Makapuku Forum

Sasa Auntie hapa itakuwaje? Maana ndiyo mambo yako haya


Mimi nitabaki kwenye para langu hili hili....
 
KIUNGO YANGA NDO BASI TENA
.
Ikiwa imebakiza mechi nne tu kumaliza Ligi Kuu, Yanga imepata pigo baada ya kuumia kwa kiungo Zawadi Mauya
atakayekaa nje ya uwanja hadi msimu ujao.
.
Mauya aliumia goti kwenye mazoezi ya timu hiyo siku chache zilizopita yanayofanyika kambini kwao Avic Town, Kigamboni.
 
Boxer, Kaseke wote wajichomoa Yanga
.
Taarifa kutoka ndani ya Singida zimethibitisha nyota wawili wanaocheza Yanga, Deus Kaseke na Paul Godfrey ‘Boxer’ wamesainishwa mikataba ya miaka miwili kila mmoja.
.
Kwa mujibu wa kigogo mmoja wa Singida Big Stars amesema Boxer na Kaseke kila mmoja amesaini mkataba wa miaka miwili na tayari pesa zao za usajili wameshawekewa kwenye akaunti zao.
 
Chelsea Yatua kwa Sterling Kisa Lukaku
.
Chelsea ipo kwenye hatua nzuri ya kumuuza straika wao, Romelu Lukaku kwenda Inter Milan na tayari imeshaanza kutafuta mbadala wake kwa kuanza mazungumzo na wawakilishi wa straika wa Manchester City, Raheem Sterling ili kumsainisha katika dirisha hili.
.
Mkataba wa Sterling unamalizika mwaka 2023 na ameonyesha anahitaji kuondoka kwa sababu haoni ikiwa atapata nafasi kwenye kikosi cha kwanza kwa msimu ujao kutokana na maingizo mapya.
.
Msimu uliopita alionyesha kiwango bora akicheza mechi 47 za michuano yote, akafunga mabao 17 na kutoa asisti tisa.
 
VLAHOVIC AIZODOA ARSENAL
.
Straika anayekipiga Juventus, Dusan Vlahovic ameichimba mkwara Arsenal kuwa hakukaribia kujiunga na timu hiyo, kipindi cha usajili majira ya kiangazi mwaka jana, licha ya kuhusishwa.
.
“Mawazo yangu yalikuwa Juventus sio Arsenal. Sina kingine cha kusema. Najisikia furaha kujiunga na timu hii. Nina furaha ninapovaa jezi ya Juventus. Hakika nimefiti katika klabu hii. Unapokuja hapa hupaswi kukata tamaa, unatakiwa kucheza kwa juhudi kila wakati" amesema Vlahovic.
.
Awali, taarifa zilidai kuwa Arsenal ilionyesha nia ya kumsajili Vlahovic mwaka huu kwenye dirisha dogo, hata hivyo nyota huyo akaipiga chini ofa hiyo na kujiunga na Juventus.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…