Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20220510-202830_OGInsta%2B.jpg
 
Imeandikwa na @swalehmawele

Ngoja niwaambieni kitu, mnaiona Azam? mnadhani ni timu ambayo inaweza kuwatingisha Simba na Yanga katika mbio za ubingwa? mnadhani Simba akitaka ubingwa anaifikiria Azam kama kikwazo? mnadhani Yanga akiutaka ubingwa anaifikiria Azam kama kikwazo? wanafikiriana wao kwa wao, Yanga anaamini akiwa juu ya Simba bingwa atakuwa yeye na hivyohivyo kwa Simba.

Twende hapa, kinachowafanya Simba na Yanga watambe katika soka la Tanzania ni wachezaji wa kigeni, yes, wachezaji wa kigeni ndo wanaoleta utofauti mkubwa ukiwalinganisha na wazawa wengi, wachezaji wazawa kwa asilimia kubwa ndio walewale wanaopatikana katika klabu za Mbeya City, Kagera Sugar, KMC na klabu nyingine, hakuna utofauti mkubwa wa uwezo baina yao.

Hii Yanga ya sasa asilimia kubwa ya wachezaji walioleta utofauti ni wachezaji wa kigeni, wale akina Bangala, Mayele, Djigui, Djuma na wengine ndio walioleta utofauti, ukichanganya na quality ya akina Bakari, Nondo na wengine Yanga inakuwa pale, hivyohivyo kwa Simba, asilimia kubwa wachezaji wa kigeni ndio walioleta utofauti ukichanganya na quality ya wazawa wachache.

Maana yangu ni hii, wachezaji wa kigeni wa Azam wengi hawaleti utofauti, hawawi chachu ya kubusti quality ya wachezaji wazawa ili kuipeleka timu katika levo fulani, tatizo la msingi linaanzia hapo, Azam inafelishwa sana na jambo hilo, yes inaweza kuwa ngumu kubeba ubingwa mbele ya Simba na Yanga lakini mkawa timu yenye ushindani hasa na itakayokuwa ngumu kudondosha alama.

Asante.
Screenshot_20220510-203017_OGInsta%2B.jpg
 
Manchester City imethibitisha kuwa tayari wamefikia makubaliano kimsingi na Borussia Dortmund kwa uhamisho wa mshambuliaji Erling Haaland kuanzia tarehe 1 Julai 2022.
Uhamisho huo unabaki chini ya City kukamilisha masharti na mchezaji huyo.
Screenshot_20220510-203750_OGInsta%2B.jpg
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara linawashikilia Watu wawili na kumtafuta mwingine mmoja kwa tuhuma za kumbaka kisha kumuua Elizabeth Steven Peter (41) Mkazi wa Kijiji cha Mkajamila Wilayani Masasi.

"May 06,2022 katika Kituo cha Polisi Wilaya ya Masasi kuliripotiwa tukio la kukutwa mwili wa Elizabeth mtaa wa Mkunguni Kata ya Migongo baada ya uchunguzi ilibainika alibakwa kisha kuuawa kwa kuvunjwa mifupa ya shingo"

"Polisi walianza upelelezi kupitia Wataalamu wa Cyber na kumkamata Innocent Ndomba (32) ambaye alikiri kuhusika na tukio kwa kushirikiana na Mume wa Marehemu Deograthias John (32) ambaye anashikiliwa pia na Polisi"

"Watuhumiwa wameleeza kuwa chanzo cha tukio ni wivu wa kimapenzi baina ya Marehemu na Mumewe ambapo inadaiwa Marehemu alikuwa akimroga Mumewe pamoja na kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Wanaume wengine"
Screenshot_20220510-204243_OGInsta%2B.jpg
 
Mahakama ya kikatiba ya Uganda imemtaka Mtoto wa Rais Yoweri Museveni, Luteni Jenerali Muhoozi Kainerugaba, kujibu shtaka analotuhumiwa nalo la kueleza nia yake ya kuwania urais akiwa bado anahudumu katika jeshi la nchi hiyo.

Wakili wa haki za binadamu Gawaya Tegulle aliiomba mahakama katika mji mkuu, Kampala, kumzuia Jenerali Kainerugaba kufanya shughuli za kisiasa akiwa bado anatumikia jeshi.

Gawaya pia anataka jenerali huyo afunguliwe mashtaka ya uhaini kufuatia madai yake ya njama ya kumrithi babake kwa kutumia mbinu haramu, Jenerali Kainerugaba, Kamanda wa Jeshi la Nchi Kavu la Uganda ana siku 10 kuwasilisha majibu yake.

Mnamo tarehe 2 Mei, alitangaza mipango ya kuzindua mpango wa kisiasa, na kuchochea uvumi kwamba alinuia kumrithi babake wa muda mrefu.

Mnamo Machi 8, alitangaza kustaafu Jeshi kwenye Twitter lakini Rais Museveni alikataa, Rais Museveni amekanusha kumuandaa Mwanae kuchukua wadhifa wake.
Screenshot_20220510-204354_OGInsta%2B.jpg
 
Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mkoa wa Kagera, Toba Nguvila ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama katika Wilaya hiyo kuwakamata na kuwachukulia hatua za kisheria wote wanaodaiwa kuchoma moto gari la Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Nyamilanda wilayani humo, Emmanuel Sheiza nyumbani kwake.

Nguvila alitoa agizo hilo jana Mei 9, 2022 alipotembelea eneo la tukio na baadaye kuongea na wanakijiji wa kitongoji cha Nyamilanda na kuelezea masikitiko yake.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia jana ambapo watu wasiofahamika walichoma moto gari la Hakimu huyo ambaye anaishi kwenye nyumba za Mahakama zilizopo jirani na Mahakama ya Mwanzo Nyamilanda.

Mkuu wa Wilaya huyo amesema "Tayari tukio hili la kusikitisha limesharipotiwa katika vyombo vya ulinzi na usalama na uchunguzi unaendelea ili kuwakamata wahusika wote na hakuna hata mmoja atakayekwepa mkono wa chuma wa sheria"
Screenshot_20220510-204448_OGInsta%2B.jpg
 
Spika wa bunge Dr. Tulia Ackson ametoa onyo kwa Wabunge kutodharau na kutweza michango ya Wabunge wenzao bali Wabunge wote waheshimiane na kama Mbunge hakubaliani na mchango wa mwenzake aseme ndani ya Bunge kwa kutoa taarifa maana kanuni zinawaruhusu na haiiruhusiwi kutoka nje na kwenda nje kutweza mchango wa Mbunge mwingine.

Onyo la Spika Dr. Tulia limetoka baada ya Mbunge wa Viri Maalum Dr.Tea Ntala kuomba mwongozo wa Spika kuhusu kauli ya Mbunge wa Sengerema Hamisi Tabasamu aliyoitoa Jana May 9, 2022 kwenye vyombo vya habari ikidaiwa amemdhihaki na kumshambulia Mbunge wa jimbo la Momba Condester Sichwale aliyekuwa bungeni na chupa za pombe akiiomba Serikali kurasimisha pombe za kienyeji ili ziwasaidie Wananchu kuwainua kiuchumi.
Screenshot_20220510-204609_OGInsta%2B.jpg
 
Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un ametuma salamu za pongezi kwa Rais Vladimir Putin baada ya kusherehekea siku ya ushindi ya Urusi, akielezea mshikamano thabiti wa nchi yake na Urusi, shirika la habari la Korea Kaskazini KCNA limeripoti.

Katika barua yake iliyotumwa Urusi tarehe 9 Mei, Kim anasema "Mshikamano madhubuti wa muda mrefu kwa sababu ya Watu wa Urusi kung'oa vitisho vya kisiasa na kijeshi na usaliti wa vikosi vya adui"

Kim amesema imani yake ni kwamba uhusiano wa kimkakati na wa jadi wa urafiki kati ya nchi hizo mbili utakuwa kwa kasi".

Hivi karibuni Korea Kaskazini imeangazia uhusiano wake wa karibu na Urusi, na kuunga mkono hadharani Urusi juu ya uvamizi wake nchini Ukraine, mwezi Februari, ililaumu mzozo wa Ukraine juu ya sera ya kivita ya Marekani na Magharibi.
Screenshot_20220510-204749_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Ukraine Vladimir Zelensky amemtunuku tuzo ya heshima ya Rais mbwa aliyepewa jina Pattern kwa huduma zake tangu uvamizi wa Urusi.

Mbwa huyo mwenye umri wa miaka miwili na nusu amekuwa shujaa wa kitaifa nchini Ukraine, ishara ya upinzani wa Ukraine dhidi ya Urusi, mbali na kubaini marundo zaidi ya 200 ya nyaya zinazohusishwa na vilipuzi, mwezi April alitajwa kugundua mabomu zaidi ya 90.

"Ninataka kuwatunuku mashujaa hawa wa Kiukreni ambao tayari wanasafisha ardhi yetu, mbwa huyu sio tu anasaidia kubaini vilipuzi, lakini pia hufundisha watoto wetu kanuni muhimu za usalama katika maeneo ambayo kuna hatari"

Sherehe ya tuzo hiyo pia ilihudhuriwa na Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau, ambaye aliwasili Ukraine siku ya Jumapili, Justin Trudeau alitangaza kwamba Canada itatoa silaha zaidi na vifaa kwa Ukraine.

Rais Zelensky alikabidhi medali kwa mbwa huyo na mmiliki wake My Hello Ilyo, Mbwa huyo mdogo kiumbo amekuwa maarufu Ukraine chini ya kitengo cha usalama tangu uvamizi wa Urusi.
Screenshot_20220510-204912_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia anatarajia kufanya ziara ya Kiserikali ya siku mbili Uganda kuanzia leo May 10 - May 11 kwa mwaliko wa Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.

Hii itakuwa ni ziara ya kwanza ya Kiserikali nchini kufanywa na Rais Samia tangu Serikali ya awamu ya sita iingie madarakani March 2021.

Madhumuni ya ziara ni kudumisha na kuimarisha zaidi historia ya mahusiano na kidiplomasia na ushirikiano wa kiuchumi na kijamii kati ya nchi hizi mbili.
Screenshot_20220510-205040_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Nishati January Makamba leo Bungeni amesema Rais Samia ametoa maelekezo kwamba katika kipindi hiki kabla mwaka mpya wa fedha haujafika, Serikali ijibane na ijinyime na zitolewe shilingi bilioni 100 kwa ajili ya kupunguza bei za mafuta hapa nchini.

"Ruzuku hii inatolewa kwa kupunguza matumizi ya Serikali katika kipindi kilichobaki cha mwaka 2021/22, kutolewa kwa ruzuku hii hakutagusa miradi ya maendeleo ambayo inaendelea"

"Nafuu nyingine inayotokana na mikopo , itakuja katika mwaka ujao wa fedha itaelezwa kwa kina zaidi na Waziri wa Fedha kwenye Bajeti ya Serikali mwezi ujao"

"Ruzuku hii ya shilingi bilioni 100 itatolewa kwa ajili ya kupunguza bei kuanzia tarehe 1 Juni 2022, hii ni kutokana na kuwa Wafanyabiashara wa jumla wamekwisha lipia gharama ya mafuta ambayo imejumuishwa katika bei hizi za Mei 2022 na wafanyabiashara wa mafuta katika vituo wamekwishanunua mafuta kwa bei hii inayotumika sasa" ——— asema Waziri wa Nishati January Makamba.
Screenshot_20220510-205151_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Nishati January Makamba leo Bungeni ameeleza hatua mbalimbali ambazo zinachukuliwa na Serikali ya Tanzania sasa hivi ili kuhakikisha bei ya mafuta inapungua huku akisisitiza ——> “changamoto za foleni na vurugu katika vituo vya mafuta zilizopo katika nchi nyingine zinazotokana na uhaba wa mafuta"

"Pamoja na changamoto ya bei ambayo sio suala letu peke yetu, usimamizi wa sekta ya mafuta hapa nchini hasa katika kipindi hiki kigumu umekuwa wa utulivu na wa umakini ikiwa ni kwa jitihada za makusudi za Serikali kwa ushirikiano na sekta binafsi"

"Bei za mafuta kupanda ni janga lakini hatari kubwa zaidi hata kwa usalama wa nchi ni kukosekana kwa mafuta, hili halijatokea hapa kwetu na hatutaruhusu litokee, leo tunapozungumza tunayo petroli ya kutosheleza kwa mahitaji ya siku 34, dizeli ipo ya kutosheleza kwa mahitaji
ya siku 27, mafuta ya taa kwa siku 81 na mafuta ya ndege kwa siku 26"

"Haya ni mafanikio kwani sote tunafahamu kwamba zipo nchi zimelazimika kutaifisha mafuta ya nchi nyingine yanayopitia kwao kutokana na uhaba" asema Waziri January Makamba.
Screenshot_20220510-205243_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Nishati wa Tanzania January Makamba leo Bungeni amezitaja baadhi ya hatua ambazo Serikali imezichukua ili kupunguza bei ya mafuta Nchini ambapo miongoni mwa hatua zisizo za kifedha zilizochukuliwa ni pamoja na kuruhusu Watu wenye uwezo wa kuleta mafuta kwa bei nafuu kufanya hivyo.

“Wizara imekamilisha kufanya tathmini ya kampuni zote zilizoonesha nia ya kuweza kuleta mafuta kwa bei nafuu kwa lengo la kujiridhisha na uwezo wao wa kuleta mafuta hayo ili kuhakikisha uwepo wa mafuta nchini ambapo mipango hii ikileta matokeo yanayotarajiwa, bei za mafuta zitapungua zaidi kuanzia mwezi Agosti 2022"

"Serikali imeandaa utaratibu wa kuanzisha mfuko maalumu utakaotumika kupunguza makali ya bei ya mafuta kipindi ambacho bei hizo zinaongezeka kwa kiasi kikubwa, mpango wa kuanzisha mfuko huu uko katika hatua za mwisho za maandalizi na utakapokamilika, utawasilishwa katika Baraza la Mawaziri.

"Serikali inakamilisha marekebisho ya Kanuni za kuanzisha na kuendesha hifadhi mafuta ya kimkakati ili nchi yetu ijihakikishie usalama wa upatikanaji wa mafuta na unafuu wa bei katika vipindi kama hivi.

"Serikali inakamilisha makubaliano ya kujenga maghala makubwa ya kuhifadhi mafuta kwa ajili ya kuuzwa ndani na nje ya nchi kulingana na uhitaji, uwepo wa kituo hiki utawezesha nchi kupata mafuta yenye bei nafuu pale bei zinapopanda kupita kiasi, mpango huu na utekelezaji wake unaweza kukamilika katika kipindi cha miaka mitatu" asema Waziri January Makamba.
Screenshot_20220510-205335_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom