Makapuku Forum

Makapuku Forum

Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), linatoa pole kwa Familia ya marehemu Ngaitepa Marias Lukumay (17) mkazi wa kijiji cha Pangaro Wilaya ya Mwanga Mkoani Kilimanjaro kwa kumpoteza kijana wao kutokana na mvutano uliotokea kati ya Askari wa Hifadhi na Wananchi baada ya mifugo ya Wananchi kukamatwa ndani ya Hifadhi ya Taifa Mkomazi Julai 5, 2022.

Shirika kwa upande wake limesema limeanza kulifanyia uchunguzi wa kina tukio hilo ili kuhakikisha kuwa mahusiano mazuri kati ya wananchi na hifadhi yanaendelea kuwapo kama kawaida.

Aidha, Shirika limesema litaendelea kutoa elimu ya uhifadhi kwa wananchi wanaoishi kandokando ya hifadhi kupitia Mradi wa Ujirani Mwema kuhusiana na Sheria za Hifadhi za Taifa na taratibu za kufuatwa kwa wanaokiuka ikiwa ni pamoja na kufanya shughuli za kibinadamu ndani ya maeneo ya Hifadhi za Taifa ili kuepuka madhara yanayoweza kutokea kunapokuwa na mvutano usiofuata taratibu za kisheria.
Screenshot_20220713-044428_OGInsta%2B.jpg
 
Watu wanane wamepoteza maisha katika ajali iliyohusisha magari mawili likiwemo gari la abiria na gari la mizigo katika Wilaya ya Biharamulo iliyopo Mkoani Kagera usiku wa kuamkia leo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera William Mwampaghale ameelezea ajali hiyo huku akisema kuwa waliopoteza maisha ni Dereva wa gari la abiria akiwa na Marafiki zake wawili waliomsindikiza pamoja na Watu watano wa Familia moja ambao ni Mama na Watoto wake wanne.

Aidha amesema kuwa kwa uchunguzi wa awali umebaini chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa gari la mizigo Raia wa Rwanda ambaye aliendesha gari hilo upande wa kulia ikiwa ni mazoea kama wanavyoendesha nchini kwao kwa kutumia upande wa kulia mwa Barabara.

Kamanda Mwampaghale amesema dereva huyo anashikiliwa na jeshi la Polisi kwa ajili ya kujibu tuhuma hizo.
Screenshot_20220713-045220_OGInsta%2B.jpg
 
Kocha mpya wa Simba, Zoran Manojnlovic leo amezungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es salaaam “Kila nchi ambayo nimewahi kufanya kazi kuna mechi za watani wa jadi, ili kufanya vizuri lazima kuwa na maandalizi ya kucheza mechi za aina hiyo”

“Nimepata mafanikio katika Timu mbalimbali ambazo nimewahi kufundisha, Simba ni Timu kubwa Tanzania na ni changamoto kwangu kwa mafanikio waliyopata Afrika hivyo kuna kazi ya kufanya”

“Nina taarifa kuhusu usajili wote ambao umekuwa ukifanywa na uongozi kwa ajili ya msimu mpya, nipo hapa kuifanya Simba kuwa bora zaidi ya msimu uliopita, mwaka huu ilimaliza nafasi ya pili, msimu ujao kuwa ya kwanza, msimu uliopita ilikuwa kwenye Kombe la Shirikisho Afrika na mwaka huu kufanya vizuri kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika”
Screenshot_20220713-045427_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Sri Lanka, Gotabaya Rajapaksa inaelezwa kuwa anatafakari kulikimbia Taifa hilo la kisiwa kwa kutumia Boti ya doria ya Jeshi la wanamaji baada ya kutokea tofauti kati yake na Maafisa wa uhamiaji katika uwanja wa ndege ambao wamekataa kugonga muhuri passport yake.

Rajapaksa ameahidi kujiuzulu kesho na kupisha njia ya kukabidhi madaraka kwa amani kufuatia maandamano makubwa dhidi yake kuhusu mzozo mkubwa kabisa wa kiuchumi nchini humo, Maafisa wanasema Rais huyo mwenye umri wa miaka 73 alitaka kusafiri kwenda Dubai.

Akiwa rais, Rajapaksa ana kinga ya kukamatwa, na inaaminika anataka kwenda ng'ambo kabla ya kujiuzulu ili kuepusha uwezekano wa kukamatwa lakini Maafisa wa uhamiaji walikataa kwenda katika eneo la wageni mashuhuri kupiga muhuri kwenye passport yake, wakati akisisitiza kuwa hawezi kutumia maeneo ya wasafiri wa kawaida akihofia kushambuliwa.

Kaka yake mdogo, Basil Rajapaksa aliyejiuzulu kama Waziri wa Fedha mwezi Aprili, aliikosa ndege yake mapema leo kwenda Dubai baada ya mkwamo kama huo katika uwanja wa ndege.
Screenshot_20220713-045523_OGInsta%2B.jpg
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam linamshikilia Jonas Ziganyige (71) Mstaafu wa Jeshi la Wananchi, Mkazi wa Mbezi juu kwa tuhuma za kumpiga risasi na kumuua Patient Romwadi (48) Mfanyabiashara, Mkazi wa Wazo Mivumoni, Kinondoni.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya DSM Muliro Jumanne amesema “Taarifa za awali, zinaonesha kuwa tarehe 09.07.2022 majira ya saa 4 asubuhi Recy Renso (52) Mkazi wa Posta alifika eneo hilo na Mtu huyo ambaye ni marehemu kwa sasa kwa lengo la kuangalia mipaka ya kiwanja chake, Mtuhumiwa alitoka ndani huku akionesha kukasirishwa na hatua ya Waty hao, akachukua bunduki na kumpiga risasi Patient Romward ambaye baadae alifariki”

“Baada ya tukio hilo Mtuhumiwa alikimbia lakini upelelezi ulifanywa haraka na tarehe 10.07.2022 alikamatwa eneo la Kibaha Maili Moja akiwa amejificha”

“Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam pia limeipata silaha aliyotumia mtuhumiwa ambayo ni aina ya Mark IV ikiwa na risasi 4, Mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani haraka iwezekanavyo kujibu mashtaka yanayomkabili”
Screenshot_20220713-045639_OGInsta%2B.jpg
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam limemkamata na linamshikilia Selemani Haruna maarufu Kwata (24), Mkazi wa Kimara Temboni mtaa wa Amani, kwa tuhuma za kumuua Editha Charles (22) Mkerewe, Binti wa kazi za ndani na kuuficha mwili huo katika stoo ya vifaa vya ujenzi katika nyumba ya Agatha Stanslaus.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya DSM, Jumanne Muliro amesema “Uchunguzi wa awali umeonesha Mtuhumiwa tarehe 06/07/2022 asubuhi alifika kwenye nyumba aliyokuwa anayoishi Binti huyo wa kazi akijifanya fundi wa umeme na kwamba alitakiwa kuweka Balbu, alipoingia alimshambulia kwa kitu chenye ncha kali Binti huyo na kumuua halafu akavunja chumba cha mwenye nyumba na kuiba Tsh 1,800,000 na kutoweka”

“Polisi kwa Kutumia Watalaamu wake wa uchunguzi wa kisayansi na vyanzo vingine vya kiuchunguzi walibaini Mtuhumiwa huyo kuwa aliingia kwenye nyumba hiyo na kukaa kwa masaa kadhaa na kutoka, baada ya kumkamata na kumhoji kwa kina alikiri kumuua Binti huyo, kuvunja mlango wa chumba na kuiba pesa Tsh 1,800,000 na mwili wa marehemu aliuficha kwenye stoo ya nyumba hiyo huku akiwa ameufunika na vifaa mbalimbali vya ujenzi ili usionekane”

“Alionesha pesa alizoziiba eneo hilo na pesa nyingine alidai mara baada ya tukio siku iliyofuata alinunua simu mpya, viatu vya mpira pea 2, na begi la mgongoni lenye nguo mbalimbali mpya ambavyo navyo vimepatikana, kitendo alichofanya Mtuhumiwa ni cha ukatili ulipita kiasi, uchunguzi wa shauri hili unakamilishwa na atafikishwa katika mifumo ya kisheria ikiwemo Mahakamani haraka”
Screenshot_20220713-045728_OGInsta%2B.jpg
 
Kampuni ya Apple imetangaza mfumo wake mpya uitwao ‘lockdown mode’ ambayo itapatikana katika iOS 16 kwenye simu za iPhone pamoja na iPads, uliopangwa kuzinduliwa baadae mwaka huu.

‘Lockdown mode’ ni mfumo unaolenga wale watu ambao vifaa vyao viko hatarini zaidi kudukuliwa na hii ‘lockdown mode’ itafanya iPhone kuwa moja ya simu salama zaidi zinazopatikana sokoni.

Inasemekana kuwa simu yako ya iPhone ikiwa kwenye hali ya lockdown, hata Serikali ya Marekani haitoweza kuifikia taarifa katika simu bila ridhaa yako.

Ili kuhakikisha kuwa inabaki hivyo, Apple inatoa zawadi ya hadi $2,000,000 (Tsh. 4,662,000,000) kwa wadukuzi ambao wataweza kupata njia za kuepuka huo mfumo wa ‘lockdown’ na kuidukua simu yako, hii imefanywa kama njia ya kuongeza umadhubuti wa mfumo wao mpya.

"Apple hutengeneza vifaa vya simu za mkononi vilivyo salama zaidi kwenye soko," Ivan Krstić, Mkuu wa Uhandisi wa Usalama na Usanifu wa Apple, amesema katika taarifa na kusema Lockdown mode’ ni uwezo wa msingi ambao unaonyesha dhamira yetu ya kulinda watumiaji dhidi ya shambulio la udukuzi.
Screenshot_20220713-045841_OGInsta%2B.jpg
 
Wasichana wanaoishi vijijini nchini Zimbabwe, wanalazimika kutumia kinyesi cha ng'ombe kama taulo za kike, ikiwa kama njia ya kujiweka katika hali ya usafi wakiwa katika siku zao za hedhi, huku mfumuko wa bei ukiathiri upatikanaji wa taulo za kike, kwa wanawake nchini humo.

Asilimia 72 ya Wasichana walioko kijiji cha Domboshava, kilomita 30 kaskazini mwa mji mkuu wa Harare hawawezi kumudu gharama za taulo za kike, kulingana na utafiti wa Shirika la Maendeleo la Uholanzi la SNV nchini Zimbabwe.

Zikiuzwa sawa na $2 ya Kimarekani, pedi ama taulo za kike haziwezi kufikiwa na Wasichana milioni 3 nchini humo walio katika siku zao za hedhi, ambao wanaishi chini ya mstari wa umaskini.

Serikali ya Zimbabwe imefanya jitihada za kupunguza hali hiyo kwa kufuta ushuru kwa bidhaa zote za usafi lakini umaskini wa kipindi hiki unazidishwa na mfumuko wa bei unaofikia zaidi ya 191.6%, kulingana na Shirika la Takwimu la Taifa la Zimbabwe.

Familia zinapaswa kuchagua kati ya kununua bidhaa za usafi wa Wanawake na kununua chakula na nyingi zikiamua kununua chakula huku wakitafuta njia mbadala.
Screenshot_20220713-045957_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia leo ameshiriki maadhimisho ya Mkutano wa 20 wa AMECEA katika ukumbi wa JNICC ambapo amewakumbusha Watanzania kuhusu umuhimu wa kuhifadhi mazingira akisema kuna maradhi mapya ambayo huko nyuma hayakuwepo lakini kwasababu ya uharibifu wa misitu viumbe ambavyo vilipaswa kubaki misituni sasa vinasambaa kwa Wanadamu.

“Kuna kila aina ya maradhi mapya yanazuka ambayo hatuyajui, nilikuwa nazungumza na Waziri Mkuu juzi ametoka ziara kule Mikoa ya Kusini, Lindi ameniambia ameona kuna maradhi mapya yameingia, Wanadamu wanatokwa tu damu puani na wanadondoka”

“Hatujui ni kitu gani ila Wanasayansi na Wataalamu wa Afya wote wamehamia huko wanaangalia ni kitu gani?, kwanini Mwanadamu atokwe tu na damu za pua adondoke, angekuwa mmoja wawili tungesema Presha imepanda vein zimepasuka anatokwa damu za pua lakini ni wengi kwa mfululizo ni maradhi ambayo hatujawahi kuona”

“Yote ni kwasababu tunaharibu makazi ya viumbe kule walikoumbwa na Mungu, tunawasogeza kwetu wanatuletea aina yote hiyo ya maradhi”
Screenshot_20220713-050103_OGInsta%2B.jpg
 
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa masikitiko imetoa taarifa ya kifo cha Mtoto Neema ambaye alitenganishwa na mwenzake Rehema, Neema amefariki Jumapili ya tarehe 10 Julai saa 3 asubuhi.

“Akiwa ICU hali yake ilibadilika ghafla, Madaktari walijitahidi kurudisha hali yake bila mafanikio na hatimaye kupoteza maisha, tuendelee kumwombea Rehema ambaye bado yupo ICU ili Mwenyezi Mungu amjalie afya njema, Bwana alitoa na Bwana ametoa, jina lake lihimidiwe sana”

Upasuaji wa kuwatenganisha Watoto waliokuwa wameungana (Neema na Rehema) ulifanyika July 01,2022 kwa mafanikio katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambapo Jopo la Wataalamu 31 walitumia saa saba kukamilisha upasuaji huo.

Watoto hao mapacha wawili wenye umri wa miezi tisa walizaliwa wakiwa wameungana sehemu ya kifua na tumbo na kwa upande wa umbo la ndani wameungana ini ila kila Mtoto ana ini lake.

Tanzania imekuwa nchi ya tatu Barani Afrika kufanya upasuaji wa aina hii baada ya Afrika ya Kusini na Misri.
Screenshot_20220713-050205_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Nishati, January Makamba ameendelea na ziara yake ya siku 21 kuzunguka kijiji kwa Kijiji na kufanikiwa kufika kwa Wajasiriamali wa kukaanga dagaa waliopo Musoma Mkoani Mara.

Akizungumza na Mwakilishi wa Kikundi cha KUSAMA kinachojishughulisha na kazi ya ukaangaji wa daga kwa kutumia nishati ya kuni na Mkaa wilayani Musoma, Makamba amewaelimisha Wanakikundi hao madhara ya Kiafya na Kimazingira ya muda mrefu ya kutumia kuni na mkaa ambapo Kwa Mkoa wa Mara, Watu kati ya 400- 600 kwa mwaka huugua magonjwa mbalimbali kutokana na athari za Moshi wa kuni na mkaa.

Mara baada ya kumaliza kuwaelimisha, Makamba amekiahidi Kikundi hicho kuwafungia mfumo wa gesi ya kupikia ili wafanye shughuli hizo kwa kutumia nishati safi na salama zaidi kwa afya yao.

Aidha asubuhi ya jana Waziri wa Nishati alifika ofisi za CCM Mkoani Mara kabla ya kuanza kufanyia kazi vijijini kwa siku 21, Mikoa 14, wilaya 38.
Screenshot_20220713-050323_OGInsta%2B.jpg
 
MOROCCO SITAKI KUPASIKIA - MSUVA

[emoji860] “Morocco [emoji1173] sitaki hata kupasikia. Kiukweli siwezi na sitaki kurudi tena Morocco. Ni mtu mmoja tu amesababisha mimi nipachukie Morocco ambaye ni Rais wa Wydad Casablanca. Ilifika steji wakafunga akaunti zangu za benki” [emoji51]

- Simon Msuva.[emoji1241]
Screenshot_20220713-050625_OGInsta%2B.jpg
 
“Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji ( EWURA) wameweka masharti mbalimbali ya uwekaji wa vituo vya mafuta lakini kama Serikali tumeona masharti ya vijijini na mijini yatofautiane hivyo kwa sasa wanarekebisha kanuni ili ziendane na mazingira ya vijijini, pamoja na marekebisho ya kanuni, Serikali imelegeza masharti ya uwekezaji vijijini kwani kwa mjini mtu anatakiwa awe na hati inayotambulika rasmi lakini kwa vijijini kinachohitajika ni Muhtasari tu wa kijiji, Ada ya leseni kwa vituo vya vijijini ni nafuu kwa kuwa ni sh. Laki Moja kwa miaka 5 huku mjini ikiwa ni milioni Moja kwa miaka 5. Pia masharti ya ujenzi yamerahishiwa kuliko mjini ambapo ukiwa na milioni 40 unaweza kujenga kijijini lakini kwa mjini itahitajika takriban milioni 200 hadi 300."

- JANUARY MAKAMBA, WAZIRI WA NISHATI, BUNDA-MARA.
Screenshot_20220713-050820_OGInsta%2B.jpg
 
[emoji383] WANAOLIPWA KIBOSI SERIE A (mwaka)
.
1. Matthijs de Ligt - Juventus, £ 10.1m
2. Alexis Sanchez - Inter Milan, £8.4m
3. Adrien Rabiot - Juventus, £ 7.6m
4. Romelu Lukaku - Inter Milan, £ 6.3m
5. Paul Pogba - Juventus, £ 6.3m
6. Dusan Vlahovic - Juventus, £ 5.9m
7. Angel Di Maria - Juventus, £ 5.9m
8. Aaron Ramsey - Juventus, £ 5.8m
9. Lautaro Martinez - Inter Milan, £ 5.2m
10. Kalidou Koulibaly - Napoli, £ 5m
Screenshot_20220713-051120_OGInsta%2B.jpg
 
[emoji981] SURE BOY HAHOFII SAJILI MPYA YANGA
.
“Sina hofu yoyote kwa ujio wa mastaa hao zaidi unanipa morali ya kupambana zaidi, uwezo nilionao ukichanganya na uzoefu wa ligi sina sababu ya kuhofia usajili unaoendelea, nina imani na kipaji changu,”
.
“Naheshimu sajili zote, naamini utakuwa chachu ya kufanya vyema na bora kwetu. Kuhusu kucheza, kila mmoja ana umuhimu wake kwa nafasi yake. Nina uhakika wa kucheza najiamini nina kipaji, nimetoka Azam FC vikosi vingi vilipangwa wakiniondoa lakini nimetua nimecheza,”
Screenshot_20220713-051600_OGInsta%2B.jpg
 
SIMBA RASMI KAMBI MISRI
.
Uongozi wa klabu ya Simba SC [emoji881] umetangaza rasmi kuweka kambi nchini Misri [emoji1093] katika mji wa Ismailia kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya.
.
Simba inatarajia kuondoka nchini Julai 14 na kurejea nchini Agosti 05.
Screenshot_20220713-051904_OGInsta%2B.jpg
 
Back
Top Bottom