Makapuku Forum

Makapuku Forum

Waziri wa Nishati, January Makamba kwenye ziara yake ya Kijiji kwa Kijiji, amefika kwenye kijiji cha Ugundu kata ya Ifucha kwenye Manispaa ya Tabora na kupokea kero mbalimbali za Wananchi wa Kijiji hiko.

Wananchi wa eneo hilo wamemueleza Waziri Makamba kuhusu kero ya kutokuwa na umeme toka Tanzania imepata uhuru ambapo Waziri wa Nishati amewahidi kuwa kazi ya kupeleka umeme kwenye Kata hiyo itaanza tarehe 25 Agosti, 2022 na Mkandarasi ameshapatikana ambaye ni kampuni ya Ceylex.

Waziri Makamba anaendelea na ziara katika mikoa mbalimbali nchini akiwa na malengo ya kusikiliza maoni, kero za Wananchi na kuzitatua, kukagua miradi ya nishati pamoja na kuhamasisha matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia.
Screenshot_20220725-035629_OGInsta%2B.jpg
 
Watu wanne wamenusurika kifo mara baada ya bajaji namba MC 567 CJK aina ya TVS iliyokuwa ikitoka maeneo ya stendi kuu ya mji wa Njombe kuelekea katikati ya mji kupinduka kutokana na mlipuko mkubwa wa simu ya abiria uliosababisha moto.

RPC wa Njombe Hamis Issah amesema bajaji hiyo imepinduka kutokana na dereva kugeuka nyuma kutokana na taharuki ya kulipuka kwa simu ndogo mali ya Siston Antony katika Barabara kuu ya Njombe-Songea majira ya saa tano asubuhi.

“Moto umelipuka mkubwa na dereva wa bajaji akageuka kuangalia abiria wake na kushindwa kuiongoza akaiachia bajaji wakapinduka, baada ya ajali hiyo Polisi imeingilia kati kutokana na Mmiliki wa bajaji kutaka kulipwa na abiria ambaye ni Mmiliki wa simu iliyosababisha mlipuko na kupelekea kupinduka kwa bajaji na kuharibika”

Aidha Kamanda Issa ametoa wito kwa Wamiliki wa vyombo vya moto kuwa na bima za vyombo vyao ili kuepusha usumbufu kama huo huku pia akitoa rai kwa Wamiliki wa simu kuwa makini na matumizi ya simu zao na kusema abiria wote walipelekwa Hospitali kwa ajili ya matibabu ya majeraha madogo na kuruhusiwa kutoka ili kuendelea na shughuli zao.
Screenshot_20220725-040328_OGInsta%2B.jpg
 
Shirika la Afya Duniani WHO limeutangaza mlipuko wa ugonjwa wa Homa ya Nyani ambao tayari umeathiri zaidi ya Watu 17,000 katika nchi 74 duniani kuwa dharura ya afya ya Ulimwengu, hiyo ni tahadhari ya juu kabisa inayoweza kutolewa na Shirika la WHO kuhusu dharura yoyote ya kiafya Ulimwengu.

Mkuu wa WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus ameuambia mkutano wa waandishi habari mjini Geneva kwamba ameamua kuitangaza Homa ya Nyani kuwa dharura ya kiafya duniani baada ya Timu ya Wataalamu kushindwa kufikia makubaliano.

Amesema tathmini ya WHO inaonesha kitisho cha Homa ya Nyani duniani bado ni cha wastani isipokuwa barani Ulaya ambako maambukizi yanaongezeka.

Marekani imeikaribisha hatua hiyo ya WHO katika wakati maambuki yakiongezeka huku asilimia 98 ya walioambikizwa wakiwa ni Wanaume wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja.
Screenshot_20220725-040424_OGInsta%2B.jpg
 
Nitaulizwa kuhusu jinsia, umri na hali za ndoa?
Jibu ni NDIYO. Siku ya sensa, kurekodi jinsia ya mtu ni muhimu. Ni miongoni mwa maswali yatakayoulizwa.
Swali hili linataka kujua jinsi ya kila mtu. Majibu ya swali hili yatatuwezesha kujua idadi ya wanaume na wanawake katika kila kaya, kila kitongoji, kijiji/mtaa, kata/shehia, wilaya, mkoa na pia Taifa.
Pia swali la umri litaulizwa. Swali hili linakusudia kupata umri kamili wa kila mwanakaya. Umri ni taarifa muhimu sana katika takwimu za watu kwenye Taifa lolote lile hapa duniani.
Kwa kujua umri, Serikali itaweza kupanga mipango yake ya kuboresha afya, elimu, maji, maendeleo ya jamii na mengine mengi bila kukosea.
Ili kuiwezesha serikali kuweka mikakati ya maendeleo, ni jambo muhimu idadi ya wazee, vijana na watoto ikajulikana. Na namna ya kujua idadi yao ni kwa kupitia zoezi la sensa mwaka huu. Sensa ya Watu na Makazi itafanyika nchini Agosti 23, 2022
Screenshot_20220725-041437_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia Suluhu Hassan amewaonya baadhi ya waendesha bodaboda kuacha kutumika katika ujambazi na kukwapua mizigo ya watu ili kulinda heshima yao.

Rais Samia ameyasema hayo leo Jumapili Julai 24, 2022 wakati alipompigia simu Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ,Anthony Mtaka kuzungumza na madereva bodaboda na bajaji.

Madereva hao wamekutana katika kongamano la kuimarisha ushiriki katika sensa ya makazi na watu ya mwaka 2022 jijini Dodoma ambapo pamoja na suala la sensa watapata nafasi ya kutoa changamoto zao mbalimbali kwa Serikali.
Screenshot_20220725-041542_OGInsta%2B.jpg
 
Mwanamuziki na muigizaji mkongwe kutoka nchini Marekani, Jennifer Lopez maarufu J Lo amebadili jina na rasmi sasa atatambulika kama Jennifer Affleck baada ya kukamilisha taratibu za kisheria za kutumia jina la mwisho la mumewe Ben Affleck.

Katika nyaraka ya leseni ya ndoa iliyosambaa mitandaoni inaonyesha mabadiliko hayo ya jina la mwanamama huyo mwenye umri wa miaka 53.

Ben na Jen wamefunga ndoa Julai 16, mwaka huu mjini Las Vegas, Marekani miaka 20 baadaye tangu wawili hao walipochumbiana mwaka 2002 kabla ya kukatisha uhusiano wao mwaka 2004.
Screenshot_20220725-041632_OGInsta%2B.jpg
 
Mfanyakazi wa Wizara ya Kilimo, Frorence Samwel anadai fidia ya Sh500 milioni Hospitali za TMJ na Hindu Mandal za jijini Dar es Salaam na daktari Moirice Mavura kwa kile anachodai kuwa ni uzembe katika kumtibu.

Pia amedai alipwe Sh53 milioni kwa ajili ya gharama mbalimbali, ikiwemo ya matibabu na usafiri

Frorence amefungua kesi hiyo dhidi ya Dk Mavura pamoja na hospitali hizo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, akidai kuwa hospitali hizo zilifanya uzembe alipokwenda kupata huduma ya matibabu.
Screenshot_20220725-041735_OGInsta%2B.jpg
 
Mfanyakazi wa Wizara ya Kilimo, Frorence Samwel anadai fidia ya Sh500 milioni Hospitali za TMJ na Hindu Mandal za jijini Dar es Salaam na daktari Moirice Mavura kwa kile anachodai kuwa ni uzembe katika kumtibu.

Pia amedai alipwe Sh53 milioni kwa ajili ya gharama mbalimbali, ikiwemo ya matibabu na usafiri

Frorence amefungua kesi hiyo dhidi ya Dk Mavura pamoja na hospitali hizo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, akidai kuwa hospitali hizo zilifanya uzembe alipokwenda kupata huduma ya matibabu.View attachment 2302843
hi kesi nitaifuatilia
 
Golikipa wa KMC, Faruk Shikhalo ameaga uongozi wa KMC baada ya kuchezea kwa msimu mmoja akitokea Yanga. Shikhalo kupitia akaunti yake ya Instagram ameandika "Imekuwa ni furaha kufanya kazi pamoja. Niwatakie kila la kheri. Asanteni sana."
Screenshot_20220725-042757_OGInsta%2B.jpg
 
KIUNGO fundi wa mpira wa timu ya wanawake ya Yanga Princess, Fatuma Ibrahim ‘Fetty Didier’ amelamba shavu baada ya kusajiliwa na klabu ya soka ya Neesatromitou iliyopo Ugiriki kwa mkataba wa miaka miwili.

Fetty alikuwa mmoja ya nyota walioiwezesha Yanga kumaliza katika nafasi ya tatu kwenye Ligi Kuu ya Wanawake (WPL), nyuma ya mabingwa Simba Queens na Fountain Gate Princess.

Kupitia ukurasa wa klabu hiyo ya Ugiriki ilimtambulisha rasmi Fetty kujiunga kuitumikia timu hiyo.

Screenshot_20220725-042858_OGInsta%2B.jpg
 
Alichoandika msemaji wa Simba, Ahmed Ally kutokea kambi ya Simba nchini Misri.

"Ni siku 8 za Pre Season bado hatujakua na timu ya ushindani lakini tuna timu inayoimarika kwa kasi sana

Hizi mechi sio za kutafuta ushindi ni mechi za kuangalia tumeimarika wapi na wapi panavuja ili tuzibe mapema

Kitu kizuri ni kwamba timu inazidi kujengeka, wachezaji wanazidi kuzoeana

Na muhimu zaidi ni kwamba wachezaji wanaelewa mafunzo na maelekezo ya mwalimu

Furaha haiko mbali nasi na Insha Allah wiki mbili zijazo tutakua bora zaidi,"

Screenshot_20220725-042959_OGInsta%2B.jpg
 
Yanga kujipima na MLANDEGE
.
Taarifa zinaeleza kikosi cha Yanga kinatarajia kucheza mchezo wa kwanza wa kirafiki na Mlandege ya Zanzibar kwaajili ya kujiweka fiti. Mechi hiyo inatarajiwa kuchezwa Jumanne huko Avic Town, Kigamboni.
Screenshot_20220725-043142_OGInsta%2B.jpg
 
MMEMSIKIA Thomas Tuchel?? Baada ya kupokea kipigo cha bao 4-0 kwa Arsenal:
.
[emoji860] "Nimeona timu ya Arsenal ambayo kiakili inajitoa kwa kiwango kikubwa kiasi kwamba hatukuweza kulingana nao wala kushindana nao kwanguvu na kiakili kwa sababu tuna wachezaji wengi ambao wanafikiria kuondoka klabuni."
Screenshot_20220725-043319_OGInsta%2B.jpg
 
YONDANI ANA MZUKA NA CAF
.
Beki mkongwe wa Geita Gold, Kelvin Yondani amesema nafasi iliyopata timu hiyo katika kushiriki michuano ya CAF itatoa fursa zaidi kwa wachezaji chipukizi kuviweka sokoni vipaji vyao.
.
“Yanga imemsajili Stephane Aziz Ki alionekana akicheza dhidi ya Simba akiwa na Asec Mimosas hata Luis Miquissone alitua Simba kupitia michuano ya CAF akiwa na UD Songo, hivyo ni fursa kwa wachezaji wenzangu wa Geita kujituma ili wajiuze kama wenzao,” amesema Yondani
Screenshot_20220725-043841_OGInsta%2B.jpg
 
Back
Top Bottom