Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20220620-051517_OGInsta%2B.jpg
 
TETESI UPDATE.

[emoji3578]kilichowapata Simba Kwa Adebayor huenda ikawatokea tena Kwa kiungo wa Horoya FC Morlaye Sylla ambaye taarifa za uhakika asubuhi hii zinasema Mabingwa wa ligi ya mabingwa Africa Wydad Casablanca wametuma ofa Yao ya kumtaka kiungo huyo.! Simba inaelezwa kinachochelewesha dili hili ni suala la pesa ikiwemo mshahara wa mchezaji huyo.
Screenshot_20220620-051909_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia leo amezindua Mwanamke Initiativea Foundation (MIF) visiwani Zanzibar ambapo amesema Watu wanaopewa fursa ya kuchaguliwa kusomea ualimu wanapaswa kuwa wale waliofaulu vizuri darasani na sio wenye ufaulu mdogo ambao wamekosa pa kukimbilia.

Rais Samia amesema “Miaka ya katikati hapa tulikuwa tunachukua Walimu tu kwasababu, Walimu mlioko hapa mtanisamehe, tulikuwa tunachukua Walimu wale ambao darasani alikuwa wa 20 au wa 30 kamaliza Shule hakupata kuendelea (hakufaulu), hakuna kazi nyingine, suluhisho kazi ilikuwa ualimu, kumbe ilikuwa tunaua elimu yetu”

“Mwalimu alitakiwa yule ambaye alikuwa na ufaulu mzuri darasani ndiye awe Mwalimu, Mwalimu awe amefaulu zaidi katika masomo yake (Sio yule ambaye hajafaulu vizuri kisha amekosa pa kukimbilia)View attachment 2266105
Kama wataanza kuchukua waliofaulu vizuri tu basi na waanze kuwalipa vizuri sasa hakuna visingizio tena
 
Back
Top Bottom