Makapuku Forum

Baada ya michezo 236 na kukimbiza LA LIGA kwa kucheza mechi zote kwa miaka sita mfululizo, juzi Inaki Williams amepata majeraha ambayo yanaweza kumfanya akae nje kwa muda.

Hatimae rekodi yake ya kutokosa mchezo wowote wa ligi hiyo imefika tamati.

Ikumbukwe Inaki alitembelea Ghana mwaka huu na amechagua kuvaa jezi ya taifa hilo kuelekea Qatar.
 
Shaffih Dauda

JARIBU KUTAZAMA MACHAGUO NDANI YA YANGA

Morrison - Mayele - Kisinda
Morrison - Mayele - Moloko
Farid Mussa - Mayele - Nkane - Ambundo

Kwa Mfano tu, Yanga ikaamka ikasema mechi ya leo tunataka tucheze sana mpira, pasi nyingi na kukimbia kidogo.

Yanga wataanza na winga mmoja, Farid Mussa, Winga mwingine Morrison, kati Fiston Mayele.

Kuna siku Yanga itaamka itasema, mechi ya leo tunataka tukimbizane, ni mwendo wa mipira mirefu kwa winga zake za pembeni.

Yanga wataanza na winga moja Tuisila Kisinda, Winga mwingine Moloko, kati ni Fiston Mayele.

Yanga wana machaguo kinachobaki ni kuchagua aanze yupi na nani atasubiri.

Na uzuri wa Yanga hii ya sasa, kila mchezaji yupo na utofauti kwa aina yake ya uchezaji.

Itakua ni mwendo wa ichukue hapa, iweke pale, niiikute kule.

Over to you Coach NABI!
 
“Wakati tumecheza na Barcelona 2016, wachezaji wenzangu wote walikuwa wanahitaji kubadilishana jezi na wachezaji wa Barca, mimi sikutaka kubadili na yoyote ila halftime Suarez alinifuata na kuomba tubadilishane”

- Jamie Vardy, mshambuliaji wa Leicester City.
 
Baada ya Jordan Henderson kupata majeraha usiku wa jana Liverpool wameulizia uwezekano wa kumpata Kiungo wa Juventus Arthur Melo kwa mkopo.

Inasemekana dili lipo kwenye hatua za mwisho na tayari Melo amepanda ndege kuelekea Liverpool ilo kukamilisha uhamisho huo ikizingatiwa kuwa Liverpool wana majeruhi wengi.
 
Mwamba Edison Cavani amesaini kwenye klabu ya Valencia inayoshiriki Laliga nchini Hispania.

Anatambulika kama El Matador ikiwa na maana ya Bullfighter, alipewa jina hilo na Mashabiki wa Napoli ya Italia kutokana na aina yake ya uchezaji.

Cavani amezaliwa jiji moja na Luis Suarez huko nchini kwao Uruguay, jiji linaitwa Salto na wamepishana siku 21 tu, Cavani yupo Hispania ambapo Suarez pia alipita.

Nyota huyo ndie mfungaji bora wa muda wote wa PSG akiwa na mabao zaidi ya 200 klabuni hapo.

 
OFFICIAL
| Klabu ya Al Ahly
imemfuta kazi Kocha Mkuu, Ricardo Soares
baada ya miezi miwili tu tangu aajiriwe.

17 - Michezo
09 - Kushinda
05 - Sare
03 - Kupoteza

Al Ahly kazi kazi
 
| Pande mbili zipo kwenye mazungumzo ambapo upande wa Tyson Furry na Aleksander Usyk wapo katika hatua za mwisho juu ya pambano la wababe hao wawili.

Usyk alifanikiwa kutetea mikanda yake mitatu ya WBF, WBO na IBF dhidi ya Antony Joshua na sasa anautaka mkanda wa WBC ambapo unashikiliwa na Gypsy King.

Taarifa zinadai kuwa pambano hilo huenda likapelekwa tena Saudi Arabia ijapo Qatar, Falme za Kiarabu na Marekani wanalitaka pia.

Tarehe rasmi ya pambano bado haijawekwa wazi ila inasemekana huenda ni Februari,2023.
 
SINGIDA YAMTEMA MWENDWA
.
Klabu ya Singida Big Stars imeachana na aliyekuwa winga wake mshambuliaji, Harrison Mwendwa
ikiwa ni mwezi mmoja tu tangu iingie naye mkataba wa mwaka mmoja.
.
Nyota huyo aliyesajiliwa kutoka Kabwe Warriors ya Zambia ili kuongeza nguvu eneo hilo ameachwa rasmi huku ikielezwa sababu kubwa ni majeraha.

……………
 
WEZI WAMVUNJA TAYA AUBAMEYANG
.
Supastaa straika, Pierre-Emerick Aubameyang ameripotiwa kuvunjika taya baada ya kushambuliwa na wezi wanne waliovamia nyumbani kwake wikiendi iliyopita. Staa huyo wa Barcelona alipigwa na kipade cha chuma kidevuni wakati akijaribu kupambana na wezi hao wasidhuru familia yake.
.
Na sasa ripoti zinafichua, Aubameyang, 33, aliumizwa taya kwenye tukio hilo. Jambo hilo litamfanya kuwa nje ya uwanja kwa wiki kadhaa na kuna uwezekano akafanyiwa upasuaji.
.
Upasuaji utamfanya mchezaji huyo kupona haraka kuliko akisubiri taya lipone lenyewe. Lakini, jambo hilo linaweza kutibua mpango wa Chelsea kunasa saini ya mshambuliaji huyo wa zamani wa Arsenal ili kurudi kukipiga Ligi Kuu England.
 
GagfatyaujH£#@&"*
Kwahiyo ni vyema huyo mwalimu na nesi akaongezewa kodi zaidi ili kumpata huyo mfugaji!! Akili ya wapi hii🙆🙆🙆
 
Yaani hata waelezee wamevua nguo, hawawezi kueleweka.
 
World Economic Forum imetoa orodha ya nchi 10 duniani zinazowalipa walimu mishahara mikubwa zaidi.

10. Austria : $62,882 (Sawa na TZS 146,640,824)
9. Ireland : $62,906 (Sawa na TZS 146,696,792)
8. Denmark: $64,259 (149,851,988)
7. Mexico: $64,491 (Sawana TZS 150,393,012)
6.United States: $65,248 (Sawa na TZS 152,158,336)
5.Australia: $65,714 (Sawa na TZS 153,245,048)
4: Canada: $71,664 (Sawa na TZS 167,120,448)
3. The Netherlands: $81,064 (Sawa na 189,041,248)
2. Germany: $91,041 (212,307,612)
1. Luxembourg: $109,204 (Sawa na 254,663,728).

 
Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amesema wananchi ndio walioshauri Serikali ipanue wigo wa tozo za miamala kwa kujumuisha miamala yote ya kielektroniki, ili wananchi wote wachangie maendeleo.

Ameeleza kuwa awali miamala iliyokuwa ikitozwa ni iliyokuwa ikifanyika kwa simu pekee.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…