Makapuku Forum

🀣🀣🀣🀣🀣
 
 
William Samoel Arap Ruto mwenye miaka 55, alimaliza chuo mwaka 1990 akaajiriwa kama mwalimu kwa miaka miwili. Amewahi kuwa Mbunge na Waziri, amewahi kuwa na mikasa kibao kisiasa.
.
Bwana Ruto kachanguliwa kuwa Rais wa taifa jirani la Kenya, na kuchaguliwa kwake kunanikumbusha haya:
.
1. HAKUNA ADUI WA KUDUMU, HAKUNA RAIS WA KUDUMU : Ruto alikuwa rafiki wa Raila Odinga, baadae akawa adui yake. Ruto akawa rafiki wa Uhuru Kenyatta wakashirikiana kumshinda Raila Odinga mwaka 2013, na mwaka huu Ruto amekuwa hasimu wa Kenyatta, Kenyatta amekuwa rafiki wa Odinga. Sitaki kuandika sana lakini nakuuliza rafiki yako ni nani? Ni rafiki wa kimkakati ama vipi? : Yes, kuna urafiki ambao tunatengeneza kimkakati tu, ishi na huo urafiki kimkakati. Labda ni kwa malengo ya siasa ama biashara au faida nyingine. Linda maslahi yako katika huo urafiki utakapoisha usiishe kwa hasara.
.
2. DHAHABU INAWEZA KUOKOTWA KWENYE TOPE.
Huyu Ruto ni mtu aliyewahi kuchafuka sana, maisha yake ni kesi tupu. Kesi za kuiba ardhi kashakumbana nazo (2019 aliambiwa kapora ekari 900 , 2001 alikuwa na kesi ya Weston Hotel, 2004 alikuwa na skendo ya KPC Ngong Forest), 2016 alihusishwa na mauaji ya mfanyabiashara Jacob Juma, bila kusahau kesi kubwa ya mahakama ya Kimataifa 2010 alipohusishwa na mauaji na fujo za baada ya uchaguzi wa 2007 (alihusishwa na kuchoma kanisa huko Kiambaa mwaka 2008). Sasa sijui kama kesi ni za kweli au laa, ninachojikumbusha hapa ni kwamba mtu huwezi kuwa ubwabwa na maharage upendwe na kila mtu, na katika safari ya kukua huwezi kuepuka kusemwa, kuchafuka na kuchafuliwa. Lakini halipswi kuzuia harakati, songa mbele.
.
3. ODINGA MMMMH.
Raila Odinga kagombea Urais mara 5 (1997,2007,2013, 2017 na hii 2022) kote hajashinda. Ruto alitaka Urais 2007 lakini hakupitishwa ndani ya chama Chake, 2013 na 2017 kawa upande wa Uhuru. Hivyo inatosha kusema kagombea Urais hii mara moja na kashinda. Aah, sijui nisemeje hapa lakini nakuombea siku moja dili yako MOJA IWE YA UHAKIKA. Labda unasubiri, kuwa mvumilivu mpaka wakati wa Mungu. Sijifunzi chochote hapa sikufundishi chochote hapa mimi sio mjuzi wa mambo, ninachosema, NAKUOMBEA HERI.
.
 
Rais mteule wa Kenya, aliyetangazwa muda mchache uliopita na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) ya Kenya, William Ruto ameahidi hatalipa kisasi kupambana na yoyote aliyekosana naye.

Ruto ametoa kauli hiyo leo, Jumatatu Agosti 15, 2022 mara baada ya kukabidhi cheti cha ushindi na Mwenyekiti wa IEBC, Wafula Chebukati ambaye alimtangaza mshindi kwa kupata kura milioni 7.1 akimshinda mpinzani wake wa karibu Raila Odinga aliyepata kura milioni 6.9

Mwanasiasa huyo amesema hakuna sababu kwa yoyote yule kuwa na wasiwasi kwakuwa yeye ni kiongozi wa Wakenya wote waliomchagua na wasiomchagua.

Ameahidi kufanya kazi na wapinzani kwa kiwango kinachostahili kwa kuwa wao ndiyo jicho la utendaji wa Serikali huku akimshukuru Rais Uhuru Kenyatta kwa kufanya naye kazi kwa miaka 10 katika mazingira mbalimbali na ataendeleza msingi imara unaoachwa na kiongozi huyo kwa faida ya Wakenya.
 
Afadhali....
Maana nilikuwa najiuliza wale wabaya wake itakuwaje sasa?

Ila Ruto ni Hustler Aiseeeee....
 
Hongera kwa Hustler WSR.
 
Jana Sir Alex Ferguson alisafiri mpaka Scotland kutazama mchezo wa kufuzu hatua ya makundi UEFA kati ya Rangers na PSV ya Uholanzi.

Alikutana na mchezaji wake wa zamani ambaye kwasasa ni Kocha wa PSV, Ruud Van Nisterloy.

United mpo tayari? Si mnaelewa mambo ya Babu Fergie
 
Kama kuna namna ya kumpa maua yake Kocha Fred Felix Minziro ayanuse ingali yu hai basi ni sasa, mzawa huyu ni ndugu yetu huyu anapambana kuonesha inawezekana

Kazipandisha timu kadhaa Premier League na akafukuzwa ila bado alirudi chini na kuanza upya, habahatishi anaonekana wala halalamiki ila akipewa wasaa wa kuonesha basi atawapa 100%

Msimu uliyopita kamaliza ndani ya nne bora, akiwa ni Kocha pekee mzawa kwenye nafasi ya nne bora! Yes ukiachana na Matola ambaye alikuwa Kocha wa mpito

Sasa yupo kimataifa na Geita yake, wachezaji wengi hawana majina ya kutisha lakini Mwalimu Minziro kawafanya watishe kwenye dakika 90 za mchezo, what a man

Kama kuna muda wa kumpa sifa zake basi ni sasa, lets do it before its too late
 
Shaffih Dauda

Simba bado wana changamoto ya uwiano wa kikosi, wana viungo wengi sana waliofanana kiasi ambacho waliteseka sana first half, kilichosaidia ni uzembe wa Geita ambao hawakuonekana kuwa na utulivu.

Edmund John, Kelvin Nashon na Yusuph Kagoma ni hazina kwa taifa, wameanza palepale walipoishia na wanazidi kuimarika leo walikuwa watulivu zaidi

Well Kiungo mkabaji pale Simba ni kichomi, licha ya kufunga sana ila Striker ni kichomi na hata yule George Mpole leo alijipa mechi yake na kuisahau timu aachane na kivuli chake cha msimu uliopita
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…