Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20220619-073505_Opera%20Mini.jpg
 
Mgombea Urais kwenye Uchaguzi Mkuu wa Kenya August 2022 Profesa George Wajackoyah wa Chama cha Roots chenye kauli mbiu ya 'tingiza mti' amesema iwapo Wakenya watamchagua kuwa Rais ataruhusu Wananchi kulima bangi na ndio njia rahisi ya kumaliza tatizo la ajira.

"Bangi gunia moja ni dola milioni 3 za Kimarekani (Tsh. Bilioni 6.9, Ksh. milioni 352) gunia moja la maharage ni shilingi elfu sita za Kenya (Tsh. laki moja na elfu kumi na tisa), sasa ukiwa na bangi kwako ukaweza kuuza gunia moja utakuwa na shida gani nyingine?"

Interview nzima ya Profesa tayari ipo kwenye YouTube ya millardayo, bonyeza link kwenye bio yangu hapa Instagram kwenda kuicheki moja kwa moja ucheke ujifunze na uchukue madini ya Profesa.
Screenshot_20220620-042103_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia leo amezindua Mwanamke Initiative Foundation (MIF) visiwani Zanzibar ambapo amesema kuna haja ya Walimu wapya kupewa muda wa kupimwa utendaji kazi wao kabla ya kupewa ajira za kudumu.

“Mnaajiri Walimu 4000 katika mwaka ujao wa fedha, chukueni walimu wenye sifa, chukueni wale ambao wameshaanza kuonesha uwezo wao kwenye kujitolea lakini pendekezo langu Walimu mkiwasainisha mkataba kwamba huyu ana ajira ya maisha anakuwa hana haja ya kujihangaisha akaongeza uwezo wake wa kufanya kazi anajua nitakwenda Shule kuuza visheti, kufundisha Watoto, mshahara wangu upo tu”

“Mkiwawekea vipindi labda hutopata confirmation (uthibitisho wa ajira) mpaka labda baada ya miaka mitatu ya ualimu wako na mkawa mnawapima wale ambao hawatofanya vizuri wakatoka, Walimu watajituma na watafanya kazi vizuri”

“Hivi tunavyokwenda nikisainishwa kazi ya ualimu ndio kazi ya maisha mpaka nistaafu Walimu hawatojituma naomba sana muwe na vipimo, mfanyie kazi hili”
Screenshot_20220620-042224_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia leo amezindua Mwanamke Initiativea Foundation (MIF) visiwani Zanzibar ambapo amesema Watu wanaopewa fursa ya kuchaguliwa kusomea ualimu wanapaswa kuwa wale waliofaulu vizuri darasani na sio wenye ufaulu mdogo ambao wamekosa pa kukimbilia.

Rais Samia amesema “Miaka ya katikati hapa tulikuwa tunachukua Walimu tu kwasababu, Walimu mlioko hapa mtanisamehe, tulikuwa tunachukua Walimu wale ambao darasani alikuwa wa 20 au wa 30 kamaliza Shule hakupata kuendelea (hakufaulu), hakuna kazi nyingine, suluhisho kazi ilikuwa ualimu, kumbe ilikuwa tunaua elimu yetu”

“Mwalimu alitakiwa yule ambaye alikuwa na ufaulu mzuri darasani ndiye awe Mwalimu, Mwalimu awe amefaulu zaidi katika masomo yake (Sio yule ambaye hajafaulu vizuri kisha amekosa pa kukimbilia)
Screenshot_20220620-042935_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Urusi Vladimir Putin amewahimiza Wafanyabiashara wakubwa hususani Raia wa Urusi kuwekeza katika uchumi wa Urusi ili wasipoteze Mamilioni ya dola katika nchi za Magharibi, Putin amesema licha ya vikwazo vinavyowekwa kwa nchi ya Urusi bado thamani ya pesa ya Urusi (ruble) ipo juu dhidi ya dola.

Putin amesema Wafanyabiashara hao wanapaswa kuwekeza nchini mwao kwa maslahi ya Taifa na kwa mustakabali wa Watoto wao, tayari Wafanyabiashara kadhaa wakubwa waliondoka Urusi, kwa mfano, Oleg Tinkov, Wataalamu wanaamini kuwa zaidi ya Mamilionea Elfu 15 wa dola wanaweza kuondoka Urusi ifikapo mwishoni mwa mwaka 2022.

Putin amesema “Matukio ya hivi majuzi ikiwemo pesa ya Urusi kupanda thamani yamethibitisha kile nilichosema hapo awali ni salama zaidi kuwekeza nyumbani, wale ambao hawakuitikia wito huu wa wazi wamepoteza mamilioni katika nchi za Magharibi”

Itakumbukwa miezi miwili baada ya thamani ya ruble kushuka hadi chini ya senti moja ya Marekani huku kukiwa na vikwazo vikali vya kiuchumi katika historia ya kisasa, sarafu hiyo ya Urusi ilileta mabadiliko makubwa Mwezi uliopita ambapo ruble iliruka 40% dhidi ya dola tangu mwezi Januari.
Screenshot_20220620-043222_OGInsta%2B.jpg
 
Polisi wa Brazil wamesema mabaki ya moja ya miili miwili iliyopatikana kwenye msitu wa Amazon ni ya Mwandishi wa Habari wa Uingereza Dom Phillips, Polisi wamesema mabaki hayo yalibainika kutokana na rekodi za meno.

Mwili wa pili unaaminika kuwa ni wa Mtaalamu wa asili ya Bruno Pereira na bado unachunguzwa, Phillips (57) na Pereira (41) waliripotiwa kutoweka tarehe June 05, mapema wiki hii, Mshukiwa alikiri kuzika miili hiyo.

Mshukiwa huyo baadaye aliitajwa kama Amarildo da Costa de Oliveira, Polisi walisema alikuwa ameeleza kwa kina jinsi alivyowaua Watu wote wawili kabla ya kuwaongoza Maafisa mahali ambapo miili yao ilizikwa.

Kaka wa mshukiwa huyo, Oseney da Costa de Oliveira, pia amekamatwa kuhusiana na mauaji hayo lakini anakanusha kuhusika kwa vyovyote vile, siku ya Ijumaa Polisi walitangaza kuwa wametoa hati ya kukamatwa kwa mshukiwa wa tatu, Jeferson da Silva Lima, ambaye kwa sasa hajulikani aliko.
Screenshot_20220620-043316_OGInsta%2B.jpg
 
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO, Jens Stoltenberg ameonya kuwa vita ya Urusi nchini Ukraine inaweza kuendelea kwa miaka mingi na mataifa ya magharibi hayapaswi kurudi nyuma katika kuisaidia Ukraine.

Stoltenberg amesema nchi za Jumuiya ya NATO ni lazima zijitayarishe na ukweli kuwa vita nchini Ukraine inaweza kudumu kwa muda mrefu na ni muhimu kuendelea kuipatia msaada Ukraine.

Amesema kuipatia Ukraine msaada wa silaha kutatanua nafasi ya vikosi vya nchi hiyo kulikomboa jimbo la mashariki la Donbas ambalo limeangukia mikononi mwa Urusi.

Kiongozi huyo pia amesema mkutano wa wakuu wa nchi wa Jumuiya ya NATO utakaofanyika mjini Madrid baadae mwezi huu, unatarajiwa kufikia makubaliano ya kuisaidia Ukraine kuboresha zana zake za vita na kuachana na zile za enzi ya dola ya kisovieti
Screenshot_20220620-043418_OGInsta%2B.jpg
 
Back
Top Bottom