Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mwamuzi raia wa Rwanda Salima Mukansanga atakuwa mwanamke wa kwanza kutoka barani Afrika kuchezesha fainali za kombe la Dunia nchini Qatar zitazofanyika November mwaka huu.
Screenshot_20220520-035921_OGInsta%2B.jpg
 
| DI MARIA JUVENTUS
.
Winga wa Paris St Germain na Argentina, Angel di Maria, 34, atajiunga na Juventus dirisha lijalo la majira ya kiangazi baada ya mkataba wake wa sasa kumalizika mwisho wa msimu huu.
.
Di Maria katika Ligi kuu ya Ufaransa msimu huu amefunga mabao 4 na Assist 6 katika mechi 25, haonekani kuwa na mpango wa kuongeza mkataba mpya na anataka kuondoka.
Screenshot_20220520-040131_OGInsta%2B.jpg
 
RASMI: Klabu ya ARSENAL wametambulisha jezi yao mpya ya nyumbani kwa msimu ujao wa 2022/23.
.
Kwa uzi huu unawapa BIG YES au BIG NO __?
Screenshot_20220520-040310_OGInsta%2B.jpg
 
DROGBA SHOO SHOO
.
Siku kama ya leo mwaka 2012, Chelsea inatwaa taji lake la kwanza la Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kuifunga Bayern Munich kwa penalti 4-3 baada ya dakika 120 kuisha kwa sare 1–1 iliyotokana na Thomas Müller kuifungia Bayern kipindi cha pili na DIDIER DROGBA kusawazisha dakika tano baadaye na mechi kwenda ‘extra time’ hadi penalti kwenye Uwanja wa Allianz Arena, Ujerumani.
Screenshot_20220520-040407_OGInsta%2B.jpg
 
Manchester City imezindua jezi yao mpya watakayotumia katika mechi za nyumbani msimu wa 2022/23.

Unawapa maksi ngapi?
Screenshot_20220520-040609_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Petr Cech anasema kuelekea fainali dhidi ya Bayern Munich, walikaa Makipa wote wa Chelsea! Yani yeye, Ross Turnbull na Hilario, pamoja na Kocha wa Makipa Christophe Lollichon

Walikaa kutazama penati zote za Bayern Munich kuanzia 2007 mpaka 2012 yani misimu mitano yote, wakizisoma penati zao kuanzia wapigaji na Makipa wao, kila taarifa muhimu waliinukuu kwa ajili yao na wapigaji wao

Ni kama waliota kwakuwa fainali hii ilikuwa na matuta sita jumla! Ambapo Chelsea walicheza matuta matatu, likiwemo lile la Arjen Robben dakika ya 105 tu

Cech aliwaambia wapigaji wote wa penati haswa wa mguu wa kushoto kuwa penati zote za wapigaji wa mguu huo basi Manuel Neur huwa anaruka upande wa kushoto hivyo namna pekee ni kupiga upande wa kulia, huwa hafuati, mara nyingi

Kwenye wapiga penati wa Chelsea usiku ule, wapjigaji wa mguu wa kushoto walikuwa Juan Mata na Ashley Cole! Hivyo walikuwa na taarifa hiyo muhimu kuhusu Manuel Neur

Bahati mbaya sana Juan Mata wakati anaenda kupiga licha ya kuwa na hiyo taarifa anasema alivyofika langoni aliamini Neur angeruka kulia hivyo akapiga kushoto, ambapo Neur alisafiri kweli na akaicheza penati ile

Mpigaji wa pili wa mguu wa kushoto alikuwa Ashley Cole ambaye nae alichagua kuiweka penati upande wa kushoto ambapo Neur alisafiri kweli na aliipangusa, bahat nzuri tu ni kuwa Cole alipiga jiwe haswa ikazama

Cech aliicheza penati ya Bastian wa Munich, anasema wakati wanazisoma penati za Bayern waligundua Bastian kwenye penati tano za mwisho kabadili style ya upigaji, hakai mbali na hakai karibu anajiposition kati kati

Hivyo Cech alifahamu Bastian atasita kisha ataupiga mpira kidogo sana, hivyo akachagua kumsubiri na akasafiri na mpira ule na kuicheza ile penati, hivyo kazi ikabaki kwa KING DD kumaliza mchakato

Drogba aliambiwa na Makipa kuhusu Neur na wapigaji wa mguu wa kushoto, hivyo akaigusa tu upande wa kulia wa Neur nae akaenda kushoto na kupotea kabisa! Chelsea tukashinda kwa penati

YEEES hivi ndivyo watu hushinda mechi, ichukue hii ilete kwenye maisha ya kawaida! Lazima uwekeze kwenye muda, ujitese kisha upate matunda’! Imagine kukesha na penati za Bayern kwa miaka mitano yote! Just imagine
Screenshot_20220520-041452_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Napata tabu sana kuiandikia hii fainali ya Ulaya 2012, ambapo Chelsea tunachukua ubingwa wa UEFA mbele ya Bayern Munich

Katika uandishi wangu nimeiandika hii mara moja tu, kila nikiandika napata kumbukumbu za furaha na kilio, kwakuwa sio tu kumbukumbu ya mpira bali ya maisha yangu

Nilianza kushabikia Chelsea 2004, nikiwa na umri wa miaka sita! Alienifanya niipende hii timu ni Baba angu mdogo ambaye leo hii hatujui kama yupo hai au amekufa, alipotea tu ghafla

Tuliipenda sana hii timu na Rafiki yangu ambaye yeye alifariki mwaka mmoja kabla ya huu usiku wa Ulaya, hakuweza kushuhudia hii fainali, nilitamani sana angekuwepo lakini mapenzi ya Mungu ni makubwa zaidi na atakalo litimie

Usiku wa hii fainali nilikuwa kidato cha pili, Mjomba wangu alikuja kunichukua nyumbani tukatazame fainali kwakuwa kijijini sio rahisi usiku kutembea peke yangu, Mjomba ambaye nae ni Marehemu kwasasa

Njiani tunakata misitu ananipa masimulizi ya wakina Gianfranco Zola ndani ya Chelsea, ananielezea kuhusu Chelsea kabla ya Roman Abramovich, huku akinihakikishia Chelsea tunaenda kuweka historia

Anko alikuwa Chelsea wa kutupwa, mdogo wa Mama Farhan wa kwanza! Kutokana na wingi wa watu, Anko aliniweka mabegani kipindi chote cha pili ili nitazame hii fainali

Nakumbuka KING DD akitupa nafasi ya kuziishi ndoto, kile kichwa dakika ya 88! Nakumbuka dakika 120 za jasho na damu bila Ramires, bila Captain Terry ila Marehemu mjomba alikuwa ananipa moyo

Yes I survived to tell the tale, nilishuhudia TIMU NAMBA MOJA KABISA moyoni mwangu ikitwaa ubingwa wa Ulaya!

The night we defied the odds, the night Legends where made, the night we made our mark in European football history

Kwangu Chelsea ni zaidi ya maisha, kwangu hii fainali ni zaidi ya furaha na maumivu, huwa sipendi sana kuizungumzia kwakuwa imebeba machozi mengi sana kwangu
Screenshot_20220520-041633_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

DAVID KAMETA ‘DUCHU’ TRANSFER UPDATES

-Ikiwa amesalia na miezi sita ya mwisho ya mkataba wake na Simba, beki kijana David Kameta amezivutia klabu kubwa mbili nchini Tanzania ambazo zinaiwinda saini yake

-Taarifa za uhakika ni kuwa Makocha wa timu zote mbili wamependekeza jina la mbavu hiyo ya kulia ambaye anacheza kwa mkopo Geita Gold akitokea Simba

- Tarehe za katikati mwa mwezi April na mwanzoni mwa mwezi Mei klabu zote mbili zilifanya mazungumzo ya kuhitaji huduma yake, huku yeye akisema wazi anahitaji muda mpaka mwishoni mwa msimu

-David amekuwa kwenye kiwango bora sana kwasasa, huku ikitarajiwa mwishoni mwa msimu akae mezani na waajiri wake ambao ni Simba kuamua hatma yake, uwezekano mkubwa kama ataachwa ni kujiunga na miamba hiyo miwili

-One of the right backs with great potential

The summer transfer window has just started, lets march together
Screenshot_20220520-042511_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

LUIS MIQUISSONE TRANSFER UPDATES

-Wakala wa Luis na Mchezaji wake bado wamewekeza muda na nguvu yao kwenye klabu ya Al Ahly, wote wakiamini muda utafika wa Kondeboy kuingia kikosini na kujihakikishia namba

-Baada ya kufuatilia kwa umakini sana mpaka sasa ni klabu moja tu imeulizia huduma ya nyota huyo, nao ni RS BERKANE ya Morocco iliyo chini ya Kocha Florent Ibenge, kwakuwa anamfahamu nyota huyo

-Kuhusu ofa na mshahara ni kuwa Berkane wapo tayari kutoa zaidi ya kile ambacho Ahly wanampa kwasasa, hivyo inasalia kwa Mchezaji, Ahly na wakala wake kuamua

-Kikubwa kwasasa ni kuwa Ahly wamefocus na michuano ya Afrika na Ligi, mchakato wowote wa Kondeboy utatazamwa mwishoni mwa msimu

-Hakuna mawasiliano yoyote kati ya Simba na Al Ahly juu ya huduma ya Mchezaji huyo mpaka sasa, Simba wapo mawindoni Kusini na Magharibi mwa Afrika kwasasa

- The Kondeboy transfer updates will proceed incase of any possible change, but as it stands he is commited to Ahly

The summer transfer window is just getting started
Screenshot_20220520-042619_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom