Makapuku Forum

Makapuku Forum

ZORAN AMLETA OUATTARA [emoji881]
.
Inaelezwa mara baada ya kusaini mkataba wa kuinoa Simba, Zoran Maki alielezwa kikosi kina shida ya beki wa kati baada ya kuachana na Pascal Wawa.
.
Zoran aliwaeleza viongozi hao wa Simba wamvute beki wa kati wa Al Hilal inayoshiriki Ligi Kuu ya Sudan, Mohamed Ouattara (29) raia wa Burkina Faso.
.
Inadaiwa Zoran aliwaambia viongozi hao wa Simba ana uhakika na kiwango bora cha Ouattara, kwani amewahi kufanya nae kazi kwa mafanikio katika klabu mbili tofauti na zote alikuwa akimtumia katika kikosi cha kwanza akianza naye Wydad Casablanca kisha Al Hilal.
Screenshot_20220713-055608_OGInsta%2B.jpg
 
HAALAND ANAWATAMANI MAN U!!
.
Straika tishio wa Manchester City, Erling Haaland alipoulizwa ni mechi gani anayoisubiria kwa hamu kubwa amesema: “Sitaki kuyasema maneno haya, lakini ni Manchester United.”
.
Ikumbukwe Baba wa straika huyo, Alf-Inge alikuwa staa wa Man City, ambapo aliwahi kuchezewa rafu na kuvunjwa mguu na kiungo wa Man United kwa wakati huo, Roy Keane kwenye mechi ya Manchester derby na hilo ndilo linalomfanya Haaland kuwasubiri kwa hamu Mashetani Wekundu.
Screenshot_20220713-055711_OGInsta%2B.jpg
 
TEN HAG: MAGWAYA NDO NAHODHA
WETU
.
Habari ndo hiyo. Kocha Mdachi, Erik ten Hag amethibitisha kwamba beki wa mpira, Harry Maguire ataendelea kuwa nahodha wa Manchester United.
.
Maguire, 29, alikuwa nahodha wa Man United msimu uliopita, lakini uongozi wake ulikuwa kwenye shaka nzito baada ya kucheza chini ya kiwango. Lakini, kocha mpya kikosini hapo, Ten Hag amethibitisha Mwingereza huyo ataendelea kuwa nahodha wa wababe hao wa Old Trafford.
.
Screenshot_20220713-055804_OGInsta%2B.jpg
 
[emoji3578] Farhan Jr

Ndugu zangu leo sitoongea kama Mchambuzi, nitaongea kama Ndugu yenu tu, naomba mchukue huu ushauri kama Ndugu yenu nikizungumza nanyi

Kwenye klabu kubwa na yenye historia kama Yanga mnayo bahati kubwa kucheza tena kwa uwezo mkubwa sana, kwenye klabu kama hii kila msimu ina malengo mapya na mapambano mapya

Yanga itasajili wachezaji wengi wakubwa kwakuwa wao ni wakubwa, najua hilo haliwezi kuwapa hofu zaidi ya kuingia uwanjani na kuendelea kupambana kwakuwa mpira ni mchezo wa wazi

Ikitokea Bangala ameanza eneo la kati na Dick upo bench basi haujapoteza bali utakaa chini na kujifunza, ikitokea Lumalisa kaanza basi Kibwana kaa bench jifunze anachokifanya

Ikitokea wapo bench nanyi mmeanza kikosini basi tumieni yale bora mliyojifunza kutoka kwao kisha ongezeni na maarifa yenu, muhimu ni kuendelea kuwapa sababu kwanini mpo Yanga

Kwetu hakuna kupoteza bali ni kujifunza, kwetu hakuna kukata tamaa bali kuishi na kuwa na sababu ya kuamini, hatujawahi kupoteza mara zote ni kushinda

Dont be obsessed with 90 minutes, ni sehemu ndogo sana kwenye mpira wa miguu! Homeboys dont go home, lets go hard

Ukisikia kwa usajili huu Kibwana basi tena, basi wewe tabasamu kwakuwa mpira wa miguu ni mchezo wa wazi sana, unazo sababu million za kuvaa jezi ya Yanga, wenyewe tunapenda changamoto

Hatushindwi bali tunajifunza, hatufeli bali tunashinda @jobdick05 @kibwana_shomari

Hii sio kama Mchambuzi bali kama ya Ndugu yenu na Homeboy tu, kuna wakati sihitaji mwamvuli wa Uchambuzi kuongea

Screenshot_20220713-060006_OGInsta%2B.jpg
 
[emoji3578][emoji3578] Farhan Jr

Wakati nasoma course ya Sports Management nakumbuka Mwalimu aligusia kitu kuhusu FOOTBALL FANS EVOLUTION, namna Mashabiki wanabadilika kutoka kizazi hadi kizazi

Alisema “In every generation there will be fans with distinctive characters than the former and the latter, very sad but lets agree, football is loosing its true custodians” akamaliza

Ndio zamani Wazee wetu waliweza kushabikia timu zao, wakamuimba Sunday Manara au Zamoyoni Mogella ingali hata machoni hajawahi kumuona, akaisifia Reli, Pamba, Simba, Tukuyu Stars au Yanga ingali hajawahi kuiona, walikuwa Mashabiki halisi

Kikaja kizazi kingine na sifa zake za kipekee, sasa tupo kwenye kizazi cha mpira cha mizuka, umaarufu na tambo nyingi sana ambazo zinaathiri moja kwa moja wachezaji na timu zetu

Leo hii itaundwa hoja ya kumkataa Gael Bigirimana hata kama profile yake ipo wazi, leo hii watamkataa Kapama hata kama anaweza kuleta kitu, wananuna kwakuwa wapo kwenye kizazi cha Showbiz na window shopping

Tupo kwenye kizazi cha mpira ambacho kinataka tuendeshe Bugatti inayotumia injini ya Bodaboda, tupo kwenye kizazi kinachotaka uongo mtamu kuliko ukweli mchungu

Viongozi na Benchi la Ufundi wawe makini na hiki kizazi chetu, wasifanye vitu kisa watu watasemaje! Wafanye kulingana na mahitaji ya timu

Tupo kwenye kizazi hiki ambacho Mchizi yupo na Manzi geto wanacheck season za Kikorea wakati Nassor Kapama anazima pale Kagera, hajawahi kumuona

Tupo kwenye kizazi ambacho Mchizi yupo photoshoot wakati Habib Kyombo anakichafua pale Majimaji, hajawahi kutazama mechi ya Mbeya Kwanza ila ataponda usajili

Tupo kwenye ambacho Gael Bigirimana anaupiga pale EPL ila Msela huku yupo busy kukata pindi Mchikichini ila ataponda usajili



Screenshot_20220713-061158_OGInsta%2B.jpg
 
[emoji3578] Farhan Jr

Vitu anavyofanya Morrison ingekuwa Jonas Mkude angepelekwa hadi hospital kupimwa

Namna anavyozichezea hizi timu kubwa mbili ingekuwa anafanya hayo David Kameta au Eliuter Mpepo basi wangesemwa kwa kila namna

Nafahamu ingekuwa local player kamwe isingekuwa stori nzuri, lakini kwakuwa ni International basi sio stori sana zaidi ya kufurahi tu

Leo hii Vijana wetu wanapisajiliwa timu kubwa wanasemwa kwa kila aina za makala, naumia kuona hayo! Yanasikitisha sana

Kijana mwenye ndoto zake aliyepata rizki timu kubwa anavunjwa moyo, ila upande wa pili wanapongezwa sana na kutambulishwa kwa bakshishi na furaha kubwa

Najaribu kuwaza kama hayo yangefanywa na kijana mwenzetu mwenye alama ya Ndui bega la kulia, pasingekalika

Ila fresh tu, tumeamua kuwapa ukiwa wakiwa nyumbani kwao, wafanyaje sasa
Screenshot_20220713-061453_OGInsta%2B.jpg
 
Vilabu vyote 32 vinapaswa kuzingatia sheria na kanuni za mashindano ili kuepuka usubufu usio wa lazima. Kila timu inapaswa kuwa na kanuni za kashindano kama kuna timu haina kakuni ifike ofisi za DRFA kwa ajili ya kupatiwa kanuni za mashindano.
Screenshot_20220713-061903_OGInsta%2B.jpg
 
Back
Top Bottom