Makapuku Forum

Makapuku Forum

Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa ametoa taarifa kwa Wafanyakzi nchini kwamba Jumanne July 26, 2022 Serikali itakutana na Viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) ili kuwasikiliza na kutoa ufafanuzi kuhusu nyongeza ya mishahara katika mishahara ya July, 2022.

Hatua hii inakuja kufuatia malalamiko ya Wafanyakazi baada ya kukutana na nyongeza wasiyoitarajia kwenye mishahara yao ya mwezi Julai, 2022.

Itakumbukwa Rais Samia alitoa ahadi ya kuongeza mishahara kwenye Maadhimisho ya Mei Mosi ambapo baadaye alitimiza ahadi hiyo na kuridhia nyongeza ya 23.3% lakini Wafanyakazi wameonekana kutoridhishwa na kiwango cha nyongeza walichokutana nacho kwenye mishahara yao.
Screenshot_20220725-035028_OGInsta%2B.jpg
 
Back
Top Bottom