

Farhan Jr
Kwanza kabisa pongezi kwako Mpiga picha @kasanga04 , nipo tayari kumuamini Mpiga picha kuliko Binadamu yoyote kwakuwa ni mkweli na anachokupa ni ukweli ulivyo pasipo kificho
Nivute kiti nikae mimi Farhan mwana wa Kihamu, nanukuu maneno ya Ansel Adams alisema “When words become unclear, I shall focus with photographs. When images become inadequate, I shall be content with silence”
Kuna wakati maneno pekee hayaelezeki, usimalize maneno kaa kimya tafakari na kuzifikiria zaidi picha, itafika siku maudhui yatakwisha ila Mpigapicha atakuwa Maudhui
Picha hii ikukumbushe Mwanangu mtaani, ofisini au majumbani usirithi ugomvi usioujua, usirithi vita ambavyo hujui chanzo chake na fahamu unaona padogo sana, ila wapo wanaotumia darubini kuona mbali
Mwijaku anaishi kwenye falsafa makini ya maisha, namkumbuka Askofu wetu aliwahi kusema “If opportunity doesn't knock, build a door.” Alinukuu maneno ya Milton Berle, ndio! Kama hakuna fursa inagonga mlango basi weka mlango
Mwijaku alimaliza kila maneno kuhusu Naseeb mwana wa Sandra, lakini ndio hesabu za maisha, hakuiona fursa kwahiyo kwakuwa haigongi mlango akaweka mlango, akageuka almasi mchangani
Hesabu za kawaida za biashara za Mtu kama Diamond ni lazima uwe na watu kama Mwijaku kwenye bus lako, italeta attention sahihi, akagonga mlango na Mwijaku akafungua kwa roho nyeupe, that’s life
Picha hii utaipenda sana picha hii inatukumbusha hakuna Rafiki wa kudumu wala adui wa kudumu bali ni maslahi ya kudumu pekee, usisahau kanuni! Usirithi vita usiyoijua
Asante mpiga picha @kasanga04 nakuacha na hii “The best thing about a picture is that it never changes, even when the people in it do.”
Hata kama hao watu pichani watabadilika basi hii picha haitobadilika kamwe