akifurahi na baadhi ya viongozi wa SBS na Mwanaspoti lilipotaka kuzungumza naye juu ya maisha yake mapya kwenye timu hiyo, Ajib alisema hawezi kuzungumza jambo lolote kwani mabosi wake ndiyo wenye mamlaka ya kuzungumza juu ya hilo.

Screenshot_20221229_052045_OGInsta%2B.jpg
 
Uongozi wa Yanga umetuma maombi kwa klabu ya Azam FC ikihitaji huduma ya nyota wake wawili James Akaminko na Kipre Jr. Uongozi wa Azam FC umethibitisha kupokea barua hiyo na walichokisema undani wa dili hilo usikose gazeti la Mwanaspoti kesho Alhamisi Desemba 29, 2022.

Screenshot_20221229_052207_OGInsta%2B.jpg
 
Uongozi wa Yanga umetuma maombi kwa klabu ya Azam FC ikihitaji huduma ya nyota wake wawili James Akaminko na Kipre Jr. Uongozi wa Azam FC umethibitisha kupokea barua hiyo na walichokisema undani wa dili hilo usikose gazeti la Mwanaspoti kesho Alhamisi Desemba 29, 2022.
Screenshot_20221229_052207_OGInsta%2B.jpg
 
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (Sua), Dk Felix Nandonde amesema kuanzishwa kwa kiwanda cha sukari Bagamoyo, Mkoa wa Pwani ni jambo kubwa ambalo litasaidia kupunguza uhaba wa sukari nchini.

Dk Nandonde amebainisha hayo leo Jumatano, Desemba 28, 2022 wakati akichangia mjadala kuhusu matukuo ya mwaka 2022 katika Mwananchi Twitter Space.

"Kwa sasa Bagamoyo Sugar wanazalisha tani 30,000 lakini kufikia mwaka 2030 watafikia tani 100,000. Wameanza vizuri kwenye hili na matumaini ni makubwa siku zijazo," amesema Dk Nandonde.

"Serikali inatengeneza mazingira wezeshi na moja ya mambo ambayo wafanyabiashara wanahitaji ni maeneo ya kufanyia biashara. Hili linawezekana tukalipatia dawa," amesema Dk Nandonde.
Screenshot_20221229_052946_OGInsta%2B.jpg
 
“Ninaomba mwaka 2023 Serikali iondoe hicho kikokotoo cha wastaafu, waonewe huruma, wangapi wastaafu ambao hawajalipwa hadi leo,

Kipindi hiki kimekuwa kigumu sana, hili limekuwa tatizo, mtu anastaafu hakujenga nyumba hana kodi ya kulipa halafu hapewi nauli ya kurudi kwao na anazungushwa. Jamii ya wastaafu inalia”- Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Kutetea na Kupambania Haki za Abiria (Shikuhata), Ambakisye Mwakifwange

Screenshot_20221229_053050_OGInsta%2B.jpg
 
Mhariri msaidizi wa habari wa gazeti la Mwananchi, Ibrahim Yamola amesema tukio la mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kutoka gerezani, Machi 4, 2022 baada ya kukaa kwa miezi nane gerezani kutokana na makosa mbalimbali yaliyokuwa yakimkabili ikiwemo la uhujumu uchumi kisha kwenda kuonana na Rais Samia Suluhu Hassan, Ikulu ya jijini Dar es Salaam yamepunguza joto la kisiasa nchini.

“Kukutana kwa Rais Samia na Mbowe kulizaa maridhiano yanayoendelea mpaka sasa baina ya Chadema, CCM na Serikali ambayo mwisho yanaweza kuwa na matokeo chanya kwa jamii na Taifa.

Matamanio ya Watanzania sasa ni kutaka kujua baada ya miezi takribani nane ya majadiliano hayo, ni nini hasa wamekubaliana” amesema Yamola

Screenshot_20221229_053141_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom