Raia wa kawaida na Wanajeshi wa Taiwan wameendelea kushiriki mazoezi ya kijeshi na kutumia silaha ikiwa ni sehemu ya kujiandaa na kujilinda dhidi ya tishio la vita kufuatia mgogoro unaoendelea kati ya China na Taiwan ambayo inaungwa mkono na Marekani.
Wiki chache zilizopita Rais wa Marekani Joe Biden aliionya China kuhusu Taiwan lakini China kupitia kwa Waziri wake wa Ulinzi, Jenerali Wei Fenghe ikapingana vikali na Marekani “Naomba niweke wazi hili ikiwa kuna Mtu atathubutu kuitenga Taiwan kutoka China, hatutasita kupigana, tutapigana kwa gharama yoyote na tutapigana hadi mwisho, hili ni chaguo pekee kwa China,"
Rais wa Marekani Joe Biden ameiambia China kwamba inachezea hatari kwa kurusha ndege zake za kivita karibu na Taiwan na akaapa kuwa Marekani itakilinda Kisiwa cha Taiwan kijeshi iwapo kitashambuliwa.
Taiwan, ambayo inajiona kuwa Taifa huru, imedaiwa kwa muda mrefu na Uchina ambayo inaamini Taiwan ni Kisiwa chake lakini Taiwan pia inaihesabu Marekani kama Mshirika wake mkubwa, na Marekani ina sheria inayoitaka kusaidia kisiwa hicho kujilinda.
Kuongezeka kwa matamshi hayo kunakuja wakati China inazidi kutuma ndege za kivita katika eneo la ulinzi wa anga la Taiwan zikiruka safu yao kubwa zaidi ya mwaka mwezi uliopita tu wakati Amerika imetuma meli za wanamaji kupitia maji ya Taiwan.