Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,870
Mhariri msaidizi wa habari wa gazeti la Mwananchi, Ibrahim Yamola amesema tukio la kujiuzulu kwa Spika wa Bunge Job Ndugai Januari 6 ni miongoni mwa matukio yaliyoibua mjadala ndani na nje ya CCM hadi kufikia kujiuzulu.
Ndugai ambaye ni mbunge wa Kongwa aljiuzulu, baada ya kumuandikia barua Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo akibainisha kuwa uamuzi huo wa kuachia nafasi hiyo ameufanya kwa hiari ikiwa ni siku chache kupita tangu kueleza tahadhari ya serikali kuendelea kukopa nje ya nchi.
“Kabla ya Ndugai kuchukua uamuzi wa kujiuzulu wanachama na wabunge wenzake wa CCM walimshambulia na kila aina ya lugha zilitolewa. Ni tukuio la kukumbukwa.
Mara baada ya kujiuzulu, aliyekuwa naibu spika, Dk Tulia Ackson alipitishwa na CCM kuwa mgombea uspika na akashinda kuongoza Bunge” amesema Yamola
Ndugai ambaye ni mbunge wa Kongwa aljiuzulu, baada ya kumuandikia barua Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo akibainisha kuwa uamuzi huo wa kuachia nafasi hiyo ameufanya kwa hiari ikiwa ni siku chache kupita tangu kueleza tahadhari ya serikali kuendelea kukopa nje ya nchi.
“Kabla ya Ndugai kuchukua uamuzi wa kujiuzulu wanachama na wabunge wenzake wa CCM walimshambulia na kila aina ya lugha zilitolewa. Ni tukuio la kukumbukwa.
Mara baada ya kujiuzulu, aliyekuwa naibu spika, Dk Tulia Ackson alipitishwa na CCM kuwa mgombea uspika na akashinda kuongoza Bunge” amesema Yamola