Makapuku Forum

Makapuku Forum

Rais Samia anatarajia kufanya ziara ya Kiserikali ya siku mbili Uganda kuanzia leo May 10 - May 11 kwa mwaliko wa Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.

Hii itakuwa ni ziara ya kwanza ya Kiserikali nchini kufanywa na Rais Samia tangu Serikali ya awamu ya sita iingie madarakani March 2021.

Madhumuni ya ziara ni kudumisha na kuimarisha zaidi historia ya mahusiano na kidiplomasia na ushirikiano wa kiuchumi na kijamii kati ya nchi hizi mbili.View attachment 2219443
Mama tena???
 

Auntie nikiona habari za mama ako inanijia picha yako hivi uliangalia royal tour na mama na uncle peter aka baba wa kambo.

Auntie niache.. nimecheka sana ujue..

Ni kile kipande Mama yupo na Peter, Wameshikana mikono wanatembea ndiyo kilinifanya nipate hamasa ya kuangalia...Wabongo hicho kipande wamejua kunichekesha jamani Wanakuambia Peter anampeleka Mama yetu Majanini kumfanyaje?

Ila Huwezi kuamini sijaweza kuangalia yote... Uvivu
 
Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mkoa wa Kagera, Toba Nguvila ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama katika Wilaya hiyo kuwakamata na kuwachukulia hatua za kisheria wote wanaodaiwa kuchoma moto gari la Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Nyamilanda wilayani humo, Emmanuel Sheiza nyumbani kwake.

Nguvila alitoa agizo hilo jana Mei 9, 2022 alipotembelea eneo la tukio na baadaye kuongea na wanakijiji wa kitongoji cha Nyamilanda na kuelezea masikitiko yake.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia jana ambapo watu wasiofahamika walichoma moto gari la Hakimu huyo ambaye anaishi kwenye nyumba za Mahakama zilizopo jirani na Mahakama ya Mwanzo Nyamilanda.

Mkuu wa Wilaya huyo amesema "Tayari tukio hili la kusikitisha limesharipotiwa katika vyombo vya ulinzi na usalama na uchunguzi unaendelea ili kuwakamata wahusika wote na hakuna hata mmoja atakayekwepa mkono wa chuma wa sheria"View attachment 2219431
....suala hapa ni kutoa hukumu za haki na zinazoonekana kuwa za haki. Kinyume chake utakutana na haya au zaidi. Nakumbusha tu wenye dhamana ya kuamua mambo
 
Rais Samia anatarajia kufanya ziara ya Kiserikali ya siku mbili Uganda kuanzia leo May 10 - May 11 kwa mwaliko wa Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.

Hii itakuwa ni ziara ya kwanza ya Kiserikali nchini kufanywa na Rais Samia tangu Serikali ya awamu ya sita iingie madarakani March 2021.

Madhumuni ya ziara ni kudumisha na kuimarisha zaidi historia ya mahusiano na kidiplomasia na ushirikiano wa kiuchumi na kijamii kati ya nchi hizi mbili.View attachment 2219443
...duh, mama hatulii !!! Kakaa karibu wiki mbili nje kuzindua filamu, ofisi inaweza kuwa popote zama hizi lakini urais sio wa kufanyia popote
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom